< Job 29 >
1 Et Job, ajoutant à ce qui précède, dit:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Qui me rendra les jours d'autrefois, le temps où Dieu prenait de soin de me garder?
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Alors sa lampe brillait sur ma tête: alors avec sa lumière je ne craignais pas de marcher dans les ténèbres.
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Alors je foulais de mes pieds la voie; alors Dieu veillait sur ma maison.
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Alors je m'asseyais à l'ombre de mes arbres, et mes enfants étaient autour de moi.
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Alors mes sentiers ruisselaient de beurre et mes collines de lait.
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Alors j'entrais dès l'aurore en la ville, et un siège m'était réservé sur les places.
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Les jeunes gens à mon aspect se voilaient; et les anciens restaient debout.
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Les forts cessaient de parler; ils se mettaient un doigt sur la bouche.
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 Attentifs à mes discours, ils me déclaraient heureux, après quoi leur langue était collée à leur gosier.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 L'oreille m'avait ouï et l'on me proclamait heureux; l'œil m'avait vu et l'on s'inclinait.
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Car j'avais délivré le pauvre des mains du riche; j'avais protégé l'orphelin qui manquait d'appui.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 La bénédiction de l'abandonné s'adressait à moi; la bouche de la veuve aussi me bénissait.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Je m'étais revêtu de justice; je m'étais enveloppé d'équité comme d'un manteau double.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 J'étais l'œil de l'aveugle et le pied du boiteux.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 J'étais le père des faibles; j'étudiais des causes que je ne connaissais pas.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Aussi j'ai brisé les mâchoires de l'injuste; j'ai arraché de ses dents la proie qu'il avait saisie.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Et j'ai dit: Mon âge se prolongera comme celui du palmier; ma vie sera de longue durée.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 La racine se montrera hors de l'eau, et la rosée passera la nuit dans ma moisson.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Ma gloire est pour moi chose vaine, et elle marche mon arc à la main.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 A peine m'avait-on entendu que l'on s'attachait à moi; on gardait le silence en recueillant mes conseils.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Nul n'ajoutait à mes discours, et les hommes étaient pleins de joie que je leur avais parlé.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Comme la terre altérée reçoit la pluie, de même ils recevaient mes paroles.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Lorsque je riais avec eux, ils n'y pouvaient croire, et l'éclat de mon visage n'en était pas amoindri.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Je leur avais indiqué la voie, ils m'avaient institué leur chef, et ma demeure semblait celle d'un roi entouré de gardes ou d'un consolateur des affligés.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.