< Jérémie 7 >

1 Écoutez tous la parole du Seigneur, peuples de la Judée;
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 Écoutez tous la parole du Seigneur, peuples de la Judée;
“Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
3 Voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël Redressez vos voies et vos pensées, et j'habiterai avec vous en ce lieu.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
4 Ne mettez pas votre confiance en vous-mêmes, ni en des paroles de mensonge; car il ne vous servira nullement de dire: Le temple du Seigneur, le temple du Seigneur est ici.
Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
5 Car si vous redressez vos voies et vos actions, si vous rendez la justice entre un homme et son prochain;
Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
6 Si vous n'opprimez pas l'étranger, ni l'orphelin, ni la veuve; si vous ne versez pas le sang innocent dans ce lieu; si vous ne courez pas, pour votre malheur, après des dieux étrangers,
kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
7 J'habiterai ce lieu avec vous, en la terre que j'ai donnée, de siècle en siècle, à vos pères.
ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
8 Mais si vous mettez votre confiance en des paroles de mensonge, dont vous ne retirerez aucun secours;
Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
9 Si vous tuez, si vous commettez des adultères, si vous volez, si vous jurez faussement, si vous brûlez de l'encens à Baal, et si vous courez, pour votre malheur, après des dieux étrangers qui vous étaient inconnus;
“‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
10 Et après cela, si vous venez, si vous vous placez devant moi en cette maison où mon nom a été invoqué, disant: Nous nous sommes abstenus de commettre ces abominations,
kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
11 Moi je vous dirai: Est-ce une caverne de voleurs, ma maison où mon nom a été invoqué devant vous? Je vous ai vus, dit le Seigneur.
Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
12 Allez en ce lieu qui m'appartient, à Silo, où d'abord j'avais abrité mon nom; et voyez comment je l'ai traité, à la vue de la méchanceté de mon peuple Israël.
“‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
13 Et maintenant parce que vous avez fait toutes ces œuvres, parce que je vous ai parlé, et que vous ne m'avez pas écouté; parce que je vous ai appelés et que vous ne m'avez pas répondu,
Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
14 Je traiterai cette maison où mon nom a été invoqué, et en qui vous mettiez votre confiance, je traiterai cette terre que j'ai donnée à vos pères et à vous, comme j'ai traité Silo.
Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
15 Et je vous rejetterai loin de ma face, comme j'ai rejeté vos frères, toute la race d'Éphraïm.
Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
16 Et toi, garde-toi de prier pour ce peuple; ne demande pas que je lui fasse miséricorde; ne prie pas et ne viens pas à moi pour eux, car je ne t'exaucerai point.
“Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
17 Ne vois-tu pas ce qu'ils font dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem?
Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
18 Leurs fils amassent le bois, et les pères allument le feu, et leurs femmes pétrissent la pâte pour offrir des gâteaux à la reine du ciel, et ils répandent des libations pour des dieux étrangers, afin de provoquer ma colère.
Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
19 Est-ce moi qu'ils provoquent ainsi? dit le Seigneur. N'est-ce pas eux- mêmes, pour que leur front soit couvert de honte?
Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
20 Et c'est pourquoi le Seigneur a dit: Voilà que ma vengeance et ma colère vont fondre sur ce lieu et sur les hommes, et sur le bétail, et sur tous les arbres de leurs champs, et sur les fruits de la terre; ma colère brûlera et ne s'éteindra point.
“‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
21 Voici ce que dit le Seigneur: Multipliez vos holocaustes et vos victimes, et mangez-en les chairs:
“‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
22 Parce que je n'ai point parlé à vos pères, et que je ne leur ai rien prescrit, le jour où je les ai ramenés de la terre d'Égypte, concernant les holocaustes et les sacrifices:
Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
23 Mais je leur ai donné ce commandement: Écoutez ma parole, et je serai votre Dieu, et vous serez mon peuple; marchez dans toutes mes voies comme je vous l'ordonne, et vous serez bénis.
lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
24 Et ils ne m'ont point écouté, et ils ne m'ont point prêté l'oreille; mais ils ont couru après tous les désirs de leurs cœurs pervers, et ils ont reculé au lieu d'avancer,
Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
25 Depuis le jour où leurs pères sont sortis de l'Égypte jusqu'à ce jour. Et je vous ai envoyé mes serviteurs les prophètes de jour en jour dès l'aurore; je les leur ai envoyés,
Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
26 Et ils ne m'ont point écouté, et ils ne m'ont point prêté l'oreille, et ils ont endurci leur tête plus que leurs pères.
Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
27 Or tu leur diras cette parole:
“Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
28 Voici la nation qui n'a point écouté la voix du Seigneur, et n'a point profité des corrections; la foi est bannie de leur bouche.
Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
29 Coupe tes cheveux, et jette-les loin de toi; et mets une lamentation sur tes lèvres; car le Seigneur a réprouvé, il a répudié la race qui a fait ces choses.
Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
30 Car les enfants de Juda ont fait le mal devant moi, dit le Seigneur; ils ont introduit leurs abominations dans la maison où était invoqué mon nom, afin de le profaner.
“‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
31 Et ils ont bâti l'autel de Tapheth dans la vallée des fils d'Ennom pour y brûler par le feu leurs fils et leurs filles, sacrifice que je ne leur ai point prescrit et auquel je n'ai jamais songé en mon cœur.
Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
32 A cause de cela, voilà que les jours arrivent, dit le Seigneur, et on ne dira plus: L'autel de Tapheth, la vallée des fils d'Ennom; mais, la vallée des égorgés; et on inhumera les morts en Tapheth, parce qu'on n'aura point d'autre place.
Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
33 Et les morts de ce peuple seront la proie des oiseaux du ciel et des bêtes fauves des champs; et nul ne sera là pour les chasser.
Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
34 Et dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem je ferai taire la voix de la joie et de l'allégresse, la voix du fiancé et de la fiancée; car toute la terre sera devenue une solitude.
Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.

< Jérémie 7 >