< Malachie 4 +

1 Voilà que le jour approche, brûlant comme une fournaise, et il les consumera; et tous les étrangers et tous ceux qui font le mal seront comme de la paille; et le jour qui approche les dévorera, dit le Seigneur tout-puissant; et il ne restera d'eux ni branche ni racine.
“Hakika siku inakuja, itawaka kama tanuru. Wote wenye kiburi na kila mtenda mabaya watakuwa mabua makavu, na siku ile inayokuja itawawasha moto,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Hakuna mzizi wala tawi litakalosalia kwao.
2 Et le Soleil de justice Se lèvera pour vous qui craignez Mon Nom; et sur Ses ailes Il portera le salut; et vous sortirez, et vous bondirez comme de jeunes bœufs délivrés de leurs liens.
Bali kwenu ninyi mnaoliheshimu Jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mabawa yake. Nanyi mtatoka nje na kurukaruka kama ndama aliyeachiwa kutoka zizini.
3 Et vous foulerez les impies; car ils seront sous vos pieds comme de la cendre, le jour que Je ferai naître, dit le Seigneur tout-puissant.
Kisha ninyi mtawakanyaga waovu, nao watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayofanya mambo haya,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Souvenez-vous de la loi de Moïse, Mon serviteur, telle que Je la lui ai intimée, en Horeb, devant tout Israël, dans ses commandements et ses préceptes.
“Kumbukeni sheria ya mtumishi wangu Mose, amri na sheria nilizompa huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote.
5 Et voilà que Je vous enverrai Élie le Thesbite, avant que vienne ce jour du Seigneur, jour grand et éclatant,
“Tazama, nitawapelekea nabii Eliya kabla ya kuja siku ile iliyo kuu na ya kutisha ya Bwana.
6 qui réunira au fils le cœur de son père, à l'homme le cœur de son prochain, de peur que Je ne survienne et que Je n'anéantisse la terre.
Ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, la sivyo nitakuja na kuipiga nchi kwa laana.”

< Malachie 4 +