< Jérémie 9 >

1 Qui donnera à ma tête un réservoir d'eau, et à mes yeux une source de larmes? Et je pleurerai mon peuple nuit et jour, et la mort de la fille de mon peuple.
Kama kichwa changu kingetoa maji, na macho yangu kuwa chemichemi ya machozi! kwa kuwa natamani kulia usiku na mchana kwa ajili yao waliokuwa binti za watu wangu ambao wameuawa.
2 Qui me donnera, dans le désert, une cabane lointaine? Et j'abandonnerai mon peuple, et je m'éloignerai de lui; car ce sont tous des adultères, c'est une assemblée de prévaricateurs.
Kama mtu anganipatia mahali pa wasafiri nyikani ili nikae, mahali ambapo ningeenda kuwatelekeza watu wangu. Kama ningewaacha, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la wenye hiana!
3 Et ils ont tendu leur langue comme un arc; le mensonge, et non la bonne foi, a prévalu sur la terre; car ils ont passé de péché en péché, et ils ne m'ont point connu.
asema BWANA, “Huupinda ulimi wao kana kwamba ni upinde ili wapate kuongea uongo, lakini si kwa uamiinifu wao kwamba wanapata nguvu duniani. Wanatoka uovu mmoja hadi mwiingine. Hawanijui mimi.”
4 Gardez-vous chacun de votre prochain, ne vous fiez pas à votre frère: tout frère supplantera son frère; tout ami s'approchera traîtreusement de son ami.
Kila mmoja wenu, awe mlinzi wa jirani yake na usimwamini hata ndugu yako yeyote. kwa kuwa kila ndugu ni mwongo,
5 Chacun se joue de ses amis; on ne dit pas la vérité. Leur langue a appris à dire des mensonges; ils ont commis l'injustice; ils ne font rien pour se convertir.
kila jirani anatembea akilaghai. Kila mwanamume anakejeli jirani yake na haongei ukweli. Ndimi zao hufundisha vitu vya uongo. Hujidhofisha ili kusema uongo.
6 Usure sur usure, fraude sur fraude; ils n'ont point voulu me connaître.
Makazi yenu yako kati ya udanganyifu; kwa uongo wao wanakataa kunitambua mimi. Asema BWANA.”
7 A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Je les ferai passer par le feu, et je les éprouverai, et j'agirai ainsi en voyant la perversité de la fille de mon peuple.
Kwa hiyo BWANA wa majeshi asema hivi, “Tazama, Niko tayari kuwajaribu. Nitawajaribu nione. Jinsi gani niwezavyo kufanya kwa binti za watu wangu?
8 Leur langue est une flèche acérée; les paroles de leur bouche sont trompeuses; au prochain, on parle de paix, et on a la haine au cœur.
Ndimi zao ni mishale iliyochongoka; huongea vitu vya uasi. Kwa midomo yao wanatangaza amani pamoja na jirani zao, lakini katika mioyo yao wanadanganya wakati wa kusubri.
9 Est-ce que je ne les visiterai pas pour ces choses? dit le Seigneur; est- ce que mon âme ne tirera pas vengeance d'un tel peuple?
Kwa nini nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya - asema BWANA na kwa nini nisijilipizie kisasi kwa taifa ambalo liko kama hili?
10 Faites entendre une lamentation sur les montagnes, chantez un cantique funèbre dans les sentiers du désert; car ces lieux sont désolés faute d'hommes. On n'y entend plus la voix d'êtres vivants, depuis les oiseaux du ciel jusqu'aux troupeaux: ils ont été frappés de stupeur, et ils ont fui.
Nitaimba wimbo wa kuomboleza na kulia kwa ajili ya milima, na wimbo wa mazishi utaimbwa nyikani. Kwa kuwa wameteketezwa kwa hiyo hakuna anAyeweza kupita kati kati yao. Hawatasikia sauti ya ng'ombe yeyote. Ndege wa angani na wanyama wote wamekimbia.
11 Et je ferai sortir de Jérusalem ses habitants, et elle sera la demeure des dragons; et je mettrai la désolation dans les villes de Juda au point qu'elles ne seront plus habitées.
Kwa hiyo nitaigeuza Yerusalemu kuwa vifusi vya ukiwa, maficho ya mbweha. Nitaifanya miji ya Yuda kuwa miji iliyoharibiwa isiyokaliwa na watu.
12 Quel homme est assez intelligent pour comprendre ces choses? Et la parole du Seigneur viendra à lui; qu'il vous annonce pourquoi la terre a péri, et a été brûlée comme un désert, au point qu'on n'y peut plus passer.
Ni nani mwenye hekima anayeyaelewa haya? Je, kinywa cha BWANA kinatangaza nini kwake ili aweze kuyasema? Kwa nini nchi imepotea? Imeharibiwa kama jangwa, ambapo hakuna apitaye kati kati yake.
13 Et le Seigneur me dit: C'est parce qu'ils ont abandonné la loi que je leur ai donnée face à face, et n'ont pas écouté ma voix.
BWANA asema, “Ni kwa sababu wameziacha sheria zake ambazo niliwatengenezea, kwa sababu hawaisikilizi sauti yangu au kuishi kwa kuifuta.
14 Mais ils ont couru après les convoitises de leur cœur pervers, et après des idoles que leurs pères leur avaient appris à adorer.
Ni kwa sababu wameishi kwa ushupavu wa mioyo yao na wamewafuata Mabaali kama baba zao walivyowafundisha kufanya.
15 A cause de cela, dit le Seigneur Dieu d'Israël, voilà que je vais les nourrir d'angoisses et les abreuver d'eau mêlée de fiel.
Kwa hiyo BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Tazama, Ninataka kuwafanya hawa watu wale pakanga na kunywa maji ya sumu.
16 Et je les disperserai parmi les nations, chez des hommes que ni eux ni leurs pères n'ont connus; et je ferai tomber sur eux le glaive, jusqu'à ce que le glaive les ait détruits.
Ndipo nitakapowasambaza kati ya mataifa ambayo hawajayajua, wao wala mababu zao. Nitatuma upanga kwa ajili yao mpaka nimewaangamiza wote kabisa.'”
17 Voici ce que dit le Seigneur: Appelez des pleureuses, et qu'elles viennent; envoyez chercher les plus habiles à pleurer, et qu'elles élèvent la voix.
BWANA wa majeshi asema hivi, “Yafikirini haya: Waiteni waliaji; waje. Tumeni wanawake wenye taaluma ya kuomboleza, waje.
18 Et qu'elles chantent une lamentation sur vous, et que des larmes tombent de vos yeux, et que vos paupières soient inondées de pleurs.
Waje haraka waimbe wimbo wa maombolezo juu yetu, ili macho yetu yatokwe na machozi na kope zetu zibubujikwe na maji.
19 Car leur voix lamentable a été entendue en Sion: Comment sommes-nous réduits à cet état de misère, tellement confondus que nous avons abandonné notre terre et renversé nos tabernacles?
Kwa kuwa sauti ya kilio imesikika Sayuni, 'Jinsi tulivyoharibiwa. Tumeaibishwa sana, kwa kuwa tumeitelekeza nchi tangu walIpoangusha nyumba zetu.'
20 Femmes, écoutez la parole de Dieu, et que vos oreilles recueillent les paroles de sa bouche: Apprenez à vos filles des lamentations, apprenez-vous les unes aux autres des cantiques funèbres:
Kwa hiyo ninyi wanawake, sikieni neno la BWANA; zingatieni ujumbe unaokuja toka kinywani mwake. Kisha wafundisheni binti zenu wimbo wa maombolezo, na kila mwanamke wa jirani wimbo wa kilio.
21 Parce que la mort est montée par vos fenêtres, et qu'elle est entrée dans vôtre terre pour exterminer au dehors les enfants à la mamelle, et dans les rues les adolescents.
Kwa kuwa vifo vimekuja kupitia dirishani; vinaelekea mahali petu. Vinawaharibu watoto kutoka nje na vijana kwenye viwanja vya miji.
22 Et les cadavres des hommes resteront en exemple sur la surface de votre terre, comme le chaume reste derrière le moissonneur; et nul ne sera là pour les recueillir.
Uyatangaze haya, 'Asema BWANA - mizoga ya wanaume itaanguka kama mavi kwenye mashamba na kama mabua baada ya mvunaji, na hapatakuwa na mtu wa kuyakusanya.'”
23 Voici ce que dit le Seigneur: Que le sage ne se glorifie pas dans sa sagesse; que le fort ne se glorifie pas dans sa force; que le riche ne se glorifie pas dans sa richesse.
BWANA asema hivi, “Usimwache mtu mwenye busara ajivune kwa ajili ya hekima yake, au shujaa kwa sababu ya uwezo wake. Usimwache mtu tajiri ajivunie utajiri wake.
24 Mais que celui qui se glorifie se glorifie de comprendre et de savoir que c'est moi le Seigneur, moi qui fais sur la terre miséricorde, jugement et justice; car c'est en cela que je me complais, dit le Seigneur.
Kwa kuwa kama mtu atajivunia chochote kile, acha iwe hivi, yeye awe na busra na kunijua mimi. Kwa kuwa mimi ni BWANA, atendaye katika agano la wema, haki, na hukumu duniani. Ni katika hili kwamba ninafurahia- asema BWANA.
25 Voilà que les jours viennent, dit le Seigneur, où je visiterai tous les circoncis en leur chair,
Tazama, siku zaja - asema BWANA wakati nitakapowaadhibu wote ambao hawajatahiriwa ambao wako hivyo hivyo katika miili yao.
26 Et l'Égypte, et l'Idumée, et Édom, et les fils d'Ammon, et les fils de Moab et tous ceux qui se coupent la chevelure au-dessus du front, et qui habitent le désert; car tous ces peuples sont incirconcis en leur chair, et toute la maison d'Israël incirconcise en son cœur.
Nitaiadhibu Misri na Yuda, Edomu, watu wa Amoni, Moabu, na watu wote wanaonyoa denge. Kwani mataifa yote haya hayajatahiriwa, na nyumba yote ya Israeli ina moyo ambao haujatahiriwa.”

< Jérémie 9 >