< Néhémie 2 >

1 Et, au mois de nisan, en la vingtième année du règne d'Arthasastha, le vin était devant moi, et je pris le vin et le versai au roi, et il n'y avait là en sa présence nul autre que moi.
Katika mwezi wa Nisani mwaka wa ishirini wa utawala wa Mfalme Artashasta, wakati divai ilipoletwa kwake, niliichukua na kumpa mfalme. Sikuwahi kuonekana mwenye huzuni mbele yake kabla ya hapo.
2 Et le roi me dit: D'où vient que ton visage est mauvais, et que tu ne te contiens pas? Cela ne serait point si le mal n'était en ton cœur. Et j'eus grande crainte.
Basi mfalme akaniuliza, “Kwa nini uso wako unaonekana una huzuni wakati wewe si mgonjwa? Jambo hili si kitu kingine bali ni huzuni ya moyo.” Niliogopa sana,
3 Et je dis au roi: Que le roi vive toujours; comment mon visage ne serait-il pas mauvais, puisque la ville qui est la maison des sépulcres de mes pères est déserte, et que ses portes ont été brûlées par le feu?
lakini nikamwambia mfalme, “Mfalme na aishi milele! Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni wakati mji walipozikwa baba zangu umebaki magofu, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”
4 Et le roi me dit: À quel sujet me demandes-tu cela? Et je priai le Dieu du ciel;
Mfalme akaniambia, “Je, haja yako ni gani?” Ndipo nikaomba kwa Mungu wa mbinguni,
5 Et je répondis au roi: S'il semble bon au roi, si son serviteur trouve grâce devant lui, je demande qu'il envoie son serviteur en Juda, à la ville des sépulcres de mes pères, et je la réédifierai.
na nikamjibu mfalme, “Kama ikimpendeza mfalme, na kama mtumishi wako amepata kibali machoni pake, anitume kule mji wa Yuda, mahali baba zangu walipozikwa, ili niweze kuujenga upya.”
6 Et le roi et sa concubine qui siégeait auprès de lui, me dirent: Jusqu'à quand durera ton voyage? quand reviendras-tu? Et le roi le trouva bon, et il me laissa partir, et je lui donnai un terme.
Kisha mfalme, na malkia akiwa ameketi karibu naye, akaniuliza, “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi lini?” Ilimpendeza mfalme kunituma, kwa hiyo nikapanga muda.
7 Et je dis au roi: Si le roi le trouve bon, qu'il me donne des lettres pour les gouverneurs au delà de l'Euphrate, afin qu'ils ne mettent point d'obstacle à mon arrivée en Juda,
Pia nikamwambia, “Kama ikimpendeza mfalme, naomba nipewe barua kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati, ili wanipe ulinzi mpaka nifike Yuda.
8 Et une lettre adressée à Asaph, le garde du jardin qui appartient au roi, afin qu'il me fournisse du bois pour réparer les portes et les murs de la ville, et la maison où je me logerai. Et, comme la bonne main du Seigneur était avec moi, le roi me donna les lettres.
Naomba nipewe barua nipeleke kwa Asafu, mtunzaji wa msitu wa mfalme, ili anipe miti ya kutengeneza boriti kwa ajili ya malango ya ngome ya Hekalu, na ukuta wa mji, na makao yangu nitakapoishi.” Kwa kuwa mkono wenye neema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu, mfalme akanijalia ombi langu.
9 Et j'arrivai chez les gouverneurs au delà de l'Euphrate, et je leur remis les lettres du roi. Or, le roi m'avait fait accompagner par des chefs de l'armée et par de la cavalerie.
Basi nilienda kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati na kuwapa barua za mfalme. Pia mfalme alikuwa ametuma maafisa wa jeshi na askari wapanda farasi pamoja nami.
10 Et Sanaballat l'Aronite, et Tobias, le serviteur ammonite, l'ouïrent; et il était mauvais pour eux qu'un homme fût venu faire du bien aux fils d'Israël.
Sanbalati Mhoroni na Tobia afisa Mwamoni waliposikia juu ya jambo hili, waliudhika sana kwamba amekuja mtu kuinua ustawi wa Waisraeli.
11 Et j'entrai à Jérusalem, et j'y restai trois jours.
Nilienda Yerusalemu, na baada ya kukaa huko siku tatu,
12 Et je me levai de nuit, moi et quelque petit nombre de gens, et je ne dis à personne ce que Dieu m'avait mis dans le cœur de faire pour Israël; et je n'avais point de bête avec moi, sinon la bête sur laquelle j'étais monté.
nikaondoka wakati wa usiku pamoja na watu wachache. Sikuwa nimemwambia mtu yeyote kile ambacho Mungu wangu alikuwa ameweka moyoni mwangu kufanya kwa ajili ya Yerusalemu. Hapakuwepo na mnyama yeyote pamoja nami isipokuwa yule niliyekuwa nimempanda.
13 Et je sortis par la porte de la Vallée, passant devant la fontaine des Figuiers, et allant à la porte du Fumier; et je marchais le cœur brisé, à cause des remparts de Jérusalem qu'ils avaient abattus, et des portes qu'ils avaient brûlées par le feu.
Nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bondeni, kuelekea Kisima cha Joka na Lango la Samadi, nikikagua kuta za Yerusalemu zilizokuwa zimebomolewa, na malango yake yaliyokuwa yameteketezwa kwa moto.
14 Et je passai devant la porte de la Fontaine, puis, devant la piscine du Roi; et il n'y avait point de place par où la bête que j'avais sous moi pût passer.
Kisha nikaelekea mpaka Lango la Chemchemi na Bwawa la Mfalme, lakini hapakuwepo nafasi ya kutosha kwa ajili ya mnyama wangu kupita,
15 Alors, je m'en allai montant, de nuit, le long du torrent, et j'avais le cœur brisé, à cause du mur, et je revins à la porte de la Vallée, et je rentrai.
kwa hiyo nikapandia bondeni usiku nikikagua ukuta. Mwishoni nikarudi na kuingia tena kupitia Lango la Bondeni.
16 Et les sentinelles ne surent ni où j'étais allé ni ce que je voulais faire; et, jusque-là, je n'en avais rien dit aux Juifs, ni aux prêtres, ni aux premiers du peuple, ni aux chefs, ni au reste de ceux qui faisaient les travaux.
Maafisa hawakujua nilikokwenda wala nilichokuwa nikifanya, kwa sababu mpaka sasa nilikuwa bado sijasema lolote kwa Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala maafisa, wala mtu yeyote ambaye angefanya kazi.
17 Et je leur dis: Vous voyez l'affliction où nous sommes: Jérusalem est déserte, et ses portes ont été brûlées par le feu. Allons, relevons les remparts de la ville, et nous ne serons plus outragés.
Ndipo nilipowaambia, “Mnaona taabu tuliyo nayo: Yerusalemu imebaki magofu na malango yake yameteketezwa kwa moto. Njooni tujenge upya ukuta wa Yerusalemu, nasi hatutakuwa tena katika aibu hii.”
18 Et je leur dis que la bonne main de Dieu était avec moi, à en juger par les paroles que le roi m'avait dites, et j'ajoutai: Levons-nous, édifions. Et leurs mains furent fortifiées en cette bonne œuvre.
Pia niliwaambia kuhusu mkono wenye neema wa Mungu wangu uliokuwa juu yangu, na kile mfalme alichokuwa ameniambia. Wakajibu, “Haya! Tuanze kujenga tena.” Kwa hiyo wakaanza kazi hii njema.
19 Et Sanaballat l'Aronite, et Tobias le serviteur ammonite, et l'Arabe Gésam, le surent, et ils nous raillèrent, et ils vinrent à nous, et ils dirent: Qu'est-ce que vous faites? Vous révoltez-vous contre le roi?
Lakini Sanbalati Mhoroni, Tobia afisa Mwamoni, na Geshemu Mwarabu waliposikia kuhusu jambo hili, walitudhihaki na kutucheka. Wakauliza, “Ni nini hiki mnachokifanya? Je, mnaasi dhidi ya mfalme?”
20 Et je leur répliquai, et je leur dis: Le Dieu du ciel lui-même mènera notre œuvre à bien; et nous, ses serviteurs, nous sommes purs, et nous édifierons. Quant à vous, vous n'avez ni part, ni droit, ni mémorial en Jérusalem.
Nikawajibu kwa kusema, “Mungu wa mbinguni atatufanikisha. Sisi watumishi wake tutaanza kujenga upya, lakini kwenu ninyi, hamna sehemu wala dai lolote wala kumbukumbu la haki katika Yerusalemu.”

< Néhémie 2 >