< Néhémie 1 >

1 Récits de Néhémias, fils d'Helcias. Au mois de chaseleu, en la vingtième année, j'étais à Suse, résidence royale.
Maneno ya Nehemia mwana wa Hakalia: Katika mwezi wa Kisleu katika mwaka wa ishirini, wakati nilikuwa ngomeni katika jumba la kifalme la Shushani,
2 Et Anani, l'un de mes frères, vint, lui et des hommes de Juda, et je les questionnai, tant sur ceux qui étaient demeurés de la captivité et vivaient encore, que sur Jérusalem.
Hanani, mmoja wa ndugu zangu, alikuja kutoka Yuda akiwa na watu wengine, nami nikawauliza kuhusu mabaki ya Wayahudi wale walionusurika kwenda uhamishoni na pia kuhusu Yerusalemu.
3 Et ils me dirent: Ceux qui sont demeurés, et qui ont été laissés de la captivité, sont dans la terre promise en grande détresse et opprobre; les murs de Jérusalem ont été abattus, et ses portes brûlées par le feu.
Wakaniambia, “Wale walionusurika kwenda uhamishoni, wale ambao wamerudi kwenye lile jimbo, wako katika taabu kubwa na aibu. Ukuta wa Yerusalemu umebomoka, na malango yake yamechomwa moto.”
4 Or, quand j'eus ouï de telles paroles, je m'assis et pleurai, et, pendant plusieurs jours, me lamentai, et j'étais jeûnant et priant devant le Dieu du ciel.
Niliposikia mambo haya, niliketi, nikalia. Kwa siku kadhaa niliomboleza na kufunga na kuomba mbele za Mungu wa mbinguni.
5 Et je dis: Que cela ne soit, je vous prie, Seigneur Dieu du ciel, Dieu fort, grand et redoutable qui gardez votre alliance et votre miséricorde à ceux qui vous aiment et observent vos commandements.
Kisha nikasema: “Ee Bwana, Mungu wa mbinguni, mkuu na mwenye kuogofya, ambaye hulishika agano lake la upendo na wale wampendao na kutii amri zake,
6 Que votre oreille soit attentive, que vos yeux s'ouvrent, afin d'ouïr l'oraison de votre serviteur que je fais maintenant devant vous, nuit et jour, pour vos serviteurs les enfants d'Israël; et je me confesse pour les péchés des enfants d'Israël, en lesquels nous avons péché contre vous. Moi et la maison de mon père avons péché.
tega masikio yako, na ufungue macho yako, ili usikie maombi ya mtumishi wako anayoomba mbele yako usiku na mchana kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli. Ninaungama dhambi zetu sisi Waisraeli, pamoja na zangu na za nyumba ya baba yangu, tulizotenda dhidi yako.
7 Nous avons rompu l'alliance; nous n'avons point gardé les commandements, les jugements et les ordonnances que vous avez intimés à Moïse, votre serviteur.
Tumetenda uovu sana mbele zako. Hatukutii amri, maagizo na sheria ulizompa Mose mtumishi wako.
8 Souvenez-vous de la parole que vous avez intimée à Moïse, votre serviteur, disant: Si vous manquez à notre alliance, je vous disperserai parmi les nations.
“Kumbuka agizo ulilompa Mose mtumishi wako, ukisema, ‘Kama mkikosa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa,
9 Et si vous revenez à moi, si vous gardez mes commandements, si vous les pratiquez, quand vous seriez disséminés jusqu'aux lieux où la terre touche le ciel, je vous en ramènerai, je vous réunirai en la terre que j'ai choisie pour que mon nom y réside.
lakini mkinirudia na kutii amri zangu, ndipo hata kama watu wenu walio uhamishoni wako mbali sana katika miisho ya dunia, nitawakusanya kutoka huko na kuwaleta mahali ambapo nimepachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina langu.’
10 Et voici vos serviteurs et votre peuple que vous avez rachetés par votre toute-puissance et votre forte main.
“Hawa ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa nguvu zako kuu na mkono wako wenye nguvu.
11 Qu'ils ne demeurent pas ainsi, Seigneur; mais que votre oreille soit attentive à l'oraison de votre serviteur et à celle de vos serviteurs qui veulent craindre votre nom. Soyez-lui propice aujourd'hui à votre serviteur; faites qu'il trouve miséricorde devant les hommes; or, j'étais échanson du roi.
Ee Bwana, tega sikio lako na usikie maombi ya huyu mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako wanaofurahia kuliheshimu Jina lako. Nipe leo, mimi mtumishi wako, mafanikio kwa kunipa kibali mbele ya mtu huyu.” Kwa maana nilikuwa mnyweshaji wa mfalme.

< Néhémie 1 >