< Job 1 >

1 Il y avait en la terre de Hus, un homme appelé Job; et cet homme était intègre, irréprochable, juste, pieux, et il s'abstenait de toute mauvaise action.
Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
2 Et il avait sept fils et trois filles.
Alikuwa na wana saba na binti watatu,
3 Et ses troupeaux étaient sept mille moutons, trois mille chamelles, cinq cents paires de bœufs, cinq cents ânesses au pâturage, et il avait une multitude de serviteurs et de grands travaux sur la terre; et cet homme avait la noblesse des fils de l'Orient.
naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
4 Et ses fils, se réunissant tour à tour, faisaient chaque jour un festin, et ils accueillaient aussi leurs trois sœurs pour boire et manger avec eux.
Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
5 Et dès que leurs jours de repas étaient écoulés, Job, s'étant levé de grand matin, les convoquait; et il les purifiait, et il immolait autant de victimes que le comportait leur nombre et de plus un bœuf pour le péché de leurs âmes. Car Job disait: Qui sait si les fils au fond du cœur, n'ont pas eu de mauvaises pensées contre Dieu? Ainsi faisait donc Job toutes les fois.
Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
6 Or, l'un de ces jours-là, les anges de Dieu s'en vinrent comparaître devant le Seigneur, et le diable vint avec eux.
Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
7 Et le Seigneur dit au diable: D'où viens-tu? Et le diable répondit: J'arrive après avoir fait le tour de la terre et parcouru tout ce qui est sous le ciel.
Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
8 Et le Seigneur reprit: As-tu remarqué Job, mon serviteur? as-tu reconnu qu'il n'a point son pareil sur la terre, que c'est un homme irréprochable, sincère, pieux, et qui s'abstient de toute mauvaise action?
Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
9 Et le diable répondit et dit devant le Seigneur: Est-ce gratis que Job honore le Seigneur?
Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
10 N'avez-vous point fortifié sa maison, au-dedans comme au dehors, et, alentour tout ce qui lui appartient? n'avez-vous béni ses œuvres et multiplié ses troupeaux sur la terre?
Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
11 Mais étendez votre main et qu'elle touche à ce qu'il possède, sinon il vous bénira en face.
Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
12 Alors le Seigneur dit au diable: Tu vois tout ce qui est à lui, je te le livre, mais ne touche pas à sa personne. Et le diable sortit de devant le Seigneur.
Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
13 Or, peu de temps après ce jour-là, les fils de Job et ses filles buvaient du vin en la maison de l'aîné de leurs frères.
Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
14 Et un messager entra chez Job et il lui dit: Tes attelages de bœufs étaient au labour et les ânesses paissaient tout auprès.
akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
15 Et des hommes en armes sont venus et ils les ont enlevés, et ils ont tué tes serviteurs à coups de glaive; j'ai seul échappé et j'accours t'en apporter la nouvelle.
Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
16 Comme celui-ci parlait encore survint un autre messager, et il dit à Job: Le feu du ciel est tombé et il a brûlé tes brebis, et il a dévoré pareillement les bergers; j'ai seul échappé et j'accours t'en apporter la nouvelle.
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
17 Comme celui-ci parlait encore survint un autre messager, et il dit à Job: Des cavaliers nous ont attaqués sur trois points, et ils ont enveloppé tes chamelles, et ils les ont enlevées; et ils ont tué tes serviteurs à coups de glaive; j'ai seul échappé et j'accours t'en apporter la nouvelle.
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
18 Comme celui-ci parlait encore survint un autre messager, et il dit à Job: Tandis que tes fils et tes filles étaient à manger et à boire chez leur frère aîné,
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
19 Soudain un grand vent est venu du désert et il a saisi les quatre coins de la maison; et elle s'est écroulée sur tes enfants; et ils sont morts; j'ai seul échappé et j'accours t'en apporter la nouvelle.
ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
20 Or, Job s'étant levé déchira ses vêtements, et il se coupa toute la chevelure, et, s'est prosternant la face contre terre, il adora, et il dit:
Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
21 Nu je suis sorti des entrailles de ma mère, nu je partirai d'ici; le Seigneur n'avait donné, le Seigneur m'a ôté, il est advenu comme il a plu au Seigneur; béni soit le nom du Seigneur.
na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
22 Malgré tout ce qui lui est arrivé, Job ne pécha point contre le Seigneur; et il n'accusa point Dieu d'avoir manqué de sagesse.
Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.

< Job 1 >