< Isaïe 48 >

1 Écoutez, maison de Jacob, vous qui portez le nom d'Israël, qui sortez de Juda et qui jurez au nom du Seigneur Dieu d'Israël, qui faites mention de tout cela, mais non dans la vérité et la justice;
“Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
2 Qui gardez le nom de la ville sainte, et qui vous appuyez sur le Dieu d'Israël; le Seigneur des armées est son nom.
ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
3 Je vous ai déjà fait connaître les choses des premiers temps: elles sont sorties de ma bouche, et tout s'est fait comme vous l'aviez entendu; j'ai agi soudain, et les faits sont advenus.
Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
4 Je sais que tu es dur; ton cou est un nerf de fer, et tu as un front d'airain.
Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
5 Aussi t'ai-je prédit les choses longtemps avant qu'elles te fussent arrivées, et je te les ai fait connaître afin que tu ne puisses dire: Ce sont mes idoles qui m'ont fait ceci; et que tu ne puisses dire: Ce sont mes sculptures ou mes statues en fonte qui m'ont ordonné cela.
Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
6 Tout ce que vous avez entendu autrefois, vous ne le connaissiez pas; mais je vais vous faire connaître des choses nouvelles, des choses présentes, et qui sont sur le point d'arriver. Et vous n'avez point dit:
Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
7 Maintenant tout s'accomplit; quant à ceci, ce n'est pas une prédiction d'autrefois, et tu n'en as pas entendu parler les jours précédents; ne dis donc pas: Assurément je connais ces choses.
Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
8 Tu ne les connais pas, tu n'en as rien su; je ne t'ai point ouvert les oreilles dès le commencement; car je savais qu'étant traître tu trahirais, et que dès le sein de ta mère tu serais appelé violateur de ma loi.
Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
9 Mais à cause de mon nom je te montrerai ma colère; puis j'accomplirai devant toi mes merveilles afin que je ne t'extermine pas.
Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
10 Voilà que je t'ai vendu, non à prix d'argent; mais je t'ai retiré d'une fournaise de misère.
Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
11 A cause de moi, j'agirai ainsi pour toi; car mon nom a été profané, et je ne donnerai pas ma gloire à un autre.
Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
12 Ecoute-moi donc, Jacob; écoute-moi, Israël, que j'appelle à moi: Je suis le premier, et je suis pour l'éternité.
“Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
13 Et ma main a fondé la terre, et ma droite a affermi le ciel. Je les appellerai, et ils se présenteront à la fois;
Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
14 Et ils se rassembleront tous, et ils m'écouteront. Qui a fait connaître ces choses à tes idoles? Par amour pour toi, j'ai fait contre Babylone ce que tu désirais, afin d'exterminer la race des Chaldéens.
“Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
15 J'ai parlé, j'ai appelé, je l'ai conduit et je lui ai préparé la voie.
Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
16 Approchez-vous de moi, écoutez ce que je vais vous dire: Dès le commencement je n'ai point parlé en secret; quand les choses ont été résolues, j'étais là, et maintenant le Seigneur Maître m'a envoyé, et avec lui son Esprit.
“Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
17 Voici ce que dit le Seigneur, qui t'a délivré, le Saint d'Israël: Je suis ton Dieu, je t'ai montré comment tu trouverais la voie où tu dois marcher.
Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
18 Et si tu avais été docile à mes commandements, ta paix aurait été comme un fleuve, et la justice comme les vagues de la mer.
Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
19 Et ta race aurait été comme le sable, et les fruits de tes entrailles comme la poussière des champs; et maintenant tu ne seras pas entièrement détruit, et ton nom ne périra pas devant moi.
Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
20 Sortez de Babylone, fuyez loin des Chaldéens; poussez un cri d'allégresse; écoutez ces paroles, publiez-les jusqu'aux extrémités de la terre, et dites: Le Seigneur a délivré son serviteur Jacob.
Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
21 Et s'ils ont soif, il les guidera à travers le désert; il fera jaillir pour eux l'eau des rochers; la pierre s'ouvrira, des eaux en couleront, et mon peuple boira.
Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
22 Mais pour les impies, il n'y a point de joie, dit le Seigneur.
“Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.

< Isaïe 48 >