< Isaïe 10 >

1 Malheur à ceux qui écrivent l'iniquité! car en écrivant ainsi, c'est l'iniquité qu'ils gravent.
Ole wao watimizao sheria zisizo za haki na waandikao sheria zisizo na haki.
2 Ils écartent du pauvre la justice, ils arrachent tout moyen de défense aux indigents de mon peuple, afin que la veuve soit pour eux un butin, l'orphelin une proie.
Wanawanyima wahitaji haki yao, wanawaibia watu wangu walio masikini haki zao, wajane mateka wao, na kuwafanya waliofiwa na baba zao mawindo yao!
3 Et que feront-ils au jour de la visite du Seigneur? car la tribulation viendra sur vous de loin. Vers qui vous réfugierez-vous pour avoir du secours? Et où cacherez-vous votre gloire,
Hutafanya nini siku ya hukumu pale siku ya uaribifu itakapokuja kutoka mbali, utakimbilia msaada kwa nani? na utauacha utajiri wako wapi?
4 Pour n'être point entraînés en captivité? Sur vous tous s'est tournée la colère du Seigneur, et sa main est encore levée.
Hakuna kitakachobaki, utaota miongoni mwa wafungwa au kuanguka miongoni mwa wauwaji. Katika mambo yote haya, hasira yake haijapungua; badala yake mkono wake ameunjoosha hata sasa.
5 Malheur aux Assyriens! la verge de mon courroux, ma colère est dans leurs mains.
Ole kwa watu wa Asiria klabu ya asira yangu, fimbo ya asira yangu!
6 J'enverrai ma colère contre une nation inique, et je commanderai à mon peuple de recueillir du butin et des dépouilles, de fouler aux pieds les villes et de les réduire en poussière.
Nimemtuma juu ya taifa lenye kiburi na juu ya watu waliobeba uwingi wa hasira. Ninaamuru chukua nyara, chukua mawindo, na kuwakanyaga wao kama matope mitaani.
7 Mais lui, telle n'est point sa pensée, tel n'est point le sentiment de son âme. Il mettra son orgueil à exterminer de nombreuses nations.
Lakini hichi sicho alichomaanisha, wala sivyo afikiriavyo. Maana katika moyo wake ni kuharibu na kuondoa mataifa.
8 Et si elles lui disent: Toi seul es roi;
Maana amesema, '' wakuu wote sio wafalme?
9 Il répondra: En effet, n'ai-je point pris la contrée au-dessus de Babylone, et Chalane où une tour a été construite? N'ai-je point pris l'Arabie, et Damas, et Samarie?
Je? kalno si kama Karkemish? Je Hamathi si kama Arpadi? Je Samaria si kama Demeski?
10 Comme je les ai prises, ainsi je prendrai tous les royaumes. Lamentez- vous, statues de Jérusalem et de Samarie!
Kama mikono yangu imeshinda falme za ibada ya sanamu, ikiwa sanamu zao za kuchonga ni bora kuliko sanamu za Yerusalemu
11 Comme j'ai traité Samarie et les dieux fabriqués de ses mains, je traiterai Jérusalem et ses idoles.
na Kama nilivyofanya kule Samaria na sanamu zake zisizo na maana, je sitaweza kufanya hivyo Yerusalemu na sanamu zake?''
12 Puis voici ce qui arrivera: quand le Seigneur aura achevé d'accomplir ce qu'il veut faire en la montagne de Sion et à Jérusalem, je visiterai ce cœur superbe, ce roi des Assyriens, et la gloire altière de ses yeux.
Pindi ambapo Bwana alipoimaliza kazi kwenye mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitayaadhibu maneno ya moyo wenye kiburi ya mfalme wa Asiria na majivuno yake.
13 Car il a dit: J'agirai dans ma force; et dans la sagesse de mon intelligence j'effacerai les bornes des nations, et je les dépouillerai de leur puissance.
Kwa maana amesema, ''Kwa nguvu zangu na kwa hekima yangu niliyoifanya. na Nimeelewa, na nimeondoa mipaka ya watu. nimewaibia akiba yao, ni kama nilioileta chini kwa wenyeji wake.
14 Et j'ébranlerai les villes habitées; et la terre entière, je la prendrai comme un nid dans ma main; et je l'enlèverai comme des œufs abandonnés; car nul ne peut m'échapper ou me contredire.
Na mkono wangu umezitoa mali za mataifa kama vile mtu ayakusanyavyo mayai, kama nilivyokusanya dunia yote. Hakuna atakayeperusha mabawa yake au kufungua midomo yake au kulia.''
15 Mais la cognée peut-elle se glorifier sans celui qui s'en sert pour abattre? La scie peut-elle s'enorgueillir sans celui qui la tire? Il faut bien que quelqu'un lève la verge ou le bâton; mais non.
Je shoka lijisifu lenyewe juu ya mtu anayelitumia? Je litajisifia lenyewe zaidi ya yule anaelitumia kukatia? Au fimbo imuinuae yeye ambaye si mti.
16 Le Seigneur des armées enverra contre ton honneur le déshonneur, et contre ta gloire il allumera un feu ardent.
Hivyo basi Yahwe wa majeshi atatuma wadhaifu miongoni mwa wasomi wa kijeshi; na chini ya utukufu na kuteketea kama kuteketea kwa moto.
17 Et la lumière d'Israël sera cette flamme; elle le sanctifiera avec un feu ardent, et dévorera la forêt comme une herbe sèche.
Mwanga wa Isreli utakuwa moto, na Mtakatifu wake atakuwa ni moto unaoteketeza na kula mbigiri siku moja.
18 En ce jour s'évanouiront montagnes, collines et forêts, et la lumière d'Israël dévorera tout, depuis l'âme jusqu'aux chairs. Et celui qui fuira sera comme un homme qui fuit une flamme ardente;
Yahwe atauteketeza utukufu wa msitu wake na shamba lake linalostawi, vyote nafsi na mwili; itakuwa kama vile mgonjwa apotezae maisha yake.
19 Et ceux qui resteront seront en petit nombre, et un petit enfant pourra les compter.
Mabaka ya miti ya misitu itakuwa michache sana, ambayo mtoto anaweza kuyahesabu.
20 Et en ce jour voici ce qui arrivera: ce qui restera d'Israël, et ceux de Jacob qui auront été sauvés n'auront plus foi en ceux qui leur auront nui; mais ils se confieront en vérité à Dieu, au Saint d'Israël.
Siku hiyo, mabaki ya Israeli, familia ya Yakobo ambayo imekimbia, hawatategemea kushindwa, lakini watamtegemea Yahwe, Mtakatifu wa Israeli.
21 Et ce qui restera de Jacob se confiera au Dieu tout-puissant.
Mabaki ya Yakobo yatarudi kwa Mungu mwenye nguvu.
22 Et quand le peuple d'Israël serait aussi nombreux que le sable de la mer, un reste en sera seul sauvé.
Kwa kupitia watu wako, Israeli ni kama mchanga kama pwani ya bahari, Mabaki yao tu ndio yatakayorudi. Uaribifu wa amri, na mahitaji ya wingi wa haki.
23 Parole abrégée et accomplie avec justice; car cette parole abrégée, le Seigneur l'étendra à toute la terre.
Maana Bwana wa majeshi, anakaribia kuleta uharibifu utachukua nafasi kubwa kitika nchi.
24 A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur des armées: Ne crains pas, ô mon peuple; habitants de Sion, ne craignez pas l'Assyrien; il te frappera avec une verge; car j'amènerai sur toi cette plaie, pour que tu y reconnaisses la voie d'Égypte.
Hivyo basi Bwana Yahwe wa majeshi anasema, ''watu wangu mhishio Sayuni, msiwaogope watu wa Asiria. Atawangamiza nyie kwa fimbo na atawanyua wafanyakazi juu yenu, kama ilivyotokea kwa Wamisri.
25 Encore un peu de temps, et ma colère s'apaisera; mais alors mon courroux se tournera contre les conseils de tes ennemis.
Msimuogope, kwa mda mfupi hasira yangu itakwisha juu yenu, na hasira yangu italeta uharibifu.''
26 Et le Seigneur suscitera contre eux une plaie semblable à celle de Madian dans le lieu de l'affliction; et son courroux éclatera comme autrefois contre l'Égypte sur le chemin de la mer Rouge.
Hivyo Yahwe wa majeshi atapiga mjeledi juu yenu kama vile alivyoishinda Midiani karibu na mwamba Orebu. Na atanyanyua fimbo yake juu ya bahari kama alivyofanya kule Misri.
27 Et en ce jour voici ce qui arrivera: ton joug sera ôté de ton épaule, et tu seras délivré de ta crainte, et le joug qui pesait sur tes épaules sera réduit en poudre.
Siku hiyo mzigo wake utanyanyuliwa kwenye mabeba yako na nira katika shingo yako, nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya unene.
28 Il marchera d'abord sur la ville d'Aggaï, passera par Maggédo et déposera à Machma ses appareils de guerre.
Adui amekuja Aiathi na amepitia Migroni; katika Michmashi ameyahifadhi mahitaji yake.
29 Puis il traversera la vallée et entrera dans Aggaï; la terreur saisira Rama, ville de Saul.
Wamevuka juu ya njia na wamepunzika huko Geba. Rama inatetemeka na Gibea ya Sauli imekimbia.
30 La fille de Gallim prendra la fuite; on l'apprendra à Lasa, on l'apprendra à Anathoth.
Lia kwa sauti, ewe binti wa Galimu! sikiliza, Laishashi! Maskini Anathothi!
31 Et la stupeur a frappé Madebina, et les habitants de Gibbeïr.
Madmena ni mkimbizi na mkazi wa Gebuni wamejikusanya wanakimbia kutafuta msada.
32 Pour vous, consolez-vous aujourd'hui et restez fermes dans la voie; ô vous, collines de Jérusalem, consolez la montagne et Sion, ma fille.
Siku hizi za leo atasimulia huko Nobi na atatingisha mlima wa binti Sayuni, mlima wa Yerusalemu.
33 Voilà que le maître, le Seigneur des armées, va de sa puissance confondre ces glorieux; et les grands seront brisés avec leur orgueil; et les superbes seront humiliés,
Tazama, Bwana Yahwe wa majeshi atapunguza matawi kwa nguvu za kutisha; miti mirefu itakatwa chini, wanaojivuna wataangushwa.
34 Et les superbes périront car le glaive; et le Liban tombera avec ses cîmes.
Atang'oa vichaka vya msitu kwa shoka, Lebanoni na utukufu wake utaanguka.

< Isaïe 10 >