< Isaïe 43 >
1 Et maintenant voici ce que dit le Seigneur: Qui t'a créé, Jacob? qui t'a formé, Israël? Ne crains pas, car je t'ai racheté; je t'ai donné ton nom, tu es à moi.
Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
2 Si tu traverses les eaux, je suis avec toi; et les fleuves ne pourront te submerger; et si tu passes à travers la flamme, tu ne seras point brûlé, le feu ne te brûlera pas.
Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
3 Car je suis le Seigneur ton Dieu, le Saint d'Israël, ton sauveur. J'ai fait de l'Égypte et de l'Éthiopie ta rançon, et pour toi j'ai livré Soène.
Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
4 Depuis que tu es devenu précieux devant moi, tu as été glorifié, et je t'aime, et je donnerai pour toi les hommes, et pour ta tête les princes.
Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
5 Ne crains pas, car je suis avec toi. De l'Orient je ramènerai ta race; je te ferai revenir de l'Occident.
Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
6 Je dirai à l'aquilon: Ramène-les; et au midi: Ne retiens pas, ramène de loin mes fils, ramène mes filles des extrémités de la terre.
Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
7 Ramène tous ceux qui ont invoqué mon nom; car j'ai préparé ce peuple, je l'ai formé, je l'ai fait pour ma gloire;
kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
8 Et j'ai éloigné de moi un peuple aveugle, et ses yeux étaient comme aveuglés, et ses oreilles étaient sourdes.
Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
9 Voilà tous les Gentils rassemblés à la fois, voilà leurs princes. Qui d'entre eux annoncera ces choses? Qui annoncera les choses à partir du commencement? Qu'ils produisent leurs témoins, qu'ils se justifient, qu'ils écoutent et disent la vérité.
Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
10 Soyez pour moi des témoins, et moi-même je porterai témoignage, dit le Seigneur Dieu; et aussi mon serviteur, celui que j'ai élu, afin que vous sachiez, que vous croyiez et compreniez que je suis. Avant moi il n'y a pas eu d'autre Dieu, et il n'en sera point après moi.
“Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
11 Je suis Dieu, et, hormis moi, nul ne sauve.
Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
12 J'ai prédit, j'ai sauvé, j'ai fait des reproches, et il n'y avait pas avec vous d'étranger. Vous êtes mes témoins, et moi je suis le Seigneur Dieu.
Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
13 Je suis depuis le commencement, et il n'est personne qui puisse rien arracher de mes mains. Je ferai mon œuvre, et qui la détruira?
Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
14 Voici ce que dit le Seigneur Dieu qui vous a racheté, le Saint d'Israël: A cause de vous, j'enverrai un ennemi contre Babylone, et je les ferai tous fuir, et les Chaldéens seront enchaînés dans des vaisseaux.
Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
15 Je suis le Seigneur Dieu, votre Saint, qui ai institué votre roi en Israël.
Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
16 Voici ce que dit le Seigneur, qui traça une voie dans la mer, et des sentiers sur les grandes eaux;
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
17 Qui y fit entrer des chars, des chevaux et une puissante multitude. Mais ils se sont endormis et ils ne se réveilleront plus; ils se sont éteints comme une mèche qu'on a éteinte.
aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
18 Mais vous ne vous souvenez pas des choses du commencement; vous ne considérez point ce qui s'est fait autrefois.
“Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19 Eh bien, je ferai de nouveaux prodiges, qui vont naître tout à l'heure, et vous les connaîtrez; je tracerai une voie dans le désert, et je ferai jaillir des fleuves sur une terre sans eau.
Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
20 Les bêtes des champs me béniront avec les petits oiseaux et les jeunes passereaux, parce que j'aurai donné de l'eau à une terre aride, et des fleuves au désert, pour abreuver ma race élue,
Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
21 Mon peuple dont j'ai pris soin, pour qu'il raconte mes vertus.
watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
22 Et pourtant je ne t'ai pas appelé, Jacob; je ne t'ai point coûté de fatigues, Israël!
“Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
23 Tu ne m'as point offert d'holocauste de tes brebis; tu ne m'as point glorifié par tes sacrifices; je ne t'ai point assujetti à m'immoler des victimes; je ne t'ai pas donné la peine de brûler pour moi de l'encens.
Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
24 Tu n'as pas acheté pour moi des victimes à prix d'argent; je n'ai point désiré la génisse de tes sacrifices, mais tu t'es présenté devant moi avec tes péchés et ton injustice.
Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
25 C'est moi cependant, c'est moi qui efface tes transgressions et tes péchés, à cause de moi-même, et je n'en garderai pas le souvenir.
“Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
26 De ton côté souviens-toi, et plaidons ensemble; confesse d'abord tes iniquités, afin que tu sois justifié.
Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
27 Vos pères les premiers, et vos princes ont péché contre moi.
Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
28 Et vos princes ont profané mes choses saintes, et j'ai livré Jacob et Israël à l'opprobre et à la destruction.
Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.