< Jonas 3 >

1 Et la parole du Seigneur vint à Jonas pour la seconde fois, disant
Ndipo neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili:
2 Lève-toi, et pars pour Ninive, la grande ville, et proclame dans ses murs la prédiction que Je t'ai déjà prescrit de proclamer.
“Ondoka uende katika mji mkubwa wa Ninawi, ukautangazie ujumbe ninaokupa.”
3 Et Jonas se leva; et il s'en alla à Ninive, comme lui avait dit le Seigneur. Or la ville de Ninive était grande de trois jours de marche.
Yona akalitii neno la Bwana naye akaenda Ninawi. Basi Ninawi ulikuwa mji maarufu sana, ilichukua siku tatu kuuzunguka.
4 Et Jonas commença par entrer dans la ville et par faire environ un jour de marche, et il cria, et il dit: Encore trois jours, et Ninive sera détruite!
Siku ya kwanza, Yona aliingia mjini. Akatangaza: “Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.”
5 Et les hommes de Ninive crurent en Dieu, et ils proclamèrent un jeûne, et ils se ceignirent de cilices, depuis le grand jusqu'au petit.
Watu wa Ninawi wakamwamini Mungu, wakatangaza kufunga, watu wote kuanzia mkubwa sana hadi yule mdogo kabisa, wakavaa nguo za gunia.
6 Et la parole de Jonas arriva au roi de Ninive, et il se leva de son trône, et il ôta sa robe, et il se ceignit d'un cilice, et il s'assit sur la cendre.
Habari zilipomfikia mfalme wa Ninawi, aliondoka kwenye kiti chake cha enzi, akavua majoho yake ya kifalme, akajifunika nguo ya gunia kisha akaketi chini mavumbini.
7 Et il fut proclamé, et il fut dit en Ninive de la part du roi et de la part de ses grands, ce qui suit: Que ni hommes, ni bêtes, ni bœufs, ni brebis ne mangent, ne paissent, ne boivent même de l'eau.
Ndipo akatoa tangazo katika Ninawi yote: “Kwa amri ya mfalme na wakuu wake: “Msiruhusu mtu yeyote au mnyama, makundi ya ngʼombe au wanyama wengine wafugwao, kuonja kitu chochote, msiwaruhusu kula wala kunywa.
8 Et les hommes et les bêtes furent couverts de cilices, et les hommes crièrent sans relâche au Seigneur. Et chacun revint de sa voie coupable et de l'iniquité de ses mains, disant:
Bali wanadamu na wanyama wafunikwe kwa nguo za gunia. Kila mmoja afanye hima kumwomba Mungu. Waziache njia zao mbaya na udhalimu ulio mikononi mwao.
9 Qui sait si le Seigneur ne Se repentira pas, et s'Il ne calmera pas les transports de Sa colère, pour que nous ne périssions point?
Ni nani ajuaye? Huenda Mungu akaghairi kwa huruma yake akaacha hasira yake kali ili tusiangamie.”
10 Et Dieu vit leurs œuvres; Il vit qu'ils revenaient de leurs voies coupables; et Dieu Se repentit du mal qu'Il avait voulu leur faire, et Il ne le leur fit pas.
Mungu alipoona walivyofanya na jinsi walivyogeuka kutoka njia zao mbaya, akawa na huruma wala hakuleta maangamizi juu yao kama alivyokuwa ameonya.

< Jonas 3 >