< Isaïe 41 >

1 Faites-moi fête; car les princes ont recouvré leurs forces: qu'ils approchent, qu'ils parlent tous à la fois, et qu'alors ils proclament le jugement.
“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
2 Qui donc a suscité de l'Orient la justice? Il lui a dit: Viens à mes pieds; et elle y viendra. Il la fera comparaître devant les nations; il frappera les rois de stupeur. Il fera tomber à terre leurs glaives; il repoussera comme des broussailles leurs arcs et leurs flèches.
“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
3 Et il les poursuivra; et il parcourra en paix la voie de ses pieds.
Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
4 Qui a opéré, qui a fait ces choses? C'est celui qui a appelé la justice, qui l'a appelée dès le commencement des générations. Je suis Dieu, le premier, et pour tous les siècles à venir je suis.
Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
5 Les nations ont vu, et elles ont eu crainte, et elles sont accourues des extrémités de la terre; et elles sont venues toutes à la fois.
Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
6 Chaque homme, jugeant pour son prochain, et pour secourir son frère, dira:
kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
7 L'artisan a réuni tous ses efforts, ainsi que l'ouvrier qui forge au marteau; et il dira: Voilà une pièce bien jointe; on en a ajusté les parties avec des clous, on va les fixer, et elles ne seront pas ébranlées.
Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
8 Et toi, Israël, toi, Jacob, mon serviteur, toi que j'ai choisi, postérité d'Abraham, mon bien-aimé;
“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
9 Toi que j'ai fait revenir des extrémités de la terre; je t'ai convoqué du haut de toutes ses collines, et je t'ai dit: Tu es mon serviteur; je t'ai élu, et je ne t'ai pas abandonné.
nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
10 Ne crains pas, car je suis avec toi; ne t'égare pas, car je suis ton Dieu; c'est moi qui t'ai fortifié, moi qui t'ai secouru, et t'ai affermi par la justice de ma droite.
Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
11 Voilà que tous tes adversaires vont être humiliés et confondus; car ils seront comme s'ils n'étaient pas, et tous tes ennemis périront.
“Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
12 Tu les chercheras et tu ne trouveras plus ces hommes qui t'insultaient dans l'ivresse; car ils seront comme s'ils n'étaient pas, et ceux qui te faisaient la guerre n'existeront plus.
Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
13 Je suis ton Dieu qui t'ai pris par la main droite et qui te dis: Ne crains pas.
Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
14 Jacob, Israël, si amoindri que tu sois, c'est moi qui t'ai secouru, dit ton Dieu; c'est moi, ô Israël, qui t'ai racheté.
Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
15 Voilà que je t'ai façonné comme les roues d'un char à moudre, neuves et dentelées; et tu moudras les montagnes, et tu aplaniras les collines, et tu les réduiras en poudre.
“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
16 Et tu les vanneras, et le vent les emportera, et un tourbillon les dispersera. Cependant tu te réjouiras dans les saints d'Israël.
Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
17 Et les pauvres et les indigents tressailliront d'allégresse; car ils auront cherché de l'eau, et il n'y en avait pas; et leur langue était desséchée par la soif. Mais moi, le Seigneur Dieu, moi le Dieu d'Israël, je les entendrai et je ne les abandonnerai pas.
“Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
18 Je ferai jaillir des fleuves sur les monts, et des sources dans la plaine; je changerai le désert en étangs, et la terre altérée en eaux courantes.
Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
19 Dans la terre sans eau je placerai le cèdre, le buis, le myrte, le cyprès et le peuplier:
Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
20 Afin que partout on voie, on sache, on comprenne, on sente à la fois que la main du Seigneur a fait ces choses, et que le Saint d'Israël les a montrées.
ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
21 Votre jugement est proche, dit le Seigneur Dieu, et proches sont vos conseils, dit le Roi de Jacob.
Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
22 Qu'ils approchent, qu'ils vous annoncent ce qui doit arriver, ou ce qui d'abord a existé; parlez, et nous appliquerons notre pensée à votre parole, et nous saurons ce que sont les choses de la fin, les choses à venir.
“Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
23 Dites-nous, annoncez-nous les choses de la fin, et nous reconnaîtrons que vous êtes des dieux. Faites le bien, faites le mal, et nous admirerons, et en même temps nous verrons
tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
24 D'où vous venez et d'où viennent vos œuvres: on vous a tirés de l'abomination de la terre.
Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
25 Mais moi j'ai suscité celui qui vient de l'Aquilon et celui qui vient de l'Orient; ils seront appelés en mon nom. Que viennent les princes, et vous serez foulés aux pieds, comme l'argile du potier; ils vous fouleront comme le potier foule l'argile.
“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
26 Qui donc, en effet, publiera les choses du commencement, afin que nous sachions ce qui précédemment a existé? Alors nous dirons: Cela est véritable. Mais il n'est personne qui prédise, ni qui écoute vos discours.
Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
27 Je donnerai la principauté à Sion, et dans la voie je consolerai Jérusalem.
Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
28 Car nul des Gentils, nulle des idoles ne peut rien apprendre; et si je leur demande: D'où venez-vous? nul ne pourra répondre.
Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
29 Ce sont ceux qui vous fabriquent qui induisent les hommes en erreur.
Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.

< Isaïe 41 >