< Isaïe 66 >

1 Voici ce que dit le Seigneur: Le ciel est mon trône, et la terre l'escabeau de mes pieds. Quelle maison me bâtirez-vous? Et quel sera le lieu où je résiderai?
Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
2 Car ma main a tout fait, et tout est à moi, dit le Seigneur. Et sur qui jetterai-je mes regards, sinon sur l'humble et le doux, sur l'homme qui tremble à ma parole?
Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
3 L'injuste me sacrifie un bœuf, c'est comme s'il tuait un chien; un autre m'offre de la fleur de farine, c'est pour moi comme du sang de pourceau; un autre brûle de l'encens pour mémorial, c'est comme s'il blasphémait; ils ont choisi leurs voies, leur âme s'est complu en leurs abominations.
Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
4 Et moi, je leur ferai payer leurs moqueries, et je punirai leurs péchés; car je les ai appelés, et ils ne m'ont pas obéi; j'ai parlé, et ils n'ont pas entendu; et devant moi ils ont fait le mal, et ce que je ne voulais pas, ils l'ont voulu.
Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
5 Écoutez ce que dit le Seigneur, vous qui tremblez à sa parole; vous avez dit: Nos frères, à ceux que vous avez en haine et en abomination; que le nom du Seigneur soit glorifié en eux, et se manifeste en leur joie; mais ils seront confondus.
Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
6 On entendra la voix de la ville, la voix du temple, la voix du Seigneur qui punira ses ennemis.
Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
7 Avant d'avoir été en mal d'enfant, avant que le moment des douleurs fût arrivé, elle a été délivrée, et elle a donné le jour à un fils.
“Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
8 Qui a jamais ouï pareille chose? qui a vu rien de semblable? La terre n'a-t-elle été en travail d'enfant qu'un seul jour? une nation est-elle née tout d'une fois, pour que Sion ait été en travail et ait mis au jour ses enfants?
Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
9 Mais c'est moi qui ai fait naître cette attente, et tu ne t'es point souvenue de moi, dit le Seigneur. N'est-ce point moi qui rends une femme féconde ou stérile? dit ton Dieu.
Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
10 Jérusalem, réjouis-toi; rassemblez-vous dans ses murs, vous tous qui l'aimez; réjouissez-vous de sa joie, vous qui vous êtes affligés sur elle:
“Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
11 Afin que vous vous allaitiez et que vous puisiez la plénitude à la mamelle de sa consolation; afin qu'après vous être allaités, vous trouviez des délices dans le retour de sa gloire.
Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
12 Car ainsi dit le Seigneur: Voilà que je détourne vers eux comme une flamme de paix, comme un torrent qui leur apportera dans ses flots la gloire des Gentils. Les enfants de mon peuple seront portés à bras; on les prendra sur les genoux pour les consoler.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
13 Telle une mère console son enfant, et je vous consolerai, et c'est en Jérusalem que vous serez consolés.
Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
14 Et vous le verrez, et votre cœur sera réjoui, et vos os fleuriront comme l'herbe. Et la main du Seigneur sera connue de ceux qui le craignent, et elle menacera les rebelles.
Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
15 Car voilà que le Seigneur viendra comme une flamme; les roues de son char seront comme un vent impétueux, apportant sa colère, sa vengeance et sa menace, dans une flamme de feu.
Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
16 Car toute la terre sera jugée par le feu du Seigneur, et toute chair par son glaive; une multitude d'hommes seront blessés par le Seigneur.
Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
17 Ceux qui se sanctifient et se purifient dans les jardins, qui mangent sous leurs portiques de la chair de porc, des souris, et d'autres mets abominables, seront tous ensemble consumés par le Seigneur.
“Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
18 Et moi qui connais leurs œuvres et leurs pensées, je vais réunir tous les peuples et toutes les langues, et ils viendront, et ils verront ma gloire.
“Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
19 Et je laisserai sur eux un signe, et j'enverrai ceux d'entre eux qui auront été sauvés chez les Gentils à Tharsis, à Phud, à Lud, à Mosoch, à Thobel, en Grèce, et aux îles lointaines, où mon nom n'a jamais été prononcé, où l'on n'a point vu ma gloire; et ils publieront ma gloire parmi les nations.
“Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
20 Et ils amèneront vos frères de toutes les nations pour en faire offrande au Seigneur, avec des chevaux et des litières freinées par des mules empanachées, dans la ville sainte, dit le Seigneur; comme lorsque les fils d'Israël offraient leurs sacrifices, en chantant des psaumes, dans le temple du Seigneur.
Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
21 Et je choisirai parmi eux des prêtres et des lévites, dit le Seigneur.
Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
22 Car de même que le ciel nouveau et la terre nouvelle que je créerai subsisteront devant moi, dit le Seigneur, de même votre race et votre nom seront fermement établis.
“Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
23 Et ceci sera de lune en lune, de sabbat en sabbat: toute chair viendra en Jérusalem pour adorer devant moi, dit le Seigneur.
Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
24 Et ils sortiront, et ils verront les membres épars de ceux qui auront péché contre moi; car le ver qui les rongera ne finira point; le feu qui les brûlera ne sera jamais éteint, et ils seront exposés à la vue de toute chair.
“Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”

< Isaïe 66 >