< Jonas 1 >

1 Et la parole du Seigneur vint à Jonas, fils d'Amathi, disant
Ndipo neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amittai, kusema,
2 Lève-toi, et pars pour Ninive, la grande ville, et proclame dans ses murs que le cri de sa méchanceté est monté jusqu'à Moi.
“Simama uende Ninawi, mji kuu, na ukapaze sauti dhidi yake, kwa sababu uovu wao umeinuka mbele yangu.”
3 Et Jonas se leva pour s'enfuir à Tharsis, loin de la face du Seigneur; et il descendit à Joppé; il y trouva une barque allant à Tharsis, et il paya son passage, et il s'embarqua pour naviguer avec les matelots, jusqu'à Tharsis, loin de la face du Seigneur.
Lakini Yona akaondoka kukimbia kutoka mbele ya Bwana na kwenda Tarshishi. Akatelemka mpaka Yafa na akaona melikebu inayokwenda Tarshishi. Kwa hiyo alilipa nauli na akapanda melikebu kwenda nayo Tarishishi, mbali na uwepo wa Yahweh.
4 Et le Seigneur excita un grand vent sur la mer, et les vagues s'élevèrent, et la barque fut en danger de se rompre.
Lakini Bwana akatuma upepo mkubwa juu ya bahari, ikawa tufani juu ya bahari. Hivi karibuni ikaonekana kwamba meli ilikuwa inataka kuvunjika.
5 Et les matelots eurent crainte, et ils crièrent chacun vers son dieu, et ils lancèrent à la mer le chargement de la barque, pour s'en alléger. Jonas descendit à fond de cale, et là il s'endormit, et il ronfla.
Wale baharia waliogopa sana na kila mtu alilia kwa mungu wake mwenyewe. Wakatupa mizigo bahari iliyokuwa merikebuni ili kuifungua. Yona alikuwa ameshuka hapa pande za ndani ya melikebu, naye alikuwa amelala huko usingizi.
6 Et le pilote l'alla trouver, et il lui dit: Pourquoi ronfles-tu? Lève- toi, et invoque ton Dieu, afin que Dieu nous sauve, et que nous ne mourions pas.
Basi nahoza akamwendea akamwambia, “kwa nini unalala? Amka! ukamwombe mungu wako! Labda mungu wako atatutambua na hatutapotea.”
7 Et chacun des matelots dit à son voisin: Allons, agitons les sorts, et sachons par qui ce malheur nous arrive. Et ils agitèrent des sorts, et le sort tomba sur Jonas.
Wote wakaambiana, 'Njoni, tupige kura, ili tujue ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata.' Basi wakapiga kura, na kura ikaangukia kwa Yona.
8 Et ils lui dirent: Déclare-nous quel est ton métier; d'où viens-tu? de quelle contrée, de quel peuple es-tu?
Kisha wakamwambia Yona, “Tafadhali tuambie ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata. Unafanya kazi gani, na umetoka wapi? Nchi yako ni ipi, na kutoka kwa watu wa kabila gani?”
9 Et il leur dit: Je suis un serviteur du Seigneur; j'adore le Seigneur Dieu du ciel, qui a créé la mer et la terre.
Yona akawaambia, Mimi ni Mhebrania; Nami namuogopa Bwana, Mungu wa mbinguni, aliyeifanya bahari na nchi kavu.
10 Et ces hommes eurent grande crainte, et ils lui dirent: Pourquoi as-tu fait cela? Car ces hommes connurent qu'il fuyait loin de la face du Seigneur; car il le leur avait déclaré.
Ndipo watu hao waliogopa zaidi, wakamwambia Yona, Ni jambo gani hili ulilolifanya? Kwa maana hao watu walijua kwamba alikuwa akikimbia mbele ya Bwana, kwa sababu alikuwa amewaambia.
11 Et ils lui dirent: Que te ferons-nous, afin que pour nous la mer se calme? Car la mer allait, et soulevait encore plus de vagues.
Ndipo wakamwambia Yona, Tukufanyie nini ili bahari iweze kutulia? Kwa maana bahari ilikuwa imechafuka zaidi na zaidi.
12 Et Jonas leur dit: Prenez-moi et jetez-moi à la mer, et la mer se calmera pour vous; car je sais que c'est à cause de moi qu'il y a contre vous ces grandes vagues.
Yona akawaambia, “Nikamateni na nitupeni baharini. Kisha bahari itatulia kwa ajili yenu, kwa maana najua kwamba ni kwa sababu yangu kwamba tufani hii kubwa iwapate.”
13 Et ces hommes s'efforcèrent de retourner à la côte; mais ils ne le purent, parce que la mer allait et soulevait contre eux toujours plus de vagues.
Hata hivyo, watu hao wavuta makasia kwa bidii ili kurudi nchi kavu, lakini hawakuweza kufanya hivyo kwa sababu bahari ilikuwa imechafuka zaidi dhidi yao.
14 Et ils crièrent au Seigneur, et ils dirent: Non, Seigneur, que nous ne périssions pas pour la vie de cet homme; ne fais pas retomber sur nous un sang innocent; car, Seigneur, Tu as fait selon Ta volonté.
Basi wakamwomba Bwana, wakasema, Tunakuomba, Bwana, tunakuomba, usiache tuangamize kwa sababu ya maisha ya mtu huyu; wala usituwekee hatia ya kufa kwake, kwa kuwa wewe, Bwana, umefanya kama ulivyopenda.
15 Et ils prirent Jonas, et ils le lancèrent à la mer; et la mer cessa de s'agiter.
Basi wakamchukua Yona wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka.
16 Et ces hommes eurent grande crainte du Seigneur; et ils offrirent au Seigneur un sacrifice, et ils Lui firent des vœux.
Ndipo watu wale wakamuogopa Bwana sana. Wakamtolea dhabihu Bwana na kuweka nadhiri.
17 Et le Seigneur prescrivit à une grande baleine d'avaler Jonas, et Jonas fut dans le ventre de la baleine trois jours et trois nuits.
Bwana alikuwa ameandaa samaki mkubwa kummeza Yona, na Yona alikuwa ndani ya tumbo lasamaki siku tatu na usiku wa tatu.

< Jonas 1 >