< Juges 1 >

1 Il advint, après la mort de Josué, que les fils d'Israël consultèrent le Seigneur, disant: Quel chef nous conduira contre les Chananéens pour les combattre?
Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
2 Et le Seigneur dit: Juda marchera; voilà que j'ai mis en sa main la terre promise.
Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
3 Et Juda dit à Siméon, son frère: Viens avec moi sur mes terres, et nous livrerons bataille aux Chananéens, ensuite j'irai avec toi sur ton territoire. Et Siméon marcha avec lui.
Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
4 Juda partit donc, et le Seigneur livra à ses mains le Chananéen et le Phérézéen; il les tailla en pièces à Bézec au nombre de dix mille.
Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
5 Après avoir surpris à Bézec Adonibézec, ils lui livrèrent bataille, et taillèrent en pièces le Chananéen et le Phérézéen.
Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
6 Adonibézec prit la fuite, ils coururent après lui, l'atteignirent et lui coupèrent les extrémités des pieds et des mains.
Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
7 Alors, Adonibézec dit: Soixante-dix rois à qui j'avais fait couper les extrémités des pieds et des mains, ont ramassé ce qui tombait sous ma table. Dieu m'a donc traité comme j'ai traité autrui. Et ils le conduisirent à Jérusalem, où il mourut.
Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
8 Et, les fils de Juda assiégèrent Jérusalem; ils la prirent, ils passèrent les habitants au fil de l'épée, et ils incendièrent la ville.
Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
9 Après cela, les fils de Juda descendirent pour combattre le Chananéen qui habitait les montagnes du midi et la plaine.
Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
10 Et Juda marcha contre le Chananéen qui habitait Hébron, et tout Hébron sortit à sa rencontre; le nom d'Hébron était autrefois Cariath-Arboc-Sépher; Juda vainquit Sessi, Achiraan et Tholmi, de la race d'Enac.
Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
11 De là, il monta pour attaquer Dabir; or, le nom de Dabir était autrefois Cariath-Sépher, ou Ville des Lettres.
Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
12 Et Caleb dit: Celui qui montera à l'assaut de la Ville des Lettres et la prendra, je lui donnerai pour femme ma fille Ascha.
Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
13 Et Gothoniel, fils de Cénez, frère puîné de Caleb, prit la ville; et Caleb lui donna pour femme sa fille Ascha.
Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
14 Tandis qu'elle s'en allait, Gothoniel lui persuada de demander à son père un champ, et, montée sur son âne, elle murmura et cria: Tu m'as établie en une terre du midi. Et Caleb lui dit: Qu'as-tu?
Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
15 Et Ascha lui dit: Accorde-moi un bienfait; tu m'as établie en une terre du midi; tu me donneras une terre arrosée d'eau - Et Caleb lui donna, selon son cœur, une terre arrosée en haut et en bas.
Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
16 En ce temps-là, les fils de Jéthro le Cinéen, beau-père de Moïse, montèrent de la Ville des Palmiers, pour se réunir aux fils de Juda, dans le désert, au midi de Juda, vers la descente d'Arad, et ils demeurèrent parmi le peuple.
Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
17 Ensuite, Juda marcha avec son frère Siméon; ils vainquirent le Chananéen qui habitait en Sépheth, ils l'exterminèrent, et ils donnèrent à cette ville le nom d'Anathème.
Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
18 Mais Juda ne prit possession ni de Gaza, ni de son territoire; ni d'Ascalon, ni de son territoire; ni d'Accaron, ni de son territoire; ni d'Asor, ni de son territoire.
Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
19 Toutefois, le Seigneur était avec Juda; il eut dans son héritage la contrée montagneuse, mais il ne put exterminer les habitants de la côte, parce que Rhéchab s'y opposait.
Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
20 Quant à Caleb, on lui avait donné, selon l'ordre de Moïse, le territoire d'Hébron, où il eut dans son héritage les trois villes des fils d'Enac.
Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
21 Les fils de Benjamin ne purent s'emparer du territoire des Jébuséens qui habitaient Jérusalem; les Jebuséens, jusqu'à ce jour, ont donc habité Jérusalem avec les fils de Benjamin.
Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
22 De leur côté, les fils de Joseph montèrent à Béthel, et le Seigneur était avec eux,
Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
23 Et, après avoir établi leur camp, ils reconnurent Béthel, dont le nom était autrefois Luza.
Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
24 Or, les gardes virent un homme qui sortait de la ville; ils le prirent, et ils lui dirent: Montre-nous par où l'on peut entrer dans la ville, et nous serons miséricordieux envers toi.
wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
25 Et il leur montra l'entrée de la ville, et ils passèrent la ville au fil de l'épée, et ils laissèrent aller l'homme avec toute sa famille.
Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
26 L'homme s'en alla dans la terre d'Heltim; il y bâtit une ville, et il lui donna le nom de Luza, qu'elle porte encore de nos jours.
Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
27 Manassé ne détruisit ni Bethsan, qui est une ville des Scythes; ni ses filles, ni ses alentours; ni Thanac, ni ses dépendances; ni les habitants de Dor, ni leurs dépendances; ni l'habitant de Balac, ni ses filles, ni ses dépendances; ni Magedo, ni ses filles, ni ses alentours; ni Jéblaam, ni ses filles, ni ses alentours. Les Chananéens commencèrent à habiter cette terre avec eux.
Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
28 Mais, lorsque Israël eut pris des forces, il assujettit le Chananéen au tribut, quoiqu'il ne le détruisit pas.
Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
29 Ephraïm ne détruisit pas le Chananéen qui habitait Gazer; le Chananéen continua de demeurer à Gazer avec lui, et lui paya un tribut.
Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
30 Zabulon ne détruisit pas les habitants de Cédron, ni ceux de Domana. Le Chananéen continua de demeurer avec lui, et devint son tributaire.
Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
31 Aser ne détruisit pas les habitants d'Accho; ils devinrent ses tributaires; il ne détruisit pas les habitants de Dor, ni ceux de Sidon, de Dalaph, d'Aschazi, de Chebda, de Naï et d'Eréo.
Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
32 Aser demeura au milieu des Chananéens qui habitaient cette terre, parce qu'il ne put les détruire.
na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
33 Nephthali ne détruisit pas les habitants de Bethsamys, ni ceux de Béthanath; Nephthali demeura au milieu du Chananéen qui habitait la contrée. Ceux de Bethsamys et de Béthanath devinrent ses tributaires.
Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
34 L'Amorrhéen resserra Dan sur les montagnes; il ne lui permit pas de descendre dans les vallées.
Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
35 Les Amorrhéens commencèrent même à habiter la montagne de l'Argile, où il y a des ours et des renards; ils eurent Myrsinon et Thalabin; mais la main de la maison de Joseph s'appesantit sur l'Amorrhéen, et celui-ci devint son tributaire.
Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
36 Les limites de l'Amorrhéen furent la montée d'Acrabin, les rochers et les hauteurs qui les dominent.
Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.

< Juges 1 >