< Josué 22 >

1 Alors, Josué convoqua les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé.
Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
2 Et il leur dit: Vous avez obéi à tout ce que vous avait ordonné Moïse, serviteur de Dieu; vous avez été dociles à ma voix, quand je vous ai rappelé tout ce qu'il vous avait prescrit.
Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
3 Vous n'avez point abandonné vos frères, durant tous ces jours nombreux, et jusqu'à ce moment vous avez exécuté l'ordre du Seigneur notre Dieu.
Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
4 Or, maintenant le Seigneur notre Dieu a donné la paix à nos frères, comme il le leur avait promis. Partez donc, retournez en vos demeures et dans la terre que Moïse vous a assignée au delà du Jourdain.
Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
5 Mais veillez diligemment à mettre en pratique les commandements et la loi que Moïse, serviteur de Dieu, vous a ordonné de pratiquer, savoir: d'aimer le Seigneur votre Dieu, de marcher en toutes ses voies, d'observer ses commandements, de vous attacher étroitement à lui, de le servir de tout votre esprit et de toute votre âme.
Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
6 Et Josué les bénit, les congédia, et ils retournèrent en leurs demeures.
Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
7 (Moïse avait donné des terres à la demi-tribu de Manassé dans le royaume de Basan, et Josué en avait donné à l'autre demi-tribu parmi leurs frères de ce côté du Jourdain à l'occident.) Lorsque Josué les renvoya dans leurs demeures, et qu'il les bénit,
Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
8 Ils retournèrent en leurs demeures avec beaucoup de richesses. Ils avaient partagé avec leurs frères un immense butin fait sur les ennemis: de nombreux troupeaux de bétail, de l'argent, de l'or et du fer, et beaucoup de vêtements.
na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
9 Les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé se séparèrent donc des fils d'Israël à Silo, dans la terre de Chanaan, pour retourner en Galaad, dans la contrée qu'ils possédaient, et que le Seigneur, par la main de Moïse, leur avait donnée pour héritage.
Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
10 Et ils arrivèrent en Galaad sur le Jourdain, qui est dans la terre de Chanaan. Et les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé bâtirent en ce lieu, sur la rive du Jourdain, un grand autel qu'on apercevait de loin.
Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
11 Or, les fils d'Israël l'apprirent de gens qui leur dirent: Voilà que les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, ont bâti un autel sur les confins de la terre de Chanaan, en Galaad aux bords du Jourdain, hors du territoire des fils d'Israël.
Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
12 Aussitôt, tous les fils d'Israël se rassemblèrent en Silo, pour s'en aller leur faire la guerre.
Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
13 Et les fils d'Israël envoyèrent aux fils de Ruben, aux fils de Gad, et aux fils de la demi-tribu de Manassé, en la terre de Galaad, Phinées, fils d'Eléazar, fils d'Aaron le grand prêtre,
Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
14 Et avec lui dix chefs, chacun chef d'une famille paternelle de toutes les tribus d'Israël; ces chefs de famille, en Israël, sont commandants de mille hommes.
na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
15 Ils se rendirent auprès des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi- tribu de Manassé, en la terre de Galaad, et ils leur parlèrent, disant:
Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
16 Toute la synagogue du Seigneur dit ces choses: Quel est ce péché que vous avez commis devant le Dieu d'Israël, en vous détournant aujourd'hui du Seigneur, et en vous bâtissant un autel, pour être des apostats du Seigneur?
“Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
17 Est-ce si peu de chose à vos yeux que le crime de Phogor dont nous ne sommes pas encore purifiés, et qui a été une plaie dans la synagogue du Seigneur?
Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
18 Et vous, vous vous détournez du Seigneur; or, si vous vous en détournez aujourd'hui, demain sa colère éclatera contre tout Israël.
Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
19 Mais quoi! la terre que vous possédez est-elle trop petite? Passez dans la terre que possède le Seigneur, dans celle où est dressé le tabernacle du Seigneur; venez la partager avec nous, et ne vous détournez pas du Seigneur; ne soyez pas apostats du Seigneur en élevant un autel autre que l'autel du Seigneur notre Dieu.
Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
20 N'avez-vous pas vu Achar, fils de Zaré, quand il a péché au sujet de l'anathème? La colère du Seigneur n'a-t-elle pas éclaté contre tout Israël? A-t-il péri seul à cause du péché que lui seul avait commis?
Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
21 Les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, répondirent aux chefs d'Israël, et ils dirent:
Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
22 Dieu est le Seigneur Dieu, et Dieu, Dieu lui-même sait, et toute la synagogue d'Israël saura si nous avons commis contre le Seigneur le péché d'apostasie; si cela est, qu'il cesse dès ce jour de nous protéger.
“Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
23 Si nous avons bâti pour nous un autel en esprit d'apostasie contre le Seigneur notre Dieu, pour brûler sur cet autel des holocaustes, y offrir des hosties pacifiques, le Seigneur se vengera.
kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
24 Mais nous avons fait cela par précaution, de peur que plus tard vos enfants ne disent aux nôtres: Qu'y a-t-il entre vous et le Dieu d'Israël?
La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
25 Le Seigneur vous a séparés de nous par le Jourdain, et vous n'avez point part au Seigneur. Ainsi, vos fils repousseront nos fils comme des étrangers, pour qu'ils n'honorent point le Seigneur.
Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
26 Nous avons donc résolu d'élever cet autel, non pour y faire des oblations, non pour y sacrifier des victimes,
Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
27 Mais pour qu'il soit entre vous et nous, entre votre postérité et la nôtre, un témoignage du culte que nous rendrons au Seigneur devant son tabernacle, par nos oblations de fruits, nos victimes et nos hosties pacifiques; de sorte que plus tard vos enfants ne disent point aux nôtres: Vous n'avez point part au Seigneur.
ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
28 Et nous avons dit: S'il arrive un jour qu'ils tiennent ce langage à nous ou à notre postérité, il leur sera répondu: Voyez cette image de l'autel du Seigneur que nos pères ont faite, non pour y offrir des fruits ou des victimes, mais pour qu'elle soit un témoignage entre vous et nous et entre nos fils.
Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
29 Que Dieu nous préserve donc aujourd'hui de nous détourner du Seigneur, d'être apostats du Seigneur, au point de bâtir pour nous un autel d'holocaustes et d'hosties pacifiques, autre que l'autel du Seigneur qui existe devant son tabernacle.
Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
30 Après avoir entendu les explications des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi-tribu de Manassé, Phinées le prêtre, et les chefs de la synagogue d'Israël en furent réjouis,
Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
31 Et Phinées le prêtre dit aux fils de Ruben, aux fils de Gad et à la demi- tribu de Manassé: Nous reconnaissons maintenant que le Seigneur est avec vous, parce que vous n'avez point commis de péché contre le Seigneur, et que vous sauvez les fils d'Israël de la main du Seigneur.
Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
32 Et Phinées le prêtre, et les chefs, quittant les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, retournèrent de la terre de Galaad en celle de Chanaan auprès des fils d'Israël, et ils leur rapportèrent tout ce qui s'était dit.
Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
33 Et cela réjouit les fils d'Israël; et, après leur avoir parle, ils bénirent tous le Dieu des fils d'Israël, et ils renoncèrent à marcher contre eux en guerre, et à ravager le domaine des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi-tribu de Manassé, qui continuèrent de l'habiter.
Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
34 Et Josué appela l'autel des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi- tribu de Manassé: Autel du témoignage, parce que, dit-il, il rend entre eux témoignage que le Seigneur est leur Dieu.
Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”

< Josué 22 >