< Lamentations 4 >

1 Aleph. Comment l'or s'est-il terni? Comment l'argent pur s'est-il changé? Comment les pierres saintes ont-elles été dispersées aux coins de toutes les rues?
Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
2 Beth. Les fils de Sion les plus honorés, ceux que l'on prisait autant que l'or, comment ont-ils été traités comme des vases de terre, œuvre des mains du potier?
Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
3 Ghimel. Les dragons eux-mêmes ont découvert leurs mamelles; et leurs petits ont allaité les filles de mon peuple, pour leur communiquer leur incurable instinct, comme l'autruche dans le désert.
Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
4 Daleth. La langue de l'enfant à la mamelle, s'est collée à son palais dans sa soif; les enfants ont demandé du pain, et nul n'était là pour leur en distribuer.
Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
5 Hé. Ceux qui se nourrissaient de mets délicats ont péri dans les rues; ceux qu'on avait élevés dans la pourpre ont été enfouis dans le fumier.
Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
6 Vav. L'iniquité de la fille de mon peuple a dépassé l'iniquité de Sodome, jadis renversée en un moment, sans que des hommes y aient fatigué leurs mains.
Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
7 Zaïn. Les Nazaréens étaient plus blancs que la neige, plus éclatants que le lait; ils étaient comme purifiés par le feu; leur poli était supérieur à celui du saphir.
Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
8 Cheth. Et leur visage est devenu plus noir que la suie, on ne les reconnaît pas dans les rues; leur peau s'est collée sur leurs os; ils se sont desséchés comme du bois mort.
Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
9 Teth. Les hommes tués par le glaive étaient plus beaux que les hommes morts de faim; car ceux-ci s'en étaient allés transpercés par la disette des fruits de la terre.
Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
10 Iod. Les mains des femmes, naturellement compatissantes, ont fait cuire leurs propres enfants; elles s'en sont nourries dans la ruine de la fille de mon peuple.
Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
11 Caph. Le Seigneur a assouvi sa colère; il a répandu son indignation et ses fureurs, et il a allumé dans Sion un feu qui l'a dévorée jusqu'en ses fondements.
Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
12 Lamed. Les rois de la terre, les peuples du monde entier ne croyaient pas qu'un ennemi, qu'un oppresseur pût entrer par les portes de Jérusalem.
Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
13 Mem. À cause des péchés de ses prophètes, et des iniquités de ses prêtres, qui au milieu d'elle versaient le sang innocent,
Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
14 Noun. Les gardes ont chancelé dans les rues, ne pouvant éviter d'y marcher; ils se sont souillés de sang, et leurs robes y ont touché.
Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
15 Samech. Éloignez-vous des impurs; criez-leur: Retirez-vous, retirez- vous, ne nous touchez pas; car ceux que les impurs ont touché ont chancelé; dites aux nations: Ils n'habiteront plus parmi nous.
Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
16 Aïn. La présence du Seigneur était leur partage; il ne les considèrera plus; ils n'ont pas respecté le visage des prêtres; ils ont été sans miséricorde pour les prophètes.
Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
17 Phé. Quand nous vivions encore, nos yeux se sont lassés à vainement regarder, et à attendre du secours.
Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
18 Tsadé. Nous nous sommes tournés vers une nation qui ne pouvait nous sauver; nous avons fait la chasse à nos petits enfants, de peur qu'ils ne sortissent dans les places publiques.
Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
19 Coph. Notre temps est proche; nos jours sont remplis; le moment est arrivé; nos persécuteurs sont venus, plus agiles que l'aigle dans le ciel; ils se sont élancés des montagnes; ils nous ont tendu des pièges dans le désert.
Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
20 Resch. L'esprit de notre face, le Christ Seigneur a été pris dans leurs filets, lui dont nous avons dit: Nous vivrons à son ombre parmi les nations!
Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
21 Schin. Réjouis-toi, sois dans l'allégresse, fille de l'Idumée qui habite la terre; le calice du Seigneur passera aussi sur toi, tu t'enivreras, et tu vomiras ton ivresse.
Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
22 Thav. Ton iniquité a cessé, fille de Sion; ta captivité touche à son terme; mais le Seigneur a visité ton iniquité, fille d'Édom, et il a mis tes impiétés à découvert.
Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.

< Lamentations 4 >