< Josué 7 >

1 Mais, les fils d'Israël commirent un grand péché; ils violèrent l'anathème, et Achar, fils de Charmi, fils de Zamhri, fils de Zaré, de la tribu de Juda, prit une part de ce qui était anathème; et le Seigneur fut rempli de colère contre les fils d'Israël.
Lakini Waisraeli hawakuwa waaminifu kuhusu vile vitu vilivyowekwa wakfu; Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, alivichukua baadhi ya hivyo vitu. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli.
2 Josué, à ce moment, envoya des hommes en Haï, qui est vers Bethel, disant: Allez reconnaître Haï.
Basi Yoshua akatuma watu kutoka Yeriko waende Ai, karibu na Beth-Aveni mashariki ya Betheli, akawaambia, “Pandeni mkaipeleleze nchi.” Basi wale watu wakapanda wakaipeleleza Ai.
3 Les hommes montèrent donc, observèrent Haï, retournèrent auprès de Josué, et lui dirent: Ne fais pas monter tout le peuple; que seulement deux ou trois mille hommes partent, et ils réduiront la ville; ne conduis pas là le peuple entier, car ils sont en petit nombre.
Waliporudi kwa Yoshua, wakasema, “Si lazima watu wote waende kupigana na Ai. Watume watu elfu mbili au tatu wakauteke huo mji. Usiwachoshe watu wote, kwa sababu huko kuna watu wachache tu.”
4 Et trois mille combattants environ montèrent; mais, ils s'enfuirent devant les hommes d'Haï.
Basi wakapanda kama watu elfu tatu tu, lakini wakashambuliwa na watu wa Ai,
5 Les hommes d'Haï en tuèrent trente-six; puis, ils les poursuivirent à partir de la porte de la ville, et ils les accablèrent de coups sur les pentes de la colline. Le cœur du peuple en fut frappé d'effroi, et son courage fut comme l'eau qui s'écoule.
ambao waliwaua watu kama thelathini na sita miongoni mwao. Wakawafukuza Waisraeli kutoka lango la mji hadi Shebarimu, nao wakawauwa huko kwenye materemko. Kutokana na hili mioyo ya watu ikayeyuka ikawa kama maji.
6 Josué alors déchira ses vêtements, Josué resta jusqu'au soir devant le Seigneur, la face contre terre, avec les anciens d'Israël, et ils se jetèrent des cendres sur la tête.
Ndipo Yoshua akayararua mavazi yake, akaanguka kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana, na akabakia hapo mpaka jioni. Wazee wa Israeli nao wakafanya vivyo hivyo wakatia mavumbi vichwani mwao.
7 Et Josué dit: Je vous conjure, Seigneur, pourquoi votre serviteur a-t-il fait passer le Jourdain à ce peuple pour être livré à l'Amorrhéen et périr? Que ne sommes-nous restés, que ne nous sommes-nous établis sur l'autre rive!
Yoshua akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, kwa nini umewavusha watu hawa ngʼambo ya Yordani ili kututia mikononi mwa Waamori watuangamize? Laiti tungeliridhika kukaa ngʼambo ile nyingine ya Yordani!
8 Et que dirai-je, maintenant qu'Israël a tourné le dos devant son ennemi?
Ee Bwana, niseme nini sasa, ikiwa sasa Israeli ameshafukuzwa na adui zake?
9 A cette nouvelle le Chananéen et tous ceux qui habitent cette terre, vont nous envelopper, et ils nous feront disparaître de leur terre; et alors que ferez-vous pour glorifier votre nom?
Wakanaani na watu wengine wa nchi watasikia habari hii, nao watatuzunguka na kutufutilia jina letu duniani. Utafanya nini basi kwa ajili ya jina lako mwenyewe lililo kuu?”
10 Et le Seigneur dit à Josué: Lève-toi; pourquoi donc es-tu tombé la face contre terre?
Bwana akamwambia Yoshua, “Simama! Unafanya nini hapo chini kifudifudi?
11 Le peuple a péché; ils ont violé l'alliance que j'ai faite avec lui, en dérobant, pour la mettre parmi leurs meubles, une part de l'anathème.
Israeli ametenda dhambi. Wamekiuka agano langu nililowaamuru kulishika. Wamechukua baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu, wameiba, wamesema uongo, wameviweka pamoja na mali zao.
12 Les fils d'Israël ne peuvent donc pas résister à leurs ennemis; ils fuiront devant eux, parce qu'ils sont devenus anathèmes, Je ne continuerai plus d'être avec vous, à moins que vous ne retranchiez l'anathème du milieu de vous.
Ndiyo sababu Waisraeli hawawezi kusimama dhidi ya adui zao. Wanawapa visogo na kukimbia kwa kuwa wanastahili maangamizi. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka mwangamize kila kitu miongoni mwenu kilichotengwa kwa maangamizi.
13 Lève-toi, purifie le peuple, prescris-lui de se purifier pour demain; dis-lui; Voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël: Un anathème est parmi vous, et vous ne pourrez point résister à vos ennemis jusqu'à ce que vous ayez retranché l'anathème du milieu de vous.
“Nenda, ukawatakase watu. Waambie, ‘Jitakaseni mjiandae kwa kesho; kwa sababu hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Kitu kilichowekwa wakfu kipo katikati yenu, ee Israeli. Hamwezi kusimama dhidi ya adui zenu mpaka mtakapokiondoa.
14 Vous vous rassemblerez tous, par tribus, demain au matin, et il y aura une tribu que désignera le Seigneur; vous ferez avancer chaque famille, et, dans celle que désignera le Seigneur, vous ferez avancer chaque maison, et, dans celle que désignera le Seigneur, vous ferez avancer chaque homme;
“‘Asubuhi, mjihudhurishe kabila kwa kabila. Itakuwa kabila lile atakalolitwaa Bwana litakuja mbele ukoo kwa ukoo, ukoo ule atakaoutwaa Bwana utakuja mbele jamaa kwa jamaa, nayo jamaa ile atakayoitwaa Bwana itakuja mbele mtu kwa mtu.
15 Et l'homme que désignera le Seigneur, sera consumé par le feu avec tout ce qui lui appartient, parce qu'il a violé l'alliance du Seigneur, et qu'il a commis un péché en Israël.
Yule atakayekutwa na vitu vilivyowekwa wakfu, atateketezwa kwa moto, pamoja na vitu vyote alivyo navyo. Kwa kuwa amelivunja agano la Bwana na kufanya kitu cha aibu katika Israeli!’”
16 Et Josué, de grand matin, rassembla le peuple par tribus, et la tribu de Juda fut désignée.
Kesho yake asubuhi na mapema Yoshua akawaamuru Israeli kuja mbele kabila kwa kabila; na Yuda akatwaliwa.
17 Elle s'avança par familles, et la famille de Zaré fut désignée; elle s'avança homme par homme,
Koo za Yuda zikaja mbele, naye akawatwaa Wazera. Akaamuru ukoo wa Wazera kuja mbele jamaa kwa jamaa, nayo jamaa ya Zabdi ikatwaliwa.
18 Et Achar, fils de Zambri, fils de Zaré, fut désigné
Yoshua akaamuru watu wa jamaa ya Zabdi kuja mbele mtu kwa mtu, naye Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, akatwaliwa.
19 Et Josué dit à Achar: Glorifie aujourd'hui le Seigneur Dieu d'Israël, donne confession à Dieu, et déclare-moi ce que tu as fait; ne me cache rien.
Ndipo Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, mtukuze Bwana, Mungu wa Israeli, nawe ukiri kwake. Niambie ni nini ulichotenda; usinifiche.”
20 Or, Achar répondit à Josué, et il lui dit: Véritablement j'ai péché devant le Seigneur Dieu d'Israël. Voici ce que j'ai fait.
Akani akamjibu Yoshua, “Ni kweli! Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana, Mungu wa Israeli. Hili ndilo nililofanya:
21 J'ai vu dans le butin un vêtement bigarré, deux cents sicles d'argent, un lingot d'or du poids de cinquante sicles, et, les ayant convoités, je les ai pris. Je les ai cachés sous ma tente, l'argent au-dessous de tout le reste.
Nilipoona katika nyara joho zuri la kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kabari ya dhahabu ya uzito wa shekeli hamsini, nikavitamani na nikavichukua. Tazama, vimefichwa ardhini ndani ya hema langu, pamoja na hiyo fedha chini yake.”
22 Aussitôt, Josué dépêcha des hommes qui coururent à la tente dans le camp; et les objets étaient cachés dans la tente d'Achar, et l'argent au-dessous de tout le reste.
Kwa hiyo Yoshua akatuma wajumbe, nao wakapiga mbio mpaka hemani, tazama, vile vitu vilikuwa vimefichwa hemani mwake, pamoja na ile fedha chini yake.
23 Ils les retirèrent de la tente, et les ayant apportés à Josué et aux anciens d'Israël, ils les déposèrent devant le Seigneur.
Wakavichukua vile vitu toka mle hemani, wakamletea Yoshua pamoja na Waisraeli wote, na wakavitandaza mbele za Bwana.
24 Et Josué saisit Achar, fils de Zaré, et il le conduisit à la vallée d'Achor, avec ses fils, ses filles, son bétail, ses bêtes de somme, ses brebis, sa tente et tout ce qui lui appartenait. Tout le peuple le suivit, et il les mena en Emécachor.
Basi Yoshua, pamoja na Israeli yote, wakamchukua Akani mwana wa Zera, pamoja na ile fedha, lile joho, ile kabari ya dhahabu, wanawe na binti zake, ngʼombe, punda na kondoo wake, hema yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta katika Bonde la Akori.
25 Là, Josué dit à Achar: Pourquoi nous as-tu perdus? Que de même le Seigneur t'extermine aujourd'hui. Et tout Israël le lapida.
Yoshua akasema, “Kwa nini umeleta taabu hii juu yetu? Bwana ataleta taabu juu yako leo hii.” Ndipo Israeli yote ikampiga Akani kwa mawe, na baada ya kuwapiga jamaa yake yote kwa mawe, wakawateketeza kwa moto.
26 Puis, ils formèrent sur lui un grand monceau de de pierres, et le Seigneur apaisa son courroux. A cause de cela, ce lieu, jusqu'à nos jours, s'est appelé Emécachor (Vallée du trouble.)
Wakakusanya lundo la mawe juu ya Akani, ambalo lipo mpaka leo. Naye Bwana akageuka kutoka hasira yake kali. Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Bonde la Akori tangu siku hiyo.

< Josué 7 >