< Isaïe 36 >
1 Et la quatorzième année du règne d'Ézéchias, Sennachérib, roi des Assyriens, vint assiéger les villes de la Judée; et il s'en rendit maître.
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
2 Et le roi des Assyriens envoya de Lachis, au roi Ézéchias, Rabsacès avec une armée nombreuse; celui-ci s'arrêta vers l'aqueduc de la piscine d'en haut, sur le chemin du champ du Foulon.
Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
3 Et Éliacim, fils d'Helcias l'économe, et Somna le scribe, et Joach fils d'Asaph l'archiviste, sortirent, et vinrent le trouver.
Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
4 Et Rabsacès leur dit: Dites à Ézéchias: Voici ce que dit le grand roi des Assyriens: D'où te vient ta confiance?
Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
5 Livre-t-on bataille avec le conseil ou les paroles des lèvres? Maintenant donc, en qui t'es-tu confié, pour te révolter contre moi?
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
6 Voilà que tu te fies à ce roseau brisé qu'on appelle l'Égypte; il entrera dans la main de quiconque s'appuiera sur lui, et il la percera; ainsi en est- il du Pharaon d'Égypte et de tous ceux qui ont confiance en lui.
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
7 Et si vous dites Nous nous confions dans le Seigneur notre Dieu;
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
8 Eh bien, combattez aujourd'hui mon maître, le roi des Assyriens, et je vous donnerai deux mille chevaux, si vous pouvez leur donner deux mille hommes pour les monter.
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
9 Et comment pourrez-vous seulement résister en face à l'un de nos chefs? Il n'y a que des esclaves qui ont mis leur confiance dans les Égyptiens, dans leurs chevaux et leurs cavaliers.
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
10 Mais est-ce que nous sommes venus combattre cette terre sans le Seigneur? Le Seigneur m'a dit: Marche sur cette terre, et détruis-la.
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
11 Et Éliacim et Somna, et Joach lui dirent: Parle syrien à tes serviteurs, car nous le comprenons; mais ne nous parle pas en langue judaïque. Pourquoi parles-tu? pour être ouï du peuple qui se tient sur les remparts?
Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
12 Mais Rabsacès leur répondit: Est-ce que mon maître ne m'a envoyé dire ces paroles qu'à votre maître et à vous? Ne sont-elles pas pour les hommes qui se tiennent sur le rempart, et qui seront réduits, comme vous, à manger leurs excréments et à boire leur urine?
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
13 Et Rabsacès se redressa, il éleva la voix et dit en langue judaïque: Écoutez les paroles du grand roi des Assyriens.
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
14 Voici ce que dit le roi: Qu'Ézéchias ne vous trompe point par des discours, car il ne pourra vous sauver.
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
15 Qu'Ézéchias ne vous dise pas que Dieu vous protègera et qu'il ne livrera point cette ville aux mains du roi des Assyriens.
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
16 N'écoutez pas Ézéchias, car voici ce que dit le roi des Assyriens: Si vous voulez être bénis, venez à moi, chacun mangera le fruit de sa vigne et ses figues, et vous boirez l'eau de vos citernes,
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
17 Jusqu'à ce que je revienne pour vous transporter en une terre comme votre terre, pleine de pain et de vin, de vignes et de froment.
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
18 Qu'Ézéchias ne vous trompe pas, disant: Dieu vous délivrera; les dieux des nations qui tour à tour sont tombées dans la main du roi les ont-ils délivrées?
“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
19 Où est le dieu d'Émath et d'Arphath? Où est le dieu de la ville d'Éppharvaïm? Est-ce qu'ils ont eu le pouvoir de délivrer Samarie de mes mains?
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
20 Quel est celui des dieux de toutes ces nations qui ait délivré sa terre de mes mains? Dieu délivrera-t-il Jérusalem de mes mains?
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
21 Et le peuple resta muet, et personne ne répondit à ce discours; car le roi avait ordonné de ne rien répondre.
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
22 Et l'économe Éliacim, fils de Chelcias, et le scribe de l'armée Somna, et l'archiviste Joach, fils d'Asaph, rentrèrent auprès d'Ézéchias, et, ayant déchiré leurs tuniques, ils lui rapportèrent les paroles de Rabsacès.
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.