< Juges 7 >

1 Après cela, Jérobaal, le même que Gédéon, se leva de grand matin, et tout le peuple avec lui; ils campèrent vers la fontaine d'Arad, et le camp de Moab était au nord de la fontaine, du côté de Gabaathamoré, dans le vallon.
Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
2 Et le Seigneur dit à Gédéon: Le peuple qui te suit est nombreux, tellement que je ne livrerai pas Madian à ses mains, de peur qu'Israël n'aille se glorifier contre moi, et ne dise: C'est ma main qui m'a sauvé.
Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
3 Parle donc au peuple, disant: Y a-t-il ici quelqu'un qui craigne et faiblisse? que celui-là s'en aille, qu'il s'éloigne des montagnes de Galaad. Or, vingt-deux mille du peuple partirent, et dix mille restèrent.
kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
4 Et le Seigneur dit à Gédéon; Ce peuple est encore nombreux; fais-le descendre auprès de l'eau, et là je le purifierai pour toi. Et celui de qui je le dirai: Il doit marcher avec toi, marchera; celui de qui je te dirai: Il ne doit point marcher avec toi, ne marchera pas.
Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
5 Et Gédéon conduisit le peuple auprès de l'eau, et le Seigneur lui dit: Celui qui prendra de l'eau avec la langue, comme le font les chiens, tu le placeras d'un côté, et tu placeras d'un autre côté tous ceux qui se mettront à genoux pour boire.
Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
6 Or, le nombre de ceux qui prirent de l'eau dans leur main et la portèrent à leur bouche s'éleva à trois cents, et tout le reste du peuple se mit à genoux pour boire.
Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
7 Et le Seigneur dit à Gédéon: C'est avec les trois cents hommes qui ont pris de l'eau dans leurs mains que je vous sauverai et vous livrerai Madian; tout le reste du peuple s'en ira, chacun en son pays.
Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
8 Les trois cents prirent donc tous les vivres du peuple et leurs cors, et Gédéon congédia tout Israël, chacun en sa demeure, puis il encouragea les trois cents. Cependant, le camp des Madianites était au-dessous de lui, au fond de la vallée.
Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
9 Et cette nuit-là même, il advint que le Seigneur lui dit: Debout, descends sur leur camp, car je l'ai livré à tes mains,
Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
10 Si tu crains de descendre seul, descends sur le camp avec Phara, ton serviteur.
Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
11 Ecoute ce qu'ils diront; après cela, tes mains seront fortifiées, et tu descendras pour attaquer le camp. Il descendit, accompagné seulement de Phara, son serviteur, vers la plus avancée des compagnies de cinquante hommes qui étaient dans le camp.
nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
12 Et Madian, Amalec et les fils de l'Orient étaient entassés au fond de la vallée, comme les sauterelles quand elles foisonnent; la multitude de leurs chameaux était innombrable, et ils étaient comme le sable sur le rivage de la mer.
Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
13 Quand Gédéon survint, voilà qu'un homme racontait à son voisin un songe, et il disait: J'ai eu un songe; j'ai vu un pain de pâte d'orge roulant sur le camp des Madianites; il arriva jusqu'à une tente, il la frappa et la fit tomber; il renversa de fond en comble la tente, et elle tomba.
Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
14 Or, son voisin lui répondit: Le pain n'est autre chose que l'épée de Gédéon, fils de Joas, homme d'Israël. Le Seigneur a livré à ses mains Madian et notre camp tout entier.
Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
15 Gédéon, ayant ouï le récit du songe et son interprétation, adora le Seigneur; il rentra au camp d'Israël, et il dit: Levez-vous, parce que le Seigneur a livré à nos mains le camp des Madianites.
Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
16 Il divisa ses trois cents hommes en trois troupes, et il leur donna des cors à tous, et dans l'autre main des pots vides, et dans chaque pot une lampe.
Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
17 Et il leur dit: Soyez attentifs a ce que je ferai, et faites de même. J'entrerai par la tête du camp, et comme je ferai vous ferez aussi.
Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
18 Je ferai retentir mon cor, et vous sonnerez de même tout à l'entour du camp, et vous direz: Au Seigneur et à Gédéon!
Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
19 Gédéon et ses cent hommes entrèrent donc par la tête du camp, au commencement de la seconde veille; le bruit qu'ils firent réveilla les gardes; et ils sonnèrent du cor, et ils agitèrent les pots qu'ils tenaient à la main.
Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
20 Les trois troupes sonnèrent du cor, et brisèrent leurs pots; alors, les hommes, tenant de la main gauche les lampes et de la main droite les cors, qu'ils faisaient retentir, crièrent: L'épée du Seigneur et de Gédéon!
Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
21 Chaque homme resta en place tout autour du camp, et tout le camp se mit à courir; les Madianites se donnèrent des ordres confus, et ils s'enfuirent.
Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
22 Et les trois cents cors sonnaient toujours, et le Seigneur tourna l'épée de chaque Madianite contre son voisin dans le camp tout entier. Le camp s'enfuit jusqu'à Bethséed, Tagaragatha, Abelméula, tirant vers Tabath.
Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
23 En Israël, Nephthali, Aser, tout Manassé apportèrent leur secours, et ils poursuivirent Madian.
Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
24 Et Gédéon dépêcha des messagers dans toutes les montagnes d'Ephraïm, disant: Descendez à la rencontre de Madian, emparez-vous de l'eau jusqu'à Béthéra, emparez-vous du cours du Jourdain. Et tous les hommes d'Ephraïm crièrent, et ils s'emparèrent de l'eau jusqu'à Béthéra; ils s'emparèrent du cours du Jourdain.
Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
25 Et ils prirent les chefs de Madian Oreb et Zeb; ils tuèrent Oreb à Sur- Oreb; ils tuèrent Zeb en Jacephzeph. Et ils poursuivirent Madian, et ils rapportèrent, de l'autre côté du Jourdain, à Gédéon, les têtes de Zeb et d'Oreb.
Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.

< Juges 7 >