< Jérémie 24 >

1 Le Seigneur me montra deux corbeilles de figues posées devant la façade du temple du Seigneur, après que Nabuchodonosor eut enlevé Jéchonias, fils de Joakim, roi de Juda, et les princes, et les artisans, et les prisonniers, et les riches de Jérusalem, et qu'il les eut emmenés à Babylone.
Baada ya Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda, kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli, Bwana akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu la Bwana.
2 L'une de ces corbeilles contenait de très bonnes figues, comme celles de la primeur; et l'autre de très mauvaises figues qu'on ne pouvait manger, tant elles étaient mauvaises.
Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza. Kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbovu mno zisizofaa kuliwa.
3 Et le Seigneur me dit: Jérémie, que vois-tu? Et je répondis: Des figues; des figues bonnes, très bonnes, et d'autres mauvaises, très mauvaises, qu'on ne peut manger, tant elles sont mauvaises.
Kisha Bwana akaniuliza, “Je, Yeremia, unaona nini?” Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu ni mbovu mno zisizofaa kuliwa.”
4 Et la parole du Seigneur vint à moi, disant:
Kisha neno la Bwana likanijia:
5 Voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël: Comme les bonnes figues, je reconnaîtrai les Juifs emmenés en captivité, que j'ai expulsés de ce lieu et envoyés en Chaldée, je les traiterai bien.
“Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo.
6 Et j'attacherai sur eux mes regards pour leur bien, et je les rétablirai pour leur bien dans cette terre, et je les réédifierai pour ne plus les abattre, et je les replanterai pour ne plus les arracher.
Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa,
7 Et je leur donnerai un cœur pour qu'ils me connaissent, pour qu'ils sachent que je suis le Seigneur; et ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu, parce qu'ils se seront convertis à moi de toute leur âme.
nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.
8 Et comme les mauvaises figues qu'on ne peut manger, tant elles sont mauvaises, dit le Seigneur, je livrerai Sédécias, roi de Juda, et ses grands, et le reste de Jérusalem qui est demeuré en cette terre, et ceux qui habitent l'Égypte.
“‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbovu mno zisizofaa kuliwa,’ asema Bwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, wawe wamebaki katika nchi hii, au wanaishi Misri.
9 Et je les livrerai à la dispersion dans tous les royaumes de la terre, et dans les lieux où je les aurai bannis, et ils seront un sujet d'outrages et de railleries, de haine et de malédiction;
Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, popote nitakapowafukuzia.
10 Et je leur enverrai la famine, et la peste, et le glaive, jusqu'à ce qu'il n'y en n'ait plus sur cette terre que je leur ai donnée.
Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao hadi wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’”

< Jérémie 24 >