< Isaïe 31 >

1 Malheur à vous qui descendez en Égypte pour chercher du secours, et qui mettez votre confiance en des chevaux et des chars, parce que les chars sont nombreux et que la multitude des cavaliers est grande! Ils n'ont point eu foi au Saint d'Israël, et ils n'ont point cherché le Seigneur.
Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
2 Et dans sa sagesse il leur a envoyé les maux prédits; et sa parole ne sera pas trompée; il s'élèvera contre les maisons des hommes pervers, et contre leur vaine espérance.
Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
3 En un Égyptien, il y a un homme et non un Dieu; en des chairs de chevaux, il n'y a pas de secours; le Seigneur portera la main sur eux; et leurs auxiliaires seront défaillants, et ils périront tous à la fois.
Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
4 Car voici ce que m'a dit le Seigneur: De même qu'un lion ou un lionceau rugit sur la proie qu'il a saisie, et crie jusqu'à ce qu'il ait rempli de sa voix les montagnes; alors les animaux sont abattus, et cette colère les fait tous trembler: ainsi le Seigneur Dieu des armées descendra pour combattre sur la montagne de Sion, sur ses montagnes.
Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
5 Tel un oiseau étend les ailes, tel le Seigneur couvrira Jérusalem; il la protègera et lui fera miséricorde; il prendra soin d'elle et la sauvera.
Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
6 Convertissez-vous, fils d'Israël, qui avez formé au fond de vos cœurs un conseil impie.
Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
7 Car ce jour-là les hommes renonceront aux idoles d'or, aux idoles d'argent, œuvres de leurs mains.
Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
8 Et Assur tombera; ce n'est pas le glaive d'un guerrier, ce n'est pas le glaive d'un homme qui le dévorera, et il ne fuira pas devant la face d'un glaive; et ses jeunes hommes seront en servitude;
“Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
9 Ils seront entourés de pierres comme d'une palissade, et ils seront défaits; et quiconque essayera de fuir sera pris. Voici ce que dit le Seigneur: Heureux celui qui a sa race en Sion, et sa demeure en Jérusalem!
Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.

< Isaïe 31 >