< Job 34 >
1 Et Elihou, continuant dit:
Kisha Elihu akasema:
2 Ecoutez-moi, sages et savants; prêtez-moi une oreille attentive,
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 Car l'oreille juge les paroles, comme le gosier goûte les aliments.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 Servons-nous en pour décider; discernons entre elles ce qui est bon.
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 Job a dit: Je suis juste, le Seigneur m'a exclu du jugement;
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 Il m'a rendu suspect par son arrêt; le trait a été violent, sans que j'eusse commis d'iniquité.
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 Quel est l'homme qu'autant que Job on ait abreuvé de railleries, comme on abreuve d'eau?
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 Et je n'ai point péché, je n'ai rien fait contre Dieu; je n'ai rien de commun avec les méchants; je n'ai point marché avec les impies.
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 Ne tiens pas ce langage, car ce qui échappe à la surveillance de l'homme n'échappe pas à celle de Dieu;
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 C'est pourquoi, vous qui m'êtes unis par le cœur, soyez attentifs; puissé-je n'être point impie devant le Seigneur, et satisfaire à ce qui est juste devant le Tout-Puissant.
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 Qu'il rétribue chacun selon ses œuvres, et il saura bien trouver un homme sur sa voie.
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 Penses-tu Job, que le Seigneur fasse des choses vaines? Le Tout-Puissant fausse-t-il la justice, lui qui a créé la terre?
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 Qui donc a fait l'étendue que le ciel recouvre et tout ce qui l'habite?
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 S'il lui plaisait de s'abstenir, de retenir son souffle,
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 Toute chair au même instant périrait; tout homme retournerait à la terre dont il a été formé.
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 S'il ne t'a pas averti, écoute ce que je vais te dire, que tes oreilles le recueillent.
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 Considère toi-même celui qui hait les pervers, celui qui extermine les méchants, celui qui est éternellement juste.
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 Celui qui ne craint pas d'appeler un roi impie; ni de dire aux grands: vous êtes corrompus, vous vivez dans le péché.
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 Celui qui n'a aucun égard pour le rang; qui ne sait point honorer la force ni lui rendre des respects.
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 A prier un homme qui pratique l'iniquité, qui méconnaît les pauvres, on n'obtiendra que des choses vaines.
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 Mais Dieu voit les œuvres des mortels; rien de ce qu'ils font ne lui est caché.
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 Il n'est point de lieu où les pervers puissent se soustraire à ses regards.
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 Il ne s'y prend pas à deux fois pour juger un homme.
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 Le Seigneur surveille tout; il est l'auteur d'une multitude de merveilles incompréhensibles et glorieuses.
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 Il connaît les travaux des humains, sur eux il ramènera la nuit et ils seront humiliés.
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 Il a éteint les impies; il ne lui est point échappé
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 Qu'ils s'étaient écartés de la loi de Dieu, et qu'ils avaient méconnu ses préceptes.
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 Ils avaient contraint les pauvres de l'invoquer, et il exaucera toujours les indigents.
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 Seul il donne la paix, et qui donc fera condamner celui à qui il l'accorde? S'il cache son front, qui le verra? Il juge les nations comme les individus.
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 Il place sur le trône un roi hypocrite, à cause des caprices du peuple.
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 Il en est qui disent au Tout-Puissant: Si j'ai pris, je ne retiendrai rien en gage.
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 Je ne puis voir par moi-même; faites-moi connaître si j'ai commis quelque iniquité, et je ne recommencerai pas.
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 Est-il juste que vous m'en punissiez; ne deviez-vous pas la prévenir; n'est-ce pas vous qui choisissez et non moi? Ce que vous savez, déclarez-le.
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 S'il est vrai que des cœurs intelligents peuvent parler en ces termes, d'autre part c'est à un homme sage que je parle, et il m'écoute.
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 Job n'a point raisonné en homme habile, ses discours ne montrent pas de savoir.
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 O Job, réfléchis donc; ne réponds pas derechef à la manière des insensés.
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 De peur que nous n'ajoutions pas à nos fautes; car il nous sera imputé à péché de nous étendre en longs discours devant le Seigneur.
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”