< Isaïe 22 >

1 Parole de la Vallée de Sion. D'où vient que maintenant vous êtes montés sur vos terrasses, disant des paroles
Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
2 Vaines? La ville est pleine de clameurs; tes blessés ne sont pas blessés par le glaive, et tes morts ne sont pas morts en combattant.
Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
3 Tous tes princes sont en fuite; tes captifs sont durement enchaînés, et tes forts se sont réfugiés au loin.
Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
4 Et c'est pourquoi j'ai dit: Laissez-moi et je pleurerai amèrement; ne cherchez pas à me consoler, quand vient d'être brisée la fille de mon sang.
Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
5 Car le jour du trouble et de la ruine, où tout est brisé et s'égare, vient du Seigneur Dieu des armées. Ils errent dans la vallée de Sion; du petit au grand ils errent sur les montagnes.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
6 Les Élamites ont pris leurs carquois; les cavaliers sont à cheval, les armées se rassemblent.
Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
7 Et tes vallons préférés seront remplis de chars, et des cavaliers envahiront les portes de Juda,
Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
8 Et ils en ouvriront les portes; et ce jour-là ils pénètreront dans les demeures choisies de la cité;
ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
9 Et, dans la citadelle de David, ils découvriront les endroits les plus cachés des maisons. Et ils ont vu combien elles sont nombreuses, et comme on a détourné l'eau de l'ancienne piscine pour ramener dans la ville,
mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
10 Et comme on a abattu les maisons de Jérusalem pour fortifier ses remparts.
Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
11 Et ainsi pour vous-mêmes, vous avez fait venir l'eau entre les deux enceintes, plus avant que l'ancienne piscine; mais vous n'avez point considéré celui qui, dès le principe, a bâti la ville, et vous n'avez point vu son Créateur.
Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
12 Et le Seigneur, le Seigneur des armées, vous a en ce jour appelés à pleurer et à gémir, à vous raser la tête et à vous ceindre de cilices;
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
13 Mais eux, ils étaient en joie et en plaisirs à égorger des veaux, à immoler des brebis, à manger de la chair et à boire du vin, disant: Mangeons et buvons, car nous mourrons demain.
Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
14 Et ces choses ont été révélées aux oreilles du Dieu des armées; car ce péché ne vous a pas été remis jusqu'à votre mort.
Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
15 Voici donc ce que dit le Seigneur Dieu des armées: Va trouver, au vestibule du temple, Somna, le trésorier, et dis-lui:
Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
16 Pourquoi es-tu ici, et qu'y fais-tu? Pourquoi as-tu taillé ici ton sépulcre? pourquoi l'as-tu placé sur un lieu élevé, et y as-tu creusé pour toi un lieu de repos?
Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
17 Voilà qu'à présent le Seigneur Dieu des armées va chasser et briser cet homme; il va t'enlever ta robe
“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
18 Et ta couronne de gloire, et il te jettera dans une grande et immense campagne, et là tu mourras; et Dieu fera de ton char brillant un objet de honte, et le palais de ton prince sera foulé aux pieds;
Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
19 Et tu seras renversé de ton rang et de ton ministère.
Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
20 Et ce jour-là j'appellerai mon serviteur Éliacim, fils d'Helcias,
“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
21 Et je le revêtirai de ta robe, et je lui donnerai ta couronne avec l'empire, et je confierai ton ministère à ses mains, et il sera comme un père pour ceux qui résident à Jérusalem et habitent en Judée.
Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
22 Et je lui donnerai la gloire de David, et il gouvernera, et il n'aura point de contradicteur;
Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
23 Et je l'établirai prince en un lieu sûr, et il sera comme un trône de gloire pour la maison de son père.
Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
24 Et tout homme en honneur dans la maison de son père, du petit au grand, mettra sa confiance en lui, et tous dépendront de lui.
Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
25 En ce jour, voilà ce que dit le Seigneur Dieu des armées: L'homme qui avait été établi en un lieu sûr, y sera ébranlé; il en sera arraché, et il tombera, et sa gloire sera anéantie; parce qu'ainsi l'a dit le Seigneur.
Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.

< Isaïe 22 >