< Michée 1 >

1 Et la parole de Dieu vint à Michée, fils de Morasthi, aux jours de Joatham, Achaz et Ézéchias, rois de Juda, sur les choses qu'il vit concernant Samarie et Jérusalem.
Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
2 Écoutez, peuples, ces paroles; que toute la terre soit attentive, et tous ceux qu'elle contient. Et le Seigneur Maître sera parmi nous comme un témoignage, le Seigneur du haut de Sa maison sainte.
Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
3 Car voilà que le Seigneur sortira du lieu où Il réside, et Il descendra, et Il marchera sur les hauteurs de la terre.
Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
4 Et sous Lui les montagnes seront émues, et les vallées fondront comme la cire devant le feu, et comme les eaux d'une cataracte.
Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
5 Et tout cela arrivera à cause de l'impiété de Jacob et des péchés de la maison d'Israël. Quelle est l'impiété de Jacob? n'est-ce pas Samarie? Quel est le péché de Juda? n'est-ce pas Jérusalem?
Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
6 Je rendrai Samarie comme la cabane d'un garde de vergers dans les champs, comme un plant de vigne; et J'arracherai ses pierres pour les jeter dans le ravin, et Je mettrai à découvert ses fondations.
“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
7 Et toutes ses statues tomberont; et tous ses salaires qu'elle a reçus seront livrés aux flammes; et J'anéantirai toutes ses idoles; car elle a amassé des salaires de prostitution; et de ces salaires de prostitution elle s'est enrichie.
Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
8 À cause de cela, elle se frappera la poitrine et se lamentera; elle ira nue et déchaussée; ses lamentations seront comme les sifflements du dragon, et ses plaintes comme celles des filles des Sirènes.
Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
9 Car la plaie l'accable; sa plaie s'est étendue jusqu'en Juda, et touche aux portes de Mon peuple, à Jérusalem.
Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
10 Ô vous, gens de Geth, ne vous glorifiez pas; vous, gens d'Énacim, n'édifiez pas avec les ruines du temple par dérision; mais répandez de la poussière sur vos têtes par dérision de vous-mêmes!
Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
11 La populeuse Sennaar, qui habite en joie ses villes, n'en est point sortie pour pleurer une maison voisine; elle entendra votre plainte douloureuse.
Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
12 Qui a commencé à faire du bien à celle qui habitait dans la douleur? Car les maux sont aussi descendus, par le Seigneur, jusqu'aux portes de Jérusalem,
Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
13 avec le tumulte des chars et des cavaliers. Celle qui demeure en Lachis est pour le fille de Sion le principe de son péché; car en toi se sont trouvés les impiétés d'Israël.
Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
14 À cause de cela, le Seigneur enverra des vengeurs jusqu'aux héritages de Geth, et jusqu'aux maisons vaines qui ont été vanités pour les rois d'Israël.
Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
15 Et ils emmèneront tes héritiers, ô toi qui demeures en Lachis! L'héritage de gloire de la fille d'Israël ne subsistera pas au delà d'Odollam.
Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
16 Rase-toi, coupe ta chevelure à cause de tes enfants, qui font tes délices; dilate ton veuvage comme un aigle; car on les a emmenés en captivité hors de toi.
Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.

< Michée 1 >