< Job 31 >

1 J'avais fait un pacte avec mes yeux, disant: Je ne regarderai plus une vierge.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 Car quelle est la part que d'en haut m'a réservée le Seigneur; quel héritage dois-je attendre du Tout-Puissant qui règne au plus haut des cieux?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Malheur, perdition à l'injuste, expulsion pour celui qui fait le mal.
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Le Seigneur ne me tiendra-t-il pas compte de mes voies, ni de la manière dont j'ai marché?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 Si j'avais été le compagnon des railleurs; si j'avais porté mes pas du côté de la fraude!
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Mais je me suis maintenu sous le joug de la justice, et le Seigneur connaît mon innocence.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 Si mon pied s'est écarté du droit chemin, si mon cœur a été égayé par mes yeux, si mes mains ont touché des présents,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Que d'autres consomment ce que j'ai semé, que sur la terre je devienne sans racines.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 Si mon cœur a convoité la femme d'autrui, si j'ai franchi ses portes,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Que ma femme plaise à un autre homme; que mes enfants soient humiliés.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 Rien ne peut apaiser la colère de Dieu contre celui qui souille la femme de son prochain.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Le feu s'attaquera à toute sa personne et dévorera tout ce qui sera issu de lui.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 Si j'avais faussé le jugement que je rendais sur mon serviteur et ma servante, lorsqu'ils recouraient à ma justice,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 Que ferais-je quand à mon tour le Seigneur me jugera? Qu'aurais-je à lui répondre, s'il m'avait surpris en quelque faute?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Ceux que j'avais à juger n'avaient-ils pas été comme moi, conçus en des entrailles? n'était-ce pas comme si les mêmes flancs nous avaient portés?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 Aussi les pauvres ont-ils toujours trouvé chez moi ce qui leur manquait; et je n'ai point fait verser de larmes à l'œil de la veuve.
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 Si j'ai mangé seul ma bouchée, si je n'en ai point fait part à l'orphelin;
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 Si dès ma jeunesse, à peine sorti du ventre de ma mère, je n'ai eu de lui des soins paternels;
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 Si j'ai méprisé l'homme nu et abandonné; si je ne l'ai point vêtu;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 Si les indigents ne m'ont point béni; si leurs épaules n'ont pas été réchauffées par les toisons de mes agneaux;
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 Si j'ai levé la main sur le pupille; si je n'ai point multiplié mes secours avec confiance;
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Que mon épaule se déboîte, que mon bras soit broyé au-dessous du coude.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 En vérité la crainte du Seigneur m'a saisi; je ne puis supporter ce qu'il m'envoie.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 Si j'avais amoncelé de l'or, si j'avais estimé surtout les pierres précieuses;
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 Si j'avais mis ma joie en de grandes richesses; si ma main s'était posée sur des trésors innombrables;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 Je me serais dit: N'ai-je point vu le soleil dans tout son éclat s'éclipser, et la lune au ciel périr? Et rien n'est au-dessus d'eux.
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 Et si mon cœur en secret s'est laissé séduire; et si j'ai baisé ma main en la portant à ma bouche,
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 Que ces fautes me soient gravement imputées; car alors j'ai menti au Seigneur Très-Haut.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 Et si je me suis réjoui de la chute de mes ennemis, et si dans mon âme j'ai dit: Bien!
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 Puisse mon oreille ouïr la malédiction qui sera portée contre moi; puissé-je être signalé à tout le peuple comme un méchant.
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 Si je n'ai pas été bon pour mes servantes, si elles ont dit de moi: Qui nous permettra de nous rassasier de sa chair?
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 Si j'ai laissé l'étranger passer la nuit en plein air, et si ma porte ne s'est pas ouverte à tout venant.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 Si ayant failli involontairement, j'ai caché mes péchés;
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Retenu par la honte de les avouer devant la multitude; si j'ai souffert que le pauvre sortît de ma maison l'estomac vide;
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Qui me donnera quelqu'un qui m'écoute? Si je n'ai point eu crainte de la main du Seigneur; le titre que j'avais contre autrui,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Que j'avais lu les épaules ceintes d'une couronne,
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 Si je ne l'ai point remis, après l'avoir déchiré, sans rien exiger du débiteur;
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 Si jamais la terre a gémi contre moi, si ses sillons ont pleuré tous ensemble,
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 Si j'ai consommé ses fruits seul et sans les payer; si en les empruntant j'ai affligé l'âme de son possesseur,
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Que les champs, au lieu de froment, ne produisent pour moi que des orties; et au lieu d'orge que des ronces. Et Job cessa de parler.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Job 31 >