< Isaïe 16 >

1 J'enverrai comme des reptiles sur la terre. La montagne de Sion, ma fille, n'est-elle pas une roche déserte?
Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
2 Comme le petit oiseau enlevé à sa mère, ainsi tu seras, fille de Moab. A ton tour, Arnon,
Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
3 Prends plus mûrement conseil, fais à Moab un abri pour y pleurer toujours; ils voudraient l'ombre pour fuir en plein midi, et ils sont dans la stupeur. Si tu veux échapper à la captivité,
“Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
4 O Moab, que mes fugitifs demeurent chez toi; et ils seront pour toi un refuge aux yeux de ton persécuteur; car ton auxiliaire t'est ravi; il a péri le prince qui foulait la terre.
Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
5 Mais un trône sera érigé avec miséricorde, et un roi y siégera avec vérité dans le tabernacle de David, jugeant et cherchant la justice, et plein de zèle pour l'équité.
Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
6 Nous avons appris l'insolence de Moab; son insolence était extrême, et je l'ai abattue; et ses divinations ne se sont point accomplies.
Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
7 Moab poussera des hurlements de douleur, tous les Moabites verseront des pleurs; médite sur les habitants de Seth, et tu ne seras point confondue.
Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
8 Les champs d'Ésebon et la vigne de Sebama seront dans le deuil. O vous qui dévorez les nations, foulez aux pieds les vignes de Sebama jusqu'à Jaser; ne venez pas en foule, errez dans le désert; les rejetons qui avaient été plantés ont été délaissés, et ils ont passé du côté de la mer.
Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
9 C'est pourquoi je pleurerai la vigne de Sebama, comme ceux de Jazer la pleurent. Ésebon et Éléalé ont jeté bas tes arbres, ô Moab; et moi, je foulerai tes blés au temps de la moisson, et tes ceps au temps de la vendange; et tout tombera.
Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
10 Et la joie et les fêtes seront enlevées à tes vignes, et dans tes vignes il n'y aura plus de réjouissances; et on ne foulera plus le vin dans tes pressoirs, car il n'y aura plus de vendange.
Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
11 C'est pourquoi mes entrailles pleureront sur Moab comme une cithare; Seigneur, vous avez tout renouvelé en moi, comme un mur en ruines.
Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
12 Et il arrivera pour sa confusion que Moab, lassé de ses autels, ira vers les idoles fabriquées de ses mains, et il les priera; mais elles ne pourront le sauver.
Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
13 Telle est la prédiction que le Seigneur a prononcée sur Moab.
Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
14 Et maintenant je dis: Dans trois ans, trois ans d'homme à gages, la gloire de Moab sera confondue avec toutes ses nombreuses richesses; et il n'échappera qu'un petit nombre de ses enfants, et ils seront sans honneur.
Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”

< Isaïe 16 >