< Juges 6 >

1 Les fils d'Israël firent encore le mal devant le Seigneur, et le Seigneur les livra aux mains de Madian, pendant sept années.
Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani.
2 Et la main de Madian prévalut sur Israël; et les fils d'Israël, à l'aspect de Madian, se firent des cachettes dans les montagnes; ils se firent des grottes et des murs de défense dans les rochers.
Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome.
3 Quand les fils d'Israël avaient semé, Madian montait avec Amalec; les fils de l'Orient marchaient dans leurs rangs, et ils campaient chez eux,
Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao.
4 Et ils détruisaient leurs fruits jusqu'aux portes de Gaza, et ils ne laissèrent rien de ce qui sert à la vie en la terre d'Israël, et ils n'épargnaient ni bœuf ni âne parmi les troupeaux,
Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda.
5 Parce qu'ils montaient avec tous leurs biens et avec leurs tentes, nombreux comme des sauterelles lorsqu'elles foisonnent; leur multitude et celle de leurs chameaux étaient innombrables; ils dominaient sur la terre d'Israël, et ils la dévastaient.
Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu.
6 Israël était tout appauvri devant la face de Madian. Et les fils d'Israël crièrent au Seigneur,
Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.
7 Et il advint ensuite que
Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani,
8 Et le Seigneur envoya un prophète aux fils d'Israël, et l'homme leur dit: Voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël: Je suis Celui qui vous ai tirés de la terre d'Egypte, qui vous ai fait sortir de votre maison de servitude.
Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa.
9 Je vous ai arrachés des mains de l'Egyptien et de tous ceux qui vous opprimaient; j'ai banni ceux-ci de devant votre face, et je vous ai donné leur territoire.
Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao.
10 Et je vous ai dit: Je suis le Seigneur votre Dieu; n'ayez point crainte des dieux des Amorrhéens, parmi lesquels vous résiderez en leur terre. Mais vous n'avez pas été dociles à ma voix.
Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”
11 Ensuite, un ange du Seigneur vint, et il s'arrêta sous le térébinthe d'Ephratha, en la terre de Joas, fils d'Esdri, comme son fils Gédéon battait du blé dans le pressoir pour échapper aux regards des Madianites.
Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione.
12 L'ange du Seigneur lui apparut, et il lui dit: Le Seigneur est avec toi, fort parmi les plus vaillants.
Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”
13 Et Gédéon dit: Je vous prie, mon Seigneur; si le Seigneur est avec nous, pourquoi ces maux nous sont-ils venus? Et où sont tous ces miracles que nous ont racontés nos pères, disant: N'est-ce point le Seigneur qui nous a fait sortir de l'Egypte? Maintenant, il nous a renversés, il nous a livrés aux mains de Madian.
Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”
14 L'ange du Seigneur le regarda, et lui dit: Marche en ta force, et tu délivreras Israël des mains de Madian. Voilà que pour cela je t'envoie.
Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”
15 Et Gédéon lui dit: Je vous prie, mon Seigneur, et comment sauverai-je Israël? Voilà que mes mille hommes sont sans force dans Manassé, et je suis le moindre de la maison de mon père.
Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”
16 L'ange reprit: Le Seigneur sera avec toi, et tu vaincras Madian comme un seul homme.
Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”
17 Et Gédéon lui dit: Si j'ai trouvé miséricorde à vos yeux, et si vous accomplissez aujourd'hui par moi tout ce que vous m'avez promis,
Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami.
18 Ne vous éloignez pas d'ici que je n'y revienne; j'apporterai une victime, et je la sacrifierai devant vous. Et l'ange répondit: Je vais rester jusqu'à ton retour.
Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.” Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”
19 Gédéon rentra donc; il prépara un chevreau, et des pains sans levain d'une mesure de farine (éphi); il mit les chairs sur une corbeille, il versa le jus dans un vase; il porta tout cela à l'ange sous le térébinthe, et il s'approcha de lui.
Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.
20 Et l'ange de Dieu lui dit: Prends les chairs et les azymes, dépose-les sur cette pierre, et répands le jus par-dessus; ainsi fit Gédéon.
Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
21 Et l'ange du Seigneur étendit le bout de la baguette qu'il tenait à la main; il toucha les chairs et les azymes, et il s'éleva de la pierre une flamme qui dévora les chairs et les azymes; et l'ange du Seigneur disparut à ses yeux.
Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.
22 Gédéon vit ainsi que c'était un ange du Seigneur, et il dit: Hélas! hélas! Seigneur, mon Seigneur, j'ai vu face à face un ange du Seigneur.
Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
23 Et le Seigneur lui dit: La paix soit avec toi; n'aie point crainte, tu ne mourras point.
Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”
24 Gédéon éleva en ce lieu un autel au Seigneur, et il le nomma la Paix du Seigneur, comme on le nomme de nos jours, car il subsiste encore en Ephratha, ville du père Esdri.
Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.
25 Cette nuit même il advint que le Seigneur dit à Gédéon: Prends le taureau de ton père, avec une seconde tête de sept ans; puis tu renverseras l'autel de Baal appartenant à ton père, et tu détruiras le bois sacré qui est tout auprès;
Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo.
26 Cela fait, tu élèveras un autel au Seigneur ton Dieu sur la cime de ce mont Maozi, en signe de résistance; tu prendras la seconde tête de bétail, et tu l'offriras comme holocauste, en la brûlant avec les arbres du bois sacré que tu auras détruit.
Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
27 Gédéon prit dix de ses serviteurs, et il fit ce que le Seigneur lui avait dit. Or, comme il craignait, à cause de la maison de son père et des hommes de la ville, de le faire en plein jour, il le fit la nuit.
Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.
28 Les hommes de la ville se levèrent de grand matin, et voilà que l'autel de Baal était renversé, et le bois sacré situé tout auprès détruit; et ils virent la seconde tête de bétail que Gédéon avait offerte, sur l'autel qu'il avait élevé.
Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!
29 Chacun dit à son voisin: Qui a fait cela? ils s'informèrent, et ils apprirent que c'était Gédéon, fils de Joas.
Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?” Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”
30 Les hommes de la ville dirent alors à Joas: Amène-nous ton fils; qu'il soit mis à mort, parce qu'il a renversé l'autel de Baal et qu'il a détruit le bois sacré situé auprès.
Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”
31 Et Gédéon, fils de Joas, dit à tous les hommes de la ville, qui s'étaient soulevés contre lui: Allez-vous plaider pour Baal? est-ce vous qui le sauverez? Que celui qui plaidera pour Baal soit mis à mort avant le lever du jour. Si Baal est Dieu, qu'il se venge, puisqu'on a renversé son autel.
Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.”
32 Et il se donna à lui-même ce jour-là le nom de Jérobaal, en disant: Que Baal se venge, puisque son autel a été renversé.
Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.
33 En ce temps-là, Madian, Amalec, et les fils de l'Orient, étaient rassembles tous à la fois; ils campaient dans la vallée de Jezraël;
Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli.
34 Et l'esprit du Seigneur vint en Gédéon; il fit sonner du cor, et sur ses pas Abiézer accourut à son secours.
Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate.
35 Alors, il dépêcha des messagers à tout Manassé, a Azer, à Zabulon et à Nephthali, et il marcha au-devant des hommes de ces tribus.
Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.
36 Et Gédéon dit à Dieu: Si votre volonté est de sauver par ma main Israël, comme vous avez dit,
Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi:
37 Voyez: je dépose dans l'aire cette toison de laine; que la rosée se montre sur la toison seule et qu'il y ait sécheresse sur toute la terre, et je reconnaîtrai votre volonté de sauver par ma main Israël, comme vous avez dit.
tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.”
38 Il en fut ainsi. Gédéon se leva de grand matin; il pressa la toison, la rosée coula de la laine, et remplit d'eau un bassin.
Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.
39 Ensuite, Gédéon dit à Dieu: Que votre courroux ne s'enflamme point contre moi, et je parlerai une seule fois encore, je ferai une seule fois encore l'épreuve de la toison: que la sécheresse se montre sur la toison seule, et la rosée sur toute la terre.
Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.”
40 Dieu fit ainsi en cette nuit même: la sécheresse se montra sur la toison seule, et il y eut de la rosée sur toute la terre.
Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.

< Juges 6 >