< Job 40 >

1 Et le Seigneur Dieu, continuant à parler à Job dit:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Est-ce qu'il décline la justice du Tout-Puissant? Celui qui a adressé des reproches au Seigneur doit lui répondre.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Et Job, reprenant, dit au Seigneur:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Pourquoi m'obstinerais-je à contester? Je me tiens pour averti; j'ai osé blâmer le Seigneur, et j'ai ouï de telles paroles, moi qui ne suis rien! Que pourrais-je répliquer? Je n'ai plus qu'à me mettre la main sur la bouche.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 J'ai parlé une fois; je me garderai bien de parler encore.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Et le Seigneur, continuant, dit à Job, à travers la nuée:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Nullement, mais ceins-toi les reins comme un homme; je vais te questionner, tu me répondras.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Ne refuse pas mon jugement: crois-tu que j'aie conversé avec toi, sinon pour que tu apparaisses juste?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Ton bras est-il le bras du Seigneur? ta voix est-elle comme son tonnerre?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Revêts-toi de grandeur et de puissance; orne-toi d'honneur et de gloire.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Envoie des anges dans ta colère, humilie tout orgueilleux.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Eteins les vaines splendeurs, fais tomber soudain l'impie en pourriture.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Cache les pécheurs ensemble sous la terre; couvre leurs fronts de honte.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Je confesserai alors que ta main peut sauver.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Mais vois auprès de toi les bêtes fauves; elles se repaissent d'herbe comme les bœufs.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 La vigueur de la bête est dans ses reins; sa force dans ses entrailles.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Elle dresse sa queue comme un cyprès; ses nerfs sont liés entre eux.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Ses côtes sont des côtes d'airain; son échine est de fer fondu.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Elle est le commencement de l'œuvre du Seigneur, créée pour être raillée par les anges.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Lorsqu'elle a gravi sur les cimes des monts, elle a réjoui les quadrupèdes dans le Tartare.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Elle se couche sous toute sorte d'arbre; auprès du papyrus, de l'herbe ou du roseau.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 L'ombre des grands rameaux la couvre, ou les jeunes tiges des champs.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Vienne le flux de la mer, elle ne le sentira pas; elle ne craint rien; le Jourdain même se briserait sur sa gueule.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 D'un coup d'œil elle réprimera son choc; pris au piège, il frémira jusqu'en ses narines.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >