< Michée 4 >

1 Et voici ce qui arrivera: au dernier jour, la montagne du Seigneur apparaîtra; on la verra au-dessus des cimes des monts; elle s'élèvera plus haut que les collines. Et les peuples auront hâte de s'en approcher;
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote; utainuliwa juu ya vilima, na watu wa mataifa watamiminika humo.
2 et les gentils viendront en grand nombre, et diront: Venons, montons sur la montagne du Seigneur, et au temple du Dieu de Jacob. On nous en montrera le chemin, et nous cheminerons en ses entiers; car de Sion sortira la loi, et de Jérusalem la parole du Seigneur.
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
3 Et Il jugera entre beaucoup de peuples, et Il châtiera, même au loin, des nations puissantes; et chez elles on forgera les glaives pour en faire des socs de charrues, et des javelines pour en faire des faux; de nation à nation, on ne s'attaquera plus par l'épée, on n'apprendra plus à combattre.
Atahukumu kati ya mataifa mengi, na ataamua migogoro ya mataifa yenye nguvu na yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
4 Et chacun se reposera sous sa vigne et sous son figuier; et nul ne leur inspirera de crainte, parce que le Seigneur tout-puissant l'a dit de Sa bouche.
Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakuna mtu atakayewaogopesha, kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.
5 Tous les peuples alors suivront chacun sa voie; mais nous, nous marcherons au Nom du Seigneur, notre Dieu, dans tous les siècles et au delà.
Mataifa yote yanaweza kutembea katika jina la miungu yao; sisi tutatembea katika jina la Bwana Mungu wetu milele na milele.
6 En ce jour, dit le Seigneur, Je réunirai celle qui a le cœur contrit et celle que J'ai repoussée, et J'accueillerai ceux que J'avais chassés;
“Katika siku hiyo,” asema Bwana, “nitawakusanya walemavu; nitawakusanya walio uhamishoni na wale niliowahuzunisha.
7 et Je mettrai en réserve celle qui a eu le cœur contrit; et Je ferai une nation puissante de celle que J'avais repoussée; et le Seigneur régnera sur elles en la montagne de Sion, depuis ce moment jusqu'à la fin des siècles.
Nitawafanya walemavu kuwa mabaki, wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu. Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni kuanzia siku hiyo na hata milele.
8 Et toi, vieille tour du troupeau, Sion Ma fille, la principauté te reviendra et rentrera dans tes murs; et le premier royaume de Babylone reviendra à Ma fille Jérusalem.
Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi, ee ngome ya Binti Sayuni, milki ya awali itarudishwa kwako, ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”
9 Et maintenant pourquoi as-tu connu le malheur? N'avais-tu pas un roi? Ou ta raison avait-elle péri pour que tu aies senti les douleurs de l'enfantement?
Kwa nini sasa unalia kwa nguvu: kwani huna mfalme? Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate kama ya mwanamke aliye na utungu wa kuzaa?
10 Souffre et prends courage, et approche, Sion, ma fille; souffre comme une femme qui enfante; car bientôt tu sortiras de tes murs, tu dresseras tes tentes dans la plaine, et tu iras jusqu'à Babylone; puis le Seigneur ton Dieu t'en délivrera, et Il te tirera des mains de tes ennemis.
Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji ukapige kambi uwanjani. Utakwenda Babeli; huko utaokolewa. Huko Bwana atakukomboa kutoka mikononi mwa adui zako.
11 Et maintenant, contre toi maintes nations se sont rassemblées, elles disaient: Réjouissons-nous, et que nos yeux surveillent Sion!
Lakini sasa mataifa mengi yamekusanyika dhidi yako. Wanasema, “Mwache anajisiwe, macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”
12 Mais elles ne savaient pas la pensée du Seigneur; elles n'avaient point compris Ses conseils; car Il les avait rassemblées comme des gerbes dans une aire.
Lakini hawayajui mawazo ya Bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.
13 Lève-toi, Sion, Ma fille, tombe sur elles comme le fléau; Je te donnerai des cornes de fer; Je te couvrirai d'armes d'airain, et tu briseras maintes nations, et tu consacreras leurs grains nombreux au Seigneur, et leurs richesses au Seigneur de toute la terre.
“Inuka upure, ee Binti Sayuni, kwa kuwa nitakupa pembe za chuma; nitakupa kwato za shaba na utavunja vipande vipande mataifa mengi.” Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana, utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.

< Michée 4 >