< Isaïe 34 >
1 Approchez, nations; princes, écoutez; que la terre soit attentive, et ceux qui l'habitent.
Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
2 Parce que la colère du Seigneur éclate contre toutes les nations, son courroux menace leur multitude; il les perdra et les livrera au meurtre.
Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
3 Leurs blessés tomberont avec leurs morts; et l'odeur s'en répandra dans l'air, et les montagnes seront humectées de leur sang.
Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
4 Et toute la milice des cieux dépérira, et le ciel sera roulé comme un livre, et toutes les étoiles tomberont comme des feuilles de vigne, comme les feuilles d'un figuier.
Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
5 Mon glaive s'est enivré dans les cieux; voilà qu'il va fondre sur l'Idumée, et sur un peuple justement condamné à périr.
Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
6 Le glaive du Seigneur s'est rempli de sang; il s'est alourdi de graisse, du sang des boucs et du sang des agneaux, de la graisse des boucs et de la graisse des béliers; car le sacrifice du Seigneur est en Bosor, et une grande immolation de victimes en Idumée;
Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
7 Et avec elle les forts tomberont, et les béliers et les taureaux; la terre s'enivrera de leur sang et se rassasiera de leur graisse;
Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
8 Car c'est le jour du jugement du Seigneur; c'est l'année de la juste vengeance de Sion.
Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
9 Et leurs torrents seront changés en poix, et leur terre en soufre; et leurs champs seront comme de la poix qui brûle
Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
10 Nuit et jour, et ne s'éteindra jamais dans la suite des siècles; et la fumée s'en élèvera en l'air; et le pays sera pour longtemps désolé dans ses générations.
Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
11 Les oiseaux, les hérissons, les ibis, les corbeaux en feront leur séjour; le cordeau de la destruction les nivellera, et les onocentaures y résideront.
Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
12 Il n'y aura plus de princes; car ses rois et ses grands ont péri.
Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
13 Et des arbres épineux croîtront dans ses villes et dans ses forteresses; elles seront l'asile des sirènes et l'abri des passereaux.
Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
14 Et les démons s'y rencontreront avec les onocentaures, et ils se crieront l'un à l'autre. C'est là que demeureront les onocentaures; car ils y trouveront un lieu de repos.
Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
15 C'est là que le hérisson a fait son nid, et que la terre y a caché en sûreté ses petits. C'est là que les cerfs se sont rencontrés, et qu'ils se sont vus face à face.
Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
16 Ils y sont venus très nombreux, et pas un n'a péri; ils ne se cherchaient pas l'un l'autre; mais le Seigneur les a conduits, et son souffle les a rassemblés.
Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
17 Et il les a tirés au sort, et sa main leur a distribué des pâturages, disant: Que ce soit à jamais votre héritage; et de génération en génération ils demeureront en cette terre.
Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.