< Josué 14 >

1 Et voici ceux des fils d'Israël qui eurent en la terre de Chanaan des héritages que leur distribuèrent le prêtre Eléazar, Josué, fils de Nau, et les chefs de famille des tribus d'Israël.
Basi haya ndiyo maeneo Waisraeli waliyopokea kama urithi katika nchi ya Kanaani, ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliwagawia.
2 Ils les distribuèrent par la voie du sort aux neuf tribus et à la demi- tribu de Manassé, de la manière que le Seigneur avait prescrite a Josué, à partir de la rive occidentale du Jourdain.
Urithi wao uligawanywa kwa kura kwa yale makabila tisa na nusu, kama Bwana alivyoamuru Mose.
3 Et parmi eux, Josué ne donna point d'héritage aux lévites,
Mose alikuwa amewapa yale makabila mawili na nusu urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi miongoni mwa hao wengine,
4 Attendu que des fils de Joseph étaient issues les deux tribus de Manassé et d'Ephraïm. Et il ne fut point attribué de part aux lévites dans la terre promise, mais des villes pour habitation, et du bétail, et des banlieues, réservées pour leurs bestiaux.
kwa kuwa wana wa Yosefu walikuwa makabila mawili; Manase na Efraimu. Walawi hawakupata mgawo wa ardhi, bali walipewa miji tu kwa ajili ya kuishi, pamoja na maeneo ya malisho kwa ajili ya makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe wao.
5 Les fils d'Israël exécutèrent ce que leur avait prescrit Moïse, et ils partagèrent la terre promise.
Kwa hiyo Waisraeli wakagawana ile nchi, kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
6 Les fils de Juda vinrent trouver Josué en Galgala, et Caleb, fils de Jephoné le Cénézéen, lui parla en ces termes: Tu sais la parole qu'a dite le Seigneur à Moïse, homme de Dieu en Cadès-Barné, concernant moi et toi-même.
Kisha watu wa Yuda wakamwendea Yoshua huko Gilgali, naye Kalebu mwana wa Yefune yule Mkenizi, akamwambia, “Unajua jambo ambalo Bwana alimwambia Mose mtu wa Mungu huko Kadesh-Barnea kukuhusu wewe na mimi.
7 Car j'avais quarante ans, lorsque Moïse, serviteur de Dieu, m'envoya de Cadès-Barné, pour reconnaître cette terre. Et je lui fis un rapport, selon sa pensée.
Nilikuwa na umri wa miaka arobaini, wakati Mose mtumishi wa Bwana, aliponituma kutoka Kadesh-Barnea kuipeleleza hiyo nchi. Nami nikamletea taarifa kama kulingana na nilivyosadiki moyoni.
8 Mes frères, ceux qui étaient montés avec moi, firent changer le cœur du peuple; et moi je persistai à suivre le Seigneur mon Dieu.
Lakini ndugu zangu tuliopanda nao waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa hofu. Bali mimi, nilimfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.
9 Ce jour-là, Moïse me fit une promesse, disant: La terre sur laquelle tu as marché sera ton héritage et celui de tes enfants à perpétuité, parce que tu as persisté à suivre le Seigneur notre Dieu.
Hivyo katika siku ile, Mose akaniapia, ‘Nchi ambayo umeikanyaga kwa miguu yako itakuwa urithi wako na wa watoto wako milele, kwa sababu umemfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.’
10 Et maintenant, le Seigneur m'a conservé, comme il l'avait dit: Nous sommes dans la quarante-cinquième année depuis le jour où le Seigneur a dit cette parole à Moïse. Or, Israël a erré dans le désert, et aujourd'hui voilà que j'ai quatre-vingt-cinq ans.
“Sasa basi, kama vile Bwana alivyoahidi, ameniweka hai kwa miaka arobaini na mitano tangu wakati alipomwambia Mose jambo hili, wakati Waisraeli wakiwa wanazunguka jangwani. Hivyo mimi hapa leo, nina umri wa miaka themanini na mitano!
11 Je suis encore aussi robuste que lorsque Moïse m'a envoyé; j'ai encore la même vigueur à la guerre pour entrer et sortir.
Bado ninazo nguvu kama siku ile Mose aliponituma. Bado ninazo nguvu za kwenda vitani sasa kama vile nilivyokuwa wakati ule.
12 Je te demande donc cette montagne, selon ce que ce jour-là m'a promis le Seigneur, parce que ce jour-là, tu as entendu sa promesse. Maintenant voici les villes d'Enac grandes et fortifiées. Si donc le Seigneur est avec moi, j'exterminerai ceux qui les habitent, comme me l'a dit le Seigneur.
Basi nipe nchi hii ya vilima, ambayo Bwana aliniahidi siku ile. Wewe mwenyewe ulisikia wakati ule kwamba Waanaki walikuwako huko na miji yao ilikuwa mikubwa na yenye maboma, lakini, kwa msaada wa Bwana, nitawafukuza watoke huko kama vile alivyonena.”
13 Et Josué le bénit, et il donna la ville d'Hébron pour héritage à Caleb, fils de Jéphoné, frère de Cénez.
Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune, na akampa Hebroni kama urithi wake.
14 A cause de cela, Hébron est restée jusqu'à ce jour l'héritage de Caleb, fils de Jéphoné le Cénézéen, pour sa fidélité à suivre les commandements du Seigneur Dieu d'Israël.
Hivyo Hebroni imekuwa mali ya Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi tangu wakati ule, kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wote.
15 Le nom d'Hébron était autrefois Argob; c'était la métropole de la race d'Enac. Et la terre fut en repos après les combats.
(Hebroni uliitwa Kiriath-Arba hapo mwanzo, kutokana na huyo Arba ambaye alikuwa mtu mkuu kupita wote miongoni mwa Waanaki.) Kisha nchi ikawa na amani bila vita.

< Josué 14 >