< Jérémie 12 >
1 Seigneur, vous êtes juste; aussi je me défendrai devant vous; je vous demanderai justice. Pourquoi la voie des impies est-elle prospère? pourquoi ceux qui vous ont répudié sont-ils florissants?
Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
2 Vous les avez plantés, et ils ont pris racine; ils ont engendré, et ils ont produit des fruits. Vous êtes près de leur bouche, et loin de leurs reins.
Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
3 Et vous, Seigneur, vous me connaissez, vous avez devant vous éprouvé mon cœur; purifiez-les pour le jour de leur égorgement.
Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
4 Jusques à quand la terre sera-t-elle en deuil avec des pâturages et des champs desséchés par la malice de ceux qui l'habitent? Les oiseaux et le bétail ont été détruits, parce que les hommes ont dit: Dieu ne verra point. nos voies.
Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
5 Tes pieds courent, et te voilà énervé; comment feras-tu donc pour combattre des cavaliers et te confier dans une terre de paix? Que feras-tu contre les débordements du Jourdain?
“Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
6 Tes frères eux-mêmes et la maison de ton père t'ont méprisé; ils ont eux- mêmes crié contre toi, ils se sont donc unis à ceux qui te poursuivaient par derrière; ne te fie pas à eux, quoiqu'ils te disent de belles paroles.
Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
7 J'ai abandonné ma maison; j'ai renoncé à mon héritage; j'ai livré aux mains de ses ennemis celle qui était ma bien-aimée et ma vie.
“Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
8 Mon héritage est devenu contre moi comme le lion dans une forêt; il a rugi contre moi; à cause de cela je l'ai pris en haine.
Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
9 Mon héritage est-il pour moi un antre d'hyène ou l'enceinte d'une caverne? Allez, rassemblez toutes les bêtes fauves de la terre, et qu'elles viennent dévorer mon héritage.
Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
10 Maints pasteurs ont ravagé ma vigne; ils ont souillé mon partage; ils ont fait de ma part bien-aimée un désert sans chemin.
Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
11 Elle a été livrée au ravage et à la dévastation. Toute la terre a été frappée de ruine à cause de moi, parce que nul homme n'a souci de moi en son cœur.
Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
12 Ceux qui la dévastaient sont venus par toutes les voies du désert, parce que le glaive du Seigneur va dévorer la terre d'une extrémité à l'autre; il n'est plus de paix pour aucune chair.
Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
13 Semez des froments, et vous récolterez des chardons; leur part d'héritage ne leur rapportera rien; soyez confondus à cause de votre orgueil et de vos outrages à la face du Seigneur.
Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
14 Car ainsi parle le Seigneur contre tous les méchants voisins qui touchent à mon héritage, que j'ai distribué à mon peuple d'Israël: Voilà que je vais les arracher de leur terre, et je rejetterai Juda du milieu d'eux.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
15 Et voici ce qui arrivera: après les avoir bannis, je changerai, et j'aurai pitié d'eux, et je les ferai rentrer dans leurs demeures, chacun dans son héritage et chacun dans son champ.
Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
16 Et ceci arrivera encore: s'ils s'instruisent, s'ils apprennent la voie de mon peuple, et à jurer en mon nom: Vive le Seigneur! comme ils avaient enseigné mon peuple à jurer par le nom de Baal, ils seront édifiés au milieu de mon peuple.
Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
17 Et s'il est une de ces nations qui ne se convertisse pas, je la détruirai, et elle sera perdue à jamais.
Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.