Aionian Verses
En vain ses fils se réunirent-ils avec ses filles, et vinrent-ils tous pour le consoler; il ne voulut point être consolé, disant: Je descendrai près de mon fils au sein de la terre en pleurant. Et le père de Joseph le pleura, (Sheol )
Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol )
Mais Jacob dit: Mon fils ne partira pas avec vous; son frère est mort, celui-ci seul m'est resté; une maladie le prendra dans le chemin où vous irez, et, de tristesse, vous ferez descendre ma vieillesse au sein de la terre. (Sheol )
Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol )
Si donc vous emmenez loin de moi celui-ci, et qu'une maladie le prenne en chemin, de tristesse, vous ferez descendre ma vieillesse au sein de la terre. (Sheol )
Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol )
Dès que notre père aura vu que l'enfant n'est pas avec nous, il mourra de douleur, et nous ferons descendre au tombeau la vieillesse de ton serviteur, notre père à nous. (Sheol )
akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol )
Mais le Seigneur va faire éclater un prodige, la terre ouvrira sa bouche; elle dévorera ces hommes, leurs familles, leurs tentes, tout ce qui leur appartient; ils descendront vivants sous la terre, et vous reconnaîtrez qu'ils ont irrité le Seigneur. (Sheol )
Lakini ikiwa Bwana ataleta jambo jipya kabisa, ardhi ikifunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na kila kitu kilicho mali yao, nao washuke chini kaburini wakiwa hai, ndipo mtafahamu kuwa watu hawa wamemdharau Bwana.” (Sheol )
Ils descendirent vivants sous la terre avec tout ce qui leur appartenait, et la terre les cacha, et ils furent détruits au milieu de la synagogue. (Sheol )
Wakashuka chini kaburini wakiwa hai, pamoja na kila kitu walichokuwa nacho; nchi ikajifunika juu yao, nao wakaangamia wakatoweka kutoka kusanyiko. (Sheol )
Le feu que mon courroux a allumé brûlera jusque sous la terre; il dévorera la terre et ses fruits, il dévorera les fondements des montagnes. (Sheol )
Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu, ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti. Utateketeza dunia pamoja na mazao yake, na kuwasha moto katika misingi ya milima. (Sheol )
Le Seigneur distribue la mort et la vie; il conduit aux enfers et il en ramène. (Sheol )
“Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol )
Les angoisses de la mort m'ont entouré, l'agonie de la mort a pris l'avance sur moi. (Sheol )
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
Tu feras ce que t'inspirera ta sagesse, et tu ne laisseras pas sa vieillesse descendre en paix au tombeau. (Sheol )
Shughulika naye kwa kadiri ya hekima yako, lakini usiache kichwa chake chenye mvi kishukie kaburi kwa amani. (Sheol )
Tu ne l'innocenteras point, car tu es un homme sage; tu sauras comment le traiter, et tu feras descendre sa vieillesse au tombeau dans le sang. (Sheol )
Lakini sasa, usidhani kwamba hana hatia. Wewe ni mtu wa hekima, utajua la kumtendea. Zishushe mvi zake kaburini kwa damu.” (Sheol )
Semblable à un nuage suspendu dans les cieux. Car une fois descendu aux enfers l'homme n'en remontera jamais. (Sheol )
Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena. (Sheol )
Le ciel est haut, que feras-tu? L'abîme est profond, que feras-tu? (Sheol )
Ni juu mno kuliko mbingu: waweza kufanya nini? Kina chake ni kirefu kuliko kuzimu: wewe waweza kujua nini? (Sheol )
Puissiez-vous me garder dans les enfers; et me cacher jusqu'à ce que votre courroux s'apaise; et me marquer le temps où vous vous souviendrez de moi. (Sheol )
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol )
Tout ce que j'ai à attendre, c'est la terre pour demeure; ma couche est déjà étendue dans les ténèbres. (Sheol )
Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi, kama nikikitandika kitanda changu gizani, (Sheol )
Est-ce que mon espoir et mes biens descendront avec moi sous la terre? Est-ce que nous serons placés ensemble dans le sépulcre? (Sheol )
Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti? Je, tutashuka pamoja mavumbini?” (Sheol )
Leur vie s'est écoulée au milieu des biens, et ils se sont endormis dans le repos du sépulcre. (Sheol )
Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani. (Sheol )
Sur la terre desséchée, car ils ont ravi la gerbe de l'orphelin. (Sheol )
Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol )
L'enfer est nu devant le Seigneur, et la perdition n'a pas de vêtement. (Sheol )
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol )
Car il n'est personne en la mort qui se souvienne de toi; et aux enfers, qui te rendra gloire? (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
Que les pécheurs soient précipités dans l'enfer, et toutes les nations qui oublient Dieu. (Sheol )
Waovu wataishia kuzimu, naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu. (Sheol )
Parce que tu ne laisseras pas mon âme aux enfers; tu ne permettras pas que ton Saint voie la corruption. (Sheol )
kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu. (Sheol )
J'étais investi par les tourments de l'enfer, j'avais été surpris par les filets de la mort. (Sheol )
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
Seigneur, tu as ramené mon âme de l'enfer; tu m'as sauvé d'entre ceux qui descendent dans le sépulcre. (Sheol )
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
Seigneur, que je ne sois point confondu, car je t'ai invoqué; que les impies rougissent et soient précipités en enfer. (Sheol )
Usiniache niaibike, Ee Bwana, kwa maana nimekulilia wewe, bali waovu waaibishwe na kunyamazishwa Kuzimu. (Sheol )
Ils sont parqués en enfer comme des brebis; la mort s'en repaîtra, et au matin les justes auront pouvoir sur eux; et l'appui qu'ils se faisaient de leur gloire vieillira en enfer. (Sheol )
Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, nacho kifo kitawala. Wanyofu watawatawala asubuhi, maumbile yao yataozea kaburini, mbali na majumba yao makubwa ya fahari. (Sheol )
Cependant Dieu rachètera mon âme de la main de l'enfer, lorsqu'il m'aura reçu. (Sheol )
Lakini Mungu atakomboa uhai wangu na kaburi, hakika atanichukua kwake. (Sheol )
Que la mort vienne sur eux, qu'ils descendent vivants en enfer; car la méchanceté est dans leurs demeures, au milieu d'eux. (Sheol )
Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, na washuke kuzimu wangali hai, kwa maana uovu upo ndani yao. (Sheol )
Car ta miséricorde est grande envers moi, et tu as retiré mon âme du plus profond des enfers. (Sheol )
Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol )
Car mon âme a été remplie de maux, et ma vie s'est approchée de l'enfer. (Sheol )
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
Quel est l'homme qui vivra et ne verra point la mort, qui retirera son âme de la main de l'enfer? (Sheol )
Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo, au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi? (Sheol )
Les douleurs de la mort m'avaient environné; les périls de l'enfer m'avaient atteint. J'avais trouvé la souffrance et la tribulation; (Sheol )
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol )
Si je monte au ciel, tu y es, si je descends en enfer, tu y es présent. (Sheol )
Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol )
Comme les glèbes de la terre sont brisées sur la terre, nos os ont été dispersés aux portes de l'enfer. (Sheol )
Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol )
engloutissons-le tout vivant, comme dans l'enfer, et effaçons de la terre tout souvenir de lui. (Sheol )
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni. (Sheol )
Car les pieds de la folie conduisent ceux qui l'aiment à l'enfer, en compagnie de la mort, et ses pas ne laissent point de traces. (Sheol )
Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini. (Sheol )
Sa maison est le chemin de l'enfer, conduisant au réceptacle de la mort. (Sheol )
Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )
Or il ne sait pas que des géants mêmes périssent auprès d'elle, et qu'il met le pied sur la trappe de l'enfer; (Sheol )
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )
L'enfer et la perdition sont visibles pour le Seigneur; comment n'en serait-il pas de même du cœur des hommes? (Sheol )
Mauti na Uharibifu viko wazi mbele za Bwana: je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu! (Sheol )
Les pensées du sage conduisent à la vie; par elles il se détourne de l'enfer. (Sheol )
Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima kumwepusha asiende chini kaburini. (Sheol )
Et si tu le frappes de verges, tu sauveras son âme de la mort. (Sheol )
Mwadhibu kwa fimbo na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini. (Sheol )
L'enfer et la perdition ne sont jamais rassasiés; de même les yeux des hommes sont insatiables; (Sheol )
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
L'enfer, l'amour d'une femme, une terre qui manque d'eau, l'eau et le feu ne diront jamais: C'est assez. (Sheol )
Ni kaburi, tumbo lisilozaa, nchi isiyoshiba maji kamwe, na moto, usiosema kamwe, ‘Yatosha!’ (Sheol )
Tout ce que ta main aura trouvé à faire, fais-le selon tes forces; car il n'y a ni œuvres, ni raison, ni savoir, ni sagesse dans le tombeau où tu cours. (Sheol )
Lolote mkono wako upatalo kufanya, fanya kwa nguvu zako zote, kwa kuwa huko kuzimu, unakokwenda, hakuna kufanya kazi wala mipango wala maarifa wala hekima. (Sheol )
Mets-moi comme un sceau sur ton cœur, et comme un sceau sur ton bras. Car l'amour est fort comme la mort, et la jalousie est cruelle comme l'enfer; ses traits sont des traits de feu, ce sont des flammes. (Sheol )
Nitie kama muhuri moyoni mwako, kama muhuri kwenye mkono wako; kwa maana upendo una nguvu kama mauti, wivu wake ni mkatili kama kuzimu. Unachoma kama mwali wa moto, kama mwali mkubwa wa moto wa Bwana hasa. (Sheol )
Et l'enfer s'en est dilaté l'âme, et il a ouvert sa bouche pour n'en point laisser échapper; et les grands, et les riches, et les hommes en honneur, et les hommes de pestilence, y descendront. (Sheol )
Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol )
Demande un signe au Seigneur ton Dieu, soit dans le ciel, soit dans l'abîme. (Sheol )
“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol )
L'enfer en ses abîmes s'est troublé à ton approche; et ils se sont levés ensemble contre toi, tous les géants, jadis princes de la terre, qui faisaient descendre de leurs trônes tous les rois des nations. (Sheol )
Kuzimu kote kumetaharuki kukulaki unapokuja, kunaamsha roho za waliokufa ili kukupokea, wote waliokuwa viongozi katika ulimwengu, kunawafanya wainuke kwenye viti vyao vya kifalme: wale wote waliokuwa wafalme juu ya mataifa. (Sheol )
Ta gloire et ta longue prospérité sont descendues aux enfers; la pourriture est ta couche, les vers ta couverture. (Sheol )
Majivuno yako yote yameshushwa mpaka kuzimu, pamoja na kelele ya vinubi vyako, mafunza yametanda chini yako, na minyoo imekufunika. (Sheol )
Et maintenant tu es descendu en enfer, et jusqu'aux fondements de la terre. (Sheol )
Lakini umeshushwa chini hadi kuzimu, hadi kwenye vina vya shimo. (Sheol )
Vous disiez: Nous avons fait un pacte avec l'enfer, et des conventions avec la mort; s'il passe un tourbillon impétueux, il ne viendra pas sur nous; nous avons fait du mensonge notre espérance, nous serons abrités par le mensonge. (Sheol )
Ninyi mnajisifu, “Tumefanya agano na mauti, tumefanya mapatano na kuzimu. Wakati pigo lifurikalo litakapopita, haliwezi kutugusa sisi, kwa kuwa tumefanya uongo kuwa kimbilio letu na miungu ya uongo kuwa mahali petu pa kujificha.” (Sheol )
Est-ce parce que Dieu n'a pu rompre votre alliance avec la mort, ni l'espérance que vous placiez sur l'enfer? Si le tourbillon impétueux passe, il vous foulera aux pieds; (Sheol )
Agano lenu na kifo litabatilishwa, patano lenu na kuzimu halitasimama. Wakati pigo lifurikalo litakapowakumba, litawaangusha chini. (Sheol )
J'ai dit: Dans la plénitude de mes jours, je descendrai aux portes de l'enfer, j'abandonnerai le reste de mes années. (Sheol )
Nilisema, “Katika ustawi wa maisha yangu, je, ni lazima nipite katika malango ya mauti, na kupokonywa miaka yangu iliyobaki?” (Sheol )
Car ceux qui sont en enfer ne vous loueront point, les morts ne vous béniront pas; en enfer on n'espère plus en votre miséricorde. (Sheol )
Kwa maana kaburi haliwezi kukusifu, mauti haiwezi kuimba sifa zako; wale washukao chini shimoni hawawezi kuutarajia uaminifu wako. (Sheol )
Et tu as multiplié tes adultères avec eux, et tu en as gagné beaucoup qui étaient loin de toi, et tu as envoyé des messagers au delà de tes frontières, et tu as été abaissée jusqu'à l'enfer. (Sheol )
Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol )
Et voici ce que dit le Seigneur Maître: Le jour où cet arbre est descendu aux enfers, l'abîme a pleuré sur lui. Et j'ai suspendu le cours de tous ses fleuves, et j'ai arrêté les grandes eaux qui l'arrosaient; et le Liban, à cause de lui, s'est couvert de ténèbres, et tous les arbres se sont affaissés de douleur. (Sheol )
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka. (Sheol )
Au bruit de sa chute, les nations ont tremblé; car je l'ai fait descendre aux enfers avec ceux qui étaient tombés dans l'abîme; et tous les arbres de délices de la terre le consolaient, et tous les beaux arbres du Liban arrosés par les eaux. (Sheol )
Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale washukao shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani. (Sheol )
Et ceux-là aussi sont descendus avec lui aux enfers, parmi les morts frappés par le glaive; et sa race, qui demeurait sous son abri, a péri au milieu de sa vie. (Sheol )
Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga. (Sheol )
Et les géants te diront: Reste au fond de l'abîme; qui est moindre que toi? Descends et dors avec les incirconcis, au milieu des morts frappés du glaive. (Sheol )
Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol )
Et ils dorment avec les géants qui sont tombés autrefois, qui sont descendus aux enfers avec l'armure des batailles; et leurs tètes reposent sur leurs glaives; et leurs iniquités sont retombées sur leurs os, parce que durant leur vie ils avaient épouvanté tous les hommes. (Sheol )
Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol )
Je les tirerai de l'enfer, dira-t-il; je les affranchirai tous de la mort. Ô mort, où est ta sentence? Enfer, où est ton aiguillon? Mais cette consolation est cachée à mes yeux. (Sheol )
“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol )
Dussent-ils se cacher en enfer, Ma main les en arracherait; dussent-ils monter aux cieux, Je les en précipiterais. (Sheol )
Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol )
Et il dit: J'ai crié dans ma tribulation au Seigneur mon Dieu, et Il m'a exaucé; mon cri est parti des entrailles de l'enfer, et Tu as écouté ma voix; (Sheol )
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol )
L'homme présomptueux, méprisant, imposteur, n'arrivera point à ses fins; celui qui a rendu son âme vaste comme l'enfer est aussi insatiable que la mort; il réunira sous lui toutes les nations, et il recevra sous lui tous les peuples. (Sheol )
hakika mvinyo humsaliti; ni mwenye kiburi na hana amani. Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu na kama kifo kamwe hatosheki; anajikusanyia mataifa yote na kuchukua watu wote mateka. (Sheol )
Matthew 5:22 (Mathayo 5:22)
(parallel missing)
Lakini mimi nawaambia kwamba, yeyote atakayemkasirikia ndugu yake, atapaswa hukumu. Tena, yeyote atakayemwambia ndugu yake, ‘Raka,’atapaswa kujibu kwa Baraza la Wayahudi. Lakini yeyote atakayesema ‘Wewe mpumbavu!’ atapaswa hukumu ya moto wa jehanamu. (Geenna )
Matthew 5:29 (Mathayo 5:29)
(parallel missing)
Jicho lako la kuume likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako mzima ukatupwa jehanamu. (Geenna )
Matthew 5:30 (Mathayo 5:30)
(parallel missing)
Kama mkono wako wa kuume ukikusababisha kutenda dhambi, ukate, uutupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako mzima utupwe jehanamu. (Geenna )
Matthew 10:28 (Mathayo 10:28)
(parallel missing)
Msiwaogope wale wauao mwili lakini hawawezi kuua roho. Afadhali mwogopeni yeye awezaye kuiangamiza roho na mwili katika jehanamu. (Geenna )
Matthew 11:23 (Mathayo 11:23)
(parallel missing)
Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs )
Matthew 12:32 (Mathayo 12:32)
(parallel missing)
Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn )
Matthew 13:22 (Mathayo 13:22)
(parallel missing)
Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn )
Matthew 13:39 (Mathayo 13:39)
(parallel missing)
Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn )
Matthew 13:40 (Mathayo 13:40)
(parallel missing)
“Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn )
Matthew 13:49 (Mathayo 13:49)
(parallel missing)
Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn )
Matthew 16:18 (Mathayo 16:18)
(parallel missing)
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs )
Matthew 18:8 (Mathayo 18:8)
(parallel missing)
Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios )
Matthew 18:9 (Mathayo 18:9)
(parallel missing)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna )
Matthew 19:16 (Mathayo 19:16)
(parallel missing)
Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios )
Matthew 19:29 (Mathayo 19:29)
(parallel missing)
Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. (aiōnios )
Matthew 21:19 (Mathayo 21:19)
(parallel missing)
Akauona mtini kando ya barabara, naye akaukaribia, lakini hakupata tunda lolote ila majani. Ndipo akauambia, “Wewe usizae matunda tena kamwe!” Papo hapo ule mtini ukanyauka. (aiōn )
Matthew 23:15 (Mathayo 23:15)
(parallel missing)
“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi! (Geenna )
Matthew 23:33 (Mathayo 23:33)
(parallel missing)
“Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? (Geenna )
Matthew 24:3 (Mathayo 24:3)
(parallel missing)
Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani, wakamuuliza, “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, nayo dalili ya kuja kwako na ya mwisho wa dunia ni gani?” (aiōn )
Matthew 25:41 (Mathayo 25:41)
(parallel missing)
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. (aiōnios )
Matthew 25:46 (Mathayo 25:46)
(parallel missing)
“Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.” (aiōnios )
Matthew 28:20 (Mathayo 28:20)
(parallel missing)
nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika mimi niko pamoja nanyi siku zote, hadi mwisho wa nyakati.” (aiōn )
Mark 3:29 (Marko 3:29)
(parallel missing)
Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn , aiōnios )
Mark 4:19 (Marko 4:19)
(parallel missing)
lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn )
Mark 9:43 (Marko 9:43)
(parallel missing)
Kama mkono wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili lakini ukaingia jehanamu, mahali ambako moto hauzimiki. [ (Geenna )
Mark 9:45 (Marko 9:45)
(parallel missing)
Kama mguu wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili lakini ukaingia jehanamu. [ (Geenna )
Mark 9:47 (Marko 9:47)
(parallel missing)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe. Ni afadhali kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa jehanamu, (Geenna )
Mark 10:17 (Marko 10:17)
(parallel missing)
Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios )
Mark 10:30 (Marko 10:30)
(parallel missing)
ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn , aiōnios )
Mark 11:14 (Marko 11:14)
(parallel missing)
Akauambia ule mti, “Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo. (aiōn )
Luke 1:33 (Luka 1:33)
(parallel missing)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
Luke 1:55 (Luka 1:55)
(parallel missing)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
Luke 1:70 (Luka 1:70)
(parallel missing)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
Luke 8:31 (Luka 8:31)
(parallel missing)
Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo. (Abyssos )
Luke 10:15 (Luka 10:15)
(parallel missing)
Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.” (Hadēs )
Luke 10:25 (Luka 10:25)
(parallel missing)
Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios )
Luke 12:5 (Luka 12:5)
(parallel missing)
Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna )
Luke 16:8 (Luka 16:8)
(parallel missing)
“Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn )
Luke 16:9 (Luka 16:9)
(parallel missing)
Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios )
Luke 16:23 (Luka 16:23)
(parallel missing)
Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs )
Luke 18:18 (Luka 18:18)
(parallel missing)
Mtawala mmoja akamuuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios )
Luke 18:30 (Luka 18:30)
(parallel missing)
ambaye hatapewa mara nyingi zaidi ya hivyo katika maisha haya, na hatimaye kupata uzima wa milele ujao.” (aiōn , aiōnios )
Luke 20:34 (Luka 20:34)
(parallel missing)
Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn )
Luke 20:35 (Luka 20:35)
(parallel missing)
Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn )
John 3:15 (Yohana 3:15)
(parallel missing)
Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios )
John 3:16 (Yohana 3:16)
(parallel missing)
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios )
John 3:36 (Yohana 3:36)
(parallel missing)
Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios )
John 4:14 (Yohana 4:14)
(parallel missing)
Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn , aiōnios )
John 4:36 (Yohana 4:36)
(parallel missing)
Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios )
John 5:24 (Yohana 5:24)
(parallel missing)
“Amin, amin nawaambia, yeyote anayesikia maneno yangu na kumwamini yeye aliyenituma, anao uzima wa milele, naye hatahukumiwa, bali amepita kutoka mautini, na kuingia uzimani. (aiōnios )
John 5:39 (Yohana 5:39)
(parallel missing)
Ninyi mnachunguza Maandiko mkidhani ya kuwa ndani yake mna uzima wa milele, maandiko haya ndiyo yanayonishuhudia Mimi. (aiōnios )
John 6:27 (Yohana 6:27)
(parallel missing)
Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.” (aiōnios )
John 6:40 (Yohana 6:40)
(parallel missing)
Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.” (aiōnios )
John 6:47 (Yohana 6:47)
(parallel missing)
Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios )
John 6:51 (Yohana 6:51)
(parallel missing)
Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn )
John 6:54 (Yohana 6:54)
(parallel missing)
Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios )
John 6:58 (Yohana 6:58)
(parallel missing)
Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn )
John 6:68 (Yohana 6:68)
(parallel missing)
Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. (aiōnios )
John 8:35 (Yohana 8:35)
(parallel missing)
Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn )
John 8:51 (Yohana 8:51)
(parallel missing)
Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn )
John 8:52 (Yohana 8:52)
(parallel missing)
Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn )
John 9:32 (Yohana 9:32)
(parallel missing)
Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn )
John 10:28 (Yohana 10:28)
(parallel missing)
nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn , aiōnios )
John 11:26 (Yohana 11:26)
(parallel missing)
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn )
John 12:25 (Yohana 12:25)
(parallel missing)
Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios )
John 12:34 (Yohana 12:34)
(parallel missing)
Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn )
John 12:50 (Yohana 12:50)
(parallel missing)
Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios )
John 13:8 (Yohana 13:8)
(parallel missing)
Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn )
John 14:16 (Yohana 14:16)
(parallel missing)
Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine akae nanyi milele. (aiōn )
John 17:2 (Yohana 17:2)
(parallel missing)
Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
John 17:3 (Yohana 17:3)
(parallel missing)
Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
Acts 2:27 (Matendo 2:27)
(parallel missing)
Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs )
Acts 2:31 (Matendo 2:31)
(parallel missing)
Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs )
Acts 3:21 (Matendo 3:21)
(parallel missing)
Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. (aiōn )
Acts 13:46 (Matendo 13:46)
(parallel missing)
Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa. (aiōnios )
Acts 13:48 (Matendo 13:48)
(parallel missing)
Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. (aiōnios )
Acts 15:18 (Matendo 15:18)
(parallel missing)
ambayo yamejulikana tangu zamani. (aiōn )
Romans 1:20 (Warumi 1:20)
(parallel missing)
Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios )
Romans 1:25 (Warumi 1:25)
(parallel missing)
Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn )
Romans 2:7 (Warumi 2:7)
(parallel missing)
Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
Romans 5:21 (Warumi 5:21)
(parallel missing)
ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios )
Romans 6:22 (Warumi 6:22)
(parallel missing)
Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakatifu, ambao mwisho wake ni uzima wa milele. (aiōnios )
Romans 6:23 (Warumi 6:23)
(parallel missing)
Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios )
Romans 9:5 (Warumi 9:5)
(parallel missing)
Wao ni wa uzao wa mababa wakuu wa kwanza, ambao kutoka kwao Kristo alikuja kwa jinsi ya mwili kama mwanadamu, yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, mwenye kuhimidiwa milele! Amen. (aiōn )
Romans 10:7 (Warumi 10:7)
(parallel missing)
“au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) (Abyssos )
Romans 11:32 (Warumi 11:32)
(parallel missing)
Kwa maana Mungu amewafunga wanadamu wote kwenye kuasi ili apate kuwarehemu wote. (eleēsē )
Romans 11:36 (Warumi 11:36)
(parallel missing)
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, viko kwake na kwa ajili yake. Utukufu ni wake milele! Amen. (aiōn )
Romans 12:2 (Warumi 12:2)
(parallel missing)
Msifuatishe tena mfano wa ulimwengu huu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Ndipo mtaweza kuonja na kuhakikisha ni nini mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yanayopendeza machoni pake na ukamilifu. (aiōn )
Romans 16:25 (Warumi 16:25)
(parallel missing)
Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios )
Romans 16:26 (Warumi 16:26)
(parallel missing)
Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios )
Romans 16:27 (Warumi 16:27)
(parallel missing)
Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn )
1-Corinthians 1:20 (1 Wakorintho 1:20)
(parallel missing)
Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn )
1-Corinthians 2:6 (1 Wakorintho 2:6)
(parallel missing)
Lakini miongoni mwa watu waliokomaa twanena hekima, wala si hekima ya ulimwengu huu au ya watawala wa dunia hii wanaobatilika. (aiōn )
1-Corinthians 2:7 (1 Wakorintho 2:7)
(parallel missing)
Sisi tunanena hekima ya Mungu ambayo ni siri, tena iliyofichika, ambayo Mungu aliikusudia kabla ya ulimwengu kuwepo, kwa ajili ya utukufu wetu. (aiōn )
1-Corinthians 2:8 (1 Wakorintho 2:8)
(parallel missing)
Hakuna hata mtawala mmoja wa nyakati hizi aliyeelewa jambo hili. Kwa maana kama wangelielewa, wasingemsulubisha Bwana wa utukufu. (aiōn )
1-Corinthians 3:18 (1 Wakorintho 3:18)
(parallel missing)
Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. (aiōn )
1-Corinthians 8:13 (1 Wakorintho 8:13)
(parallel missing)
Kwa hiyo, kama kile ninachokula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke. (aiōn )
1-Corinthians 10:11 (1 Wakorintho 10:11)
(parallel missing)
Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn )
1-Corinthians 15:55 (1 Wakorintho 15:55)
(parallel missing)
“Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs )
2-Corinthians 4:4 (2 Wakorintho 4:4)
(parallel missing)
Kwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu. (aiōn )
2-Corinthians 4:17 (2 Wakorintho 4:17)
(parallel missing)
Kwa maana dhiki yetu nyepesi iliyo ya kitambo inatutayarisha kwa ajili ya utukufu wa milele unaozidi kuwa mwingi kupita kiasi, (aiōnios )
2-Corinthians 4:18 (2 Wakorintho 4:18)
(parallel missing)
kwa sababu hatuangalii yale yanayoweza kuonekana bali yale yasiyoweza kuonekana. Kwa maana yale yanayoweza kuonekana ni ya kitambo tu, bali yale yasiyoweza kuonekana ni ya milele. (aiōnios )
2-Corinthians 5:1 (2 Wakorintho 5:1)
(parallel missing)
Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios )
2-Corinthians 9:9 (2 Wakorintho 9:9)
(parallel missing)
Kama ilivyoandikwa: “Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele.” (aiōn )
2-Corinthians 11:31 (2 Wakorintho 11:31)
(parallel missing)
Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye anahimidiwa milele, anajua ya kuwa mimi sisemi uongo. (aiōn )
Galatians 1:4 (Wagalatia 1:4)
(parallel missing)
aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn )
Galatians 1:5 (Wagalatia 1:5)
(parallel missing)
Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
Galatians 6:8 (Wagalatia 6:8)
(parallel missing)
Apandaye kwa mwili, katika mwili wake atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. (aiōnios )
Ephesians 1:21 (Waefeso 1:21)
(parallel missing)
juu sana kuliko falme zote na mamlaka, enzi na milki, na juu ya kila jina litajwalo, si katika ulimwengu huu tu, bali katika ule ujao pia. (aiōn )
Ephesians 2:2 (Waefeso 2:2)
(parallel missing)
ambazo mlizitenda mlipofuatisha namna ya ulimwengu huu na za yule mtawala wa ufalme wa anga, yule roho atendaye kazi sasa ndani ya wale wasiotii. (aiōn )
Ephesians 2:7 (Waefeso 2:7)
(parallel missing)
ili katika ule ulimwengu ujao apate kuonyesha wingi wa neema yake isiyopimika, iliyodhihirishwa kwetu kwa wema wake ndani ya Kristo Yesu. (aiōn )
Ephesians 3:9 (Waefeso 3:9)
(parallel missing)
na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn )
Ephesians 3:11 (Waefeso 3:11)
(parallel missing)
sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
Ephesians 3:21 (Waefeso 3:21)
(parallel missing)
yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn )
Ephesians 6:12 (Waefeso 6:12)
(parallel missing)
Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. (aiōn )
Philippians 4:20 (Wafilipi 4:20)
(parallel missing)
Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
Colossians 1:26 (Wakolosai 1:26)
(parallel missing)
Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. (aiōn )
2-Thessalonians 1:9 (2 Wathesalonike 1:9)
(parallel missing)
Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, (aiōnios )
2-Thessalonians 2:16 (2 Wathesalonike 2:16)
(parallel missing)
Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios )
1-Timothy 1:16 (1 Timotheo 1:16)
(parallel missing)
Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. (aiōnios )
1-Timothy 1:17 (1 Timotheo 1:17)
(parallel missing)
Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
1-Timothy 6:12 (1 Timotheo 6:12)
(parallel missing)
Pigana vile vita vizuri vya imani. Shika uzima wa milele ambao ndio ulioitiwa ulipokiri ule ukiri mzuri mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios )
1-Timothy 6:16 (1 Timotheo 6:16)
(parallel missing)
yeye peke yake ambaye hapatikani na mauti, na anakaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa, ambaye hakuna mwanadamu aliyemwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye milele. Amen. (aiōnios )
1-Timothy 6:17 (1 Timotheo 6:17)
(parallel missing)
Waagize wale ambao ni matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke tumaini lao katika mali ambayo si ya hakika, bali waweke tumaini lao katika Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie. (aiōn )
2-Timothy 1:9 (2 Timotheo 1:9)
(parallel missing)
ambaye alituokoa na kutuita katika mwito mtakatifu: si kwa kadiri ya matendo yetu mema bali kwa sababu ya kusudi lake mwenyewe na neema yake. Neema hii tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele. (aiōnios )
2-Timothy 2:10 (2 Timotheo 2:10)
(parallel missing)
Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios )
2-Timothy 4:10 (2 Timotheo 4:10)
(parallel missing)
kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn )
2-Timothy 4:18 (2 Timotheo 4:18)
(parallel missing)
Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
Titus 1:2 (Tito 1:2)
(parallel missing)
imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios )
Titus 2:12 (Tito 2:12)
(parallel missing)
Nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia, ili tupate kuishi maisha ya kiasi, ya haki na ya utaua katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn )
Titus 3:7 (Tito 3:7)
(parallel missing)
ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios )
Philemon 1:15 (Filemoni 1:15)
(parallel missing)
Huenda sababu ya yeye kutengwa nawe kwa kitambo kidogo ni ili uwe naye daima. (aiōnios )
Hebrews 1:2 (Wahebrania 1:2)
(parallel missing)
lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn )
Hebrews 1:8 (Wahebrania 1:8)
(parallel missing)
Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn )
Hebrews 5:6 (Wahebrania 5:6)
(parallel missing)
Pia mahali pengine asema, “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.” (aiōn )
Hebrews 5:9 (Wahebrania 5:9)
(parallel missing)
na akiisha kukamilishwa, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii. (aiōnios )
Hebrews 6:2 (Wahebrania 6:2)
(parallel missing)
mafundisho kuhusu aina za ubatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. (aiōnios )
Hebrews 6:5 (Wahebrania 6:5)
(parallel missing)
ambao wameonja uzuri wa Neno la Mungu na nguvu za wakati ujao, (aiōn )
Hebrews 6:20 (Wahebrania 6:20)
(parallel missing)
mahali ambapo Yesu mtangulizi wetu aliingia kwa niaba yetu. Yeye amekuwa Kuhani Mkuu milele, kwa mfano wa Melkizedeki. (aiōn )
Hebrews 7:17 (Wahebrania 7:17)
(parallel missing)
Kwa maana imeshuhudiwa kwamba: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.” (aiōn )
Hebrews 7:21 (Wahebrania 7:21)
(parallel missing)
lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alimwambia: “Bwana ameapa naye hatabadilisha mawazo yake: ‘Wewe ni kuhani milele.’” (aiōn )
Hebrews 7:24 (Wahebrania 7:24)
(parallel missing)
Lakini kwa sababu Yesu anaishi milele, anao ukuhani wa kudumu. (aiōn )
Hebrews 7:28 (Wahebrania 7:28)
(parallel missing)
Kwa kuwa sheria huwaweka makuhani wakuu watu ambao ni dhaifu; lakini lile neno la kiapo, lililokuja baada ya sheria, lilimweka Mwana, ambaye amefanywa kuwa mkamilifu milele. (aiōn )
Hebrews 9:12 (Wahebrania 9:12)
(parallel missing)
Hakuingia kwa njia ya damu ya mbuzi na ya ndama; lakini aliingia Patakatifu pa Patakatifu mara moja tu kwa damu yake mwenyewe, akiisha kupata ukombozi wa milele. (aiōnios )
Hebrews 9:14 (Wahebrania 9:14)
(parallel missing)
Basi ni zaidi aje damu ya Kristo, ambaye kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na waa, itatusafisha dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo mauti, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai! (aiōnios )
Hebrews 9:15 (Wahebrania 9:15)
(parallel missing)
Kwa sababu hii Kristo ni mpatanishi wa agano jipya, ili kwamba wale walioitwa waweze kupokea ile ahadi ya urithi wa milele: kwa vile yeye alikufa awe ukombozi wao kutoka kwa dhambi walizozitenda chini ya agano la kwanza. (aiōnios )
Hebrews 9:26 (Wahebrania 9:26)
(parallel missing)
Ingekuwa hivyo, ingempasa Kristo kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Lakini sasa ametokea mara moja tu katika mwisho wa nyakati aiondoe dhambi kwa kujitoa mwenyewe kuwa dhabihu. (aiōn )
Hebrews 11:3 (Wahebrania 11:3)
(parallel missing)
Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn )
Hebrews 13:8 (Wahebrania 13:8)
(parallel missing)
Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn )
Hebrews 13:20 (Wahebrania 13:20)
(parallel missing)
Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios )
Hebrews 13:21 (Wahebrania 13:21)
(parallel missing)
awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
James 3:6 (Yakobo 3:6)
(parallel missing)
Ulimi pia ni moto, ndio ulimwengu wa uovu kati ya viungo vya mwili. Ulimi huutia mwili wote wa mtu unajisi na kuuwasha moto mfumo mzima wa maisha yake, nao wenyewe huchomwa moto wa jehanamu. (Geenna )
1-Peter 1:23 (1 Petro 1:23)
(parallel missing)
Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn )
1-Peter 1:25 (1 Petro 1:25)
(parallel missing)
lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn )
1-Peter 4:11 (1 Petro 4:11)
(parallel missing)
Yeyote asemaye hana budi kusema kama mtu asemaye maneno ya Mungu mwenyewe. Yeyote ahudumuye hana budi kuhudumu kwa nguvu zile anazopewa na Mungu, ili Mungu apate kutukuzwa katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
1-Peter 5:10 (1 Petro 5:10)
(parallel missing)
Nanyi mkiisha kuteswa kwa kitambo kidogo, Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atawarejesha na kuwatia nguvu, akiwaimarisha na kuwathibitisha. (aiōnios )
1-Peter 5:11 (1 Petro 5:11)
(parallel missing)
Uweza una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
2-Peter 1:11 (2 Petro 1:11)
(parallel missing)
na mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios )
2-Peter 2:4 (2 Petro 2:4)
(parallel missing)
Kwa maana, kama Mungu hakuwasamehe malaika walipotenda dhambi, bali aliwatupa kuzimu katika vifungo vya giza wakae humo mpaka ije hukumu; (Tartaroō )
2-Peter 3:18 (2 Petro 3:18)
(parallel missing)
Bali kueni katika neema na katika kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na milele! Amen. (aiōn )
1-John 1:2 (1 Yohana 1:2)
(parallel missing)
Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. (aiōnios )
1-John 2:17 (1 Yohana 2:17)
(parallel missing)
Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele. (aiōn )
1-John 2:25 (1 Yohana 2:25)
(parallel missing)
Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele. (aiōnios )
1-John 3:15 (1 Yohana 3:15)
(parallel missing)
Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
1-John 5:11 (1 Yohana 5:11)
(parallel missing)
Huu ndio ushuhuda: kwamba Mungu ametupa uzima wa milele, nao huo uzima umo katika Mwanawe. (aiōnios )
1-John 5:13 (1 Yohana 5:13)
(parallel missing)
Nawaandikia mambo haya ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu ili mpate kujua ya kuwa mnao uzima wa milele. (aiōnios )
1-John 5:20 (1 Yohana 5:20)
(parallel missing)
Nasi pia twajua ya kwamba Mwana wa Mungu amekuja, naye ametupa sisi ufahamu ili tupate kumjua yeye aliye Kweli. Nasi tumo ndani yake yeye aliye Kweli, yaani, ndani ya Yesu Kristo Mwanawe. Yeye ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele. (aiōnios )
2-John 1:2 (2 Yohana 1:2)
(parallel missing)
kwa sababu ya ile kweli ikaayo ndani yetu na ambayo itaendelea kukaa nasi milele: (aiōn )
Jude 1:6 (Yuda 1:6)
(parallel missing)
Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios )
Jude 1:7 (Yuda 1:7)
(parallel missing)
Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios )
Jude 1:13 (Yuda 1:13)
(parallel missing)
Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn )
Jude 1:21 (Yuda 1:21)
(parallel missing)
Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios )
Jude 1:25 (Yuda 1:25)
(parallel missing)
kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn )
Revelation 1:6 (Ufunuo 1:6)
(parallel missing)
akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. (aiōn )
Revelation 1:18 (Ufunuo 1:18)
(parallel missing)
Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn , Hadēs )
Revelation 4:9 (Ufunuo 4:9)
(parallel missing)
Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aketiye kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, (aiōn )
Revelation 4:10 (Ufunuo 4:10)
(parallel missing)
wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aketiye kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema: (aiōn )
Revelation 5:13 (Ufunuo 5:13)
(parallel missing)
Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba: “Sifa na heshima na utukufu na uweza ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi na kwa Mwana-Kondoo, milele na milele!” (aiōn )
Revelation 6:8 (Ufunuo 6:8)
(parallel missing)
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs )
Revelation 7:12 (Ufunuo 7:12)
(parallel missing)
wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn )
Revelation 9:1 (Ufunuo 9:1)
(parallel missing)
Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake, nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka toka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ilipewa ufunguo wa lile Shimo. (Abyssos )
Revelation 9:2 (Ufunuo 9:2)
(parallel missing)
Alipolifungua hilo Shimo, moshi ukapanda kutoka humo kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vikatiwa giza na ule moshi uliotoka katika hilo Shimo. (Abyssos )
Revelation 9:11 (Ufunuo 9:11)
(parallel missing)
Walikuwa na mfalme wao, ambaye ni malaika wa lile Shimo, ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani ni Apolioni. (Abyssos )
Revelation 10:6 (Ufunuo 10:6)
(parallel missing)
Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn )
Revelation 11:7 (Ufunuo 11:7)
(parallel missing)
Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos )
Revelation 11:15 (Ufunuo 11:15)
(parallel missing)
Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn )
Revelation 14:6 (Ufunuo 14:6)
(parallel missing)
Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios )
Revelation 14:11 (Ufunuo 14:11)
(parallel missing)
Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn )
Revelation 15:7 (Ufunuo 15:7)
(parallel missing)
Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn )
Revelation 17:8 (Ufunuo 17:8)
(parallel missing)
Huyo mnyama ambaye ulimwona, wakati fulani alikuwepo, lakini sasa hayupo, naye atapanda kutoka lile Shimo na kwenda kwenye maangamizo yake. Watu waishio duniani ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuumbwa kwa ulimwengu watastaajabu kumwona huyo mnyama, kwa maana alikuwepo wakati fulani, na sasa hayupo, lakini atakuwepo. (Abyssos )
Revelation 19:3 (Ufunuo 19:3)
(parallel missing)
Wakasema tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” (aiōn )
Revelation 19:20 (Ufunuo 19:20)
(parallel missing)
Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
Revelation 20:1 (Ufunuo 20:1)
(parallel missing)
Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, akiwa ameshika ufunguo wa lile Shimo na mnyororo mkubwa mkononi mwake. (Abyssos )
Revelation 20:3 (Ufunuo 20:3)
(parallel missing)
Akamtupa katika lile Shimo, akamfunga humo na kulitia lakiri, ili kumzuia asiendelee kudanganya mataifa mpaka hiyo miaka 1,000 itimie. Baada ya hayo lazima afunguliwe kwa muda mfupi. (Abyssos )
Revelation 20:10 (Ufunuo 20:10)
(parallel missing)
Naye ibilisi aliyewadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti walikokuwa wametupwa yule mnyama na yule nabii wa uongo. Watateswa humo usiku na mchana, milele na milele. (aiōn , Limnē Pyr )
Revelation 20:13 (Ufunuo 20:13)
(parallel missing)
Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, nayo mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Kila mtu akahukumiwa kulingana na yale aliyoyatenda. (Hadēs )
Revelation 20:14 (Ufunuo 20:14)
(parallel missing)
Kisha mauti na Kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. (Hadēs , Limnē Pyr )
Revelation 20:15 (Ufunuo 20:15)
(parallel missing)
Iwapo mtu jina lake halikuonekana katika kile kitabu cha uzima, alitupwa ndani ya lile ziwa la moto. (Limnē Pyr )
Revelation 21:8 (Ufunuo 21:8)
(parallel missing)
Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr )
Revelation 22:5 (Ufunuo 22:5)
(parallel missing)
Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, kwa maana Bwana Mungu atakuwa nuru yao, nao watatawala milele na milele. (aiōn )
Son âme s'est approchée de la mort et sa vie de l'enfer. ()
Les portes de la mort s'ouvrent-elles sans t'effrayer? Peux-tu soutenir sans épouvante les regards des gardiens de l'enfer? ()
Si le Seigneur ne m'eût aidé, peu s'en est fallu que mon âme n'ait habité l'enfer. ()
Les morts, Seigneur, ne te loueront point ni tous ceux qui descendent en enfer. ()
et qui oublie l'alliance divine, a mis sa maison près de la mort, et ses voies près de l'enfer avec les fils de la terre. ()
Il est une voie qui aux hommes semble droite; mais elle aboutit aux abîmes de l'enfer. ()
Il est des voies qui semblent droites à l'homme; mais leur extrémité lui fait voir dans le fond de l'enfer. ()
Et quand l'enfer sèmera la division entre les frères, le Seigneur enverra contre lui un vent brûlant du désert, et Il desséchera les veines de la mort, et Il tarira ses sources; Lui-même fera de ses champs une terre aride, et enlèvera ses vases les plus précieux. ()