< Isaïe 27 >

1 En ce jour-là Dieu tirera son épée sainte, sa grande et forte épée, contre le dragon fuyant, contre le dragon aux replis tortueux, et il tuera le dragon.
Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
2 Et ce jour-là il y aura un beau vignoble, et le désir de chanter sur la vigne.
Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
3 Je suis une ville forte, une ville assiégée; vainement je lui porterai à boire. Car elle sera prise la nuit, et le jour ses murs tomberont;
Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
4 Il n'est point de femme qui ne s'en soit emparée. Qui me placera pour garder la récolte dans un champ? A cause de cet état de guerre, je l'ai négligée. C'est pourquoi le Seigneur a fait toutes les choses qu'il avait ordonnées. J'ai été brûlée.
Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
5 Ses habitants crieront: Faisons la paix avec lui, faisons la paix.
Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
6 Ceux qui viennent sont des enfants de Jacob. Et Israël germera, et il fleurira, et la terre sera remplie de son fruit.
Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
7 Est-ce que Dieu les frappera, comme il a frappé? Les tuera-t-il comme il a tué les autres?
Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
8 Il les renverra avec des paroles de reproche et de colère. N'est-ce pas vous qui, dans un esprit de dureté, vouliez les tuer du souffle de votre courroux?
Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
9 A cause de cela l'iniquité de Jacob lui sera remise; et cela même sera pour lui une bénédiction, puisque je lui remettrai ses péchés lorsqu'ils auront brisé les pierres de leurs autels, et qu'ils les auront réduits en poudre, et que leurs arbres n'existeront plus, et que leurs idoles seront abattues, comme leurs grands bois sacrés.
Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
10 Le troupeau qui demeure là sera épars comme un troupeau abandonné; et il restera longtemps au pâturage, et le bétail s'y reposera.
Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
11 Et à la longue il ne trouvera plus d'herbe, à cause de la sécheresse. Femmes qui venez de voir un tel spectacle, approchez; car ce peuple est sans intelligence. A cause de cela, celui qui les a formés sera pour eux sans miséricorde; celui qui les a formés ne leur pardonnera point.
Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
12 Et ce jour-là Dieu parquera les hommes depuis le lit du fleuve jusqu'au Rhinocorure. Et vous, rassemblez un à un les fils d'Israël.
Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
13 Et ce jour-là on sonnera à grand bruit de la trompette; et ceux qui étaient perdus en Assyrie, et ceux qui étaient perdus en Égypte reviendront, et ils adoreront le Seigneur sur la montagne sainte, en Jérusalem.
Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.

< Isaïe 27 >