< Juges 5 >

1 Ce jour-là, Débora et Barac, fils d'Abinéem, chantèrent ainsi:
Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
2 Une révélation s'est faite en Israël, quand le peuple a été de bonne volonté; bénissez le Seigneur.
“Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Bwana!
3 Ecoutez, rois; prêtez l'oreille, princes; je vais chanter un psaume au Seigneur Dieu d'Israël.
“Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Bwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
4 Seigneur, quand vous êtes sorti de Séir, quand vous avez quitté les champs d'Edom, la terre a tremblé, le ciel a fait tomber de la rosée, les nuages ont répandu de l'eau.
“Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
5 Les montagnes ont été ébranlées à la face du Seigneur Eloï, et aussi le Sina, à la face du Seigneur Dieu d'Israël.
Milima ilitetemeka mbele za Bwana, hata ule wa Sinai, mbele za Bwana, Mungu wa Israeli.
6 Durant les jours de Samegar, fils d'Anath, durant les jours de Jaël, ils ont quitté les voies, ils ont pris des sentiers, ils ont suivi des chemins détournés.
“Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
7 Les hommes forts ont manqué en Israël, ils ont manqué jusqu'à ce que vint Débora, jusqu'à ce que s'élevât une mère en Israël.
Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
8 Ils s'étaient choisi de nouveaux dieux; alors, les ennemis ont attaqué même les villes des princes. Si l'on avait vu alors un bouclier et une lance parmi les quarante mille guerriers d'Israël!
Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.
9 Mon cœur est tout aux commandements donnés à Israël; vous qui parmi le peuple êtes de bonne volonté, bénissez le Seigneur.
Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, pamoja na wale wanaojitoa wenyewe kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Bwana!
10 Vous qui montez sur des ânesses belles et luisantes, vous qui êtes assis sur le siège où l'on rend la justice, vous qui vous avancez sur la route des sièges ou vers cette route; racontez ces hauts faits,
“Nanyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mtembeao barabarani, fikirini
11 Loin du bruit des perturbateurs, au milieu de ceux qui puisent paisiblement de l'eau, au lieu où l'on rend la justice. Seigneur, multipliez la justice en Israël. Alors, le peuple du Seigneur descendra aux portes de la ville.
juu ya sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Bwana walipoteremka malangoni pa mji.
12 Réveille-toi, réveille-toi, Débora, réveille-toi, réveille-toi; chante un cantique; debout, ô Barac; emmène en captivité tes prisonniers, fils d'Abinéem.
‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
13 Ce jour-là, est descendu ce qui restait des forts. Le peuple du Seigneur est descendu avec le Seigneur, et les vaillants excités par moi.
“Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wenye nguvu, watu wa Bwana, wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
14 Ephraïm les a déracinés en Amalec, et, à votre suite, Seigneur, Benjamin et tout votre peuple. Ceux de Machir sont descendus avec moi, ardents à chercher l'ennemi; et ceux de Zabulon, même ceux qui maniaient la plume des scribes raconteurs.
Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini akiwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
15 Les princes d'Issachar étaient avec Débora; ainsi, elle envoya Balac à pied dans les vallons, sur le territoire de Ruben, où il y a grandes angoisses atteignant le cœur.
Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
16 Pourquoi demeurent-ils, au milieu des parcs, à entendre les beuglements de leurs grands troupeaux, pendant les discordes de Ruben? là, il y a de grandes épreuves du cœur.
Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
17 Galaad est de l'autre côté du Jourdain, ou il a dressé ses tentes. Et Dan, pourquoi se tient-il sur ses barques? Aser s'est assis sur la côte maritime, il habite vers les embouchures de ses cours d'eau.
Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
18 Le peuple de Zabulon a exposé sa vie à la mort; Nephthali est venu sur les hauts lieux de sa terre.
Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
19 Les rois se sont ranges en bataille, les rois de Chanaan ont combattu en Thanaach, près des eaux de Mageddo; ils n'ont point recueilli de butin.
“Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
20 Les étoiles, du haut du ciel, ont pris part à la lutte, sans quitter leurs voies; elles ont combattu contre Sisara.
Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
21 Le torrent de Cison les a balayés, le torrent des anciens, le torrent de Cison! Mon âme dans sa force foulera aux pieds les ennemis.
Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
22 Lorsque les jambes des chevaux furent embarrassées, ses forts se hâtèrent de fuir.
Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
23 Maudite soit Méroz, dit l'ange du Seigneur, maudissez-la. Maudits soient tous ceux qui l'habitent, parce qu'ils ne sont point venus au secours du Seigneur, parce qu'ils ne lui ont point envoyé leurs hommes vaillants.
Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe. Walaaniwe watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’
24 Bénie soit, parmi les femmes, Jaël, l'épouse d'Haber le Cinéen; que sous leurs tentes les femmes la bénissent.
“Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote waishio kwenye mahema.
25 Il avait demandé de l'eau; elle lui donna du lait dans une coupe; elle lui présenta le beurre que l'on offre aux grands;
Aliomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
26 Elle étendit sa main gauche vers le clou et sa main droite vers le marteau des travailleurs; elle en frappa Sisara, elle fit entrer le clou dans sa tête, et elle frappa encore, et elle poussa le clou au travers de sa tempe.
Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
27 Et il roula entre ses pieds, il défaillit, et il mourut entre ses pieds; il s'était étendu devant elle, et il mourut dans son sommeil, et, au lieu même ou il s'était endormi, la vie l'abandonna.
Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Pale alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
28 La mère de Sisara s'est penchée à sa fenêtre, et, regardant par le treillis, elle a dit: Pourquoi son char tarde-t-il? D'où vient que son attelage se fait attendre?
“Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa?’
29 Les sages princesses qui l'entouraient lui ont répondu, et elle-même a répété leurs paroles:
Wanawake wenye busara kuliko wengine wote wakamjibu; naam, husema moyoni mwake,
30 Ne le trouvera-t-on pas distribuant le butin? Mais elle pleurera, et pleurera sur la tête de l'homme; des étoffes teintes pour Sisara, des étoffes teintes de couleurs diverses, de riches étoffes, des dépouilles, tout autour de sa tête!
‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: yote haya yakiwa nyara?’
31 Ainsi périssent tous vos ennemis, ô Seigneur! Que ceux qui aiment le Seigneur soient comme le lever du soleil dans toute sa puissance. La terre ensuite fut en repos durant quarante années.
“Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana! Bali wote wakupendao na wawe kama jua lichomozavyo kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.

< Juges 5 >