< Osée 13 >

1 À la parole de Jéroboam, Éphraïm a pris lui-même des commandements en Israël et les a mis devant Baal, et Éphraïm est mort.
Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
2 Et maintenant ils continuent de pécher, et ils se sont fait de leur argent des statues en fonte à l'image des idoles, œuvres accomplies d'un artiste; et ils se disent entre eux: Sacrifiez des hommes, car il y a disette de bœufs!
Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
3 À cause de cela, ils seront comme le nuage du matin, comme la rosée qui vient à l'aurore, comme la poudre que le vent emporte hors de l'aire, comme la vapeur des larmes.
Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
4 Moi, le Seigneur ton Dieu, qui ai affermi le ciel; Moi, le Créateur de la terre, Moi, dont les mains ont créé toute l'armée céleste, Je ne t'ai point montré ces créatures pour que tu chemines après elles; c'est Moi qui t'ai délivré de la terre d'Égypte, et tu ne connaîtras point d'autre Dieu que Moi, et nul autre que Moi ne sauve.
“Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
5 J'ai été ton pasteur dans le désert, en une terre inhabitée
Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
6 et sans pâturages; et ils s'y sont rassasiés et remplis, et leurs cœurs se sont enorgueillis, et à cause de cela ils M'ont oublié.
Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
7 Et Je serai pour eux comme une panthère et comme un léopard, sur la route de l'Assyrie.
Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
8 J'accourrai au-devant d'eux comme une ourse affamée, et Je briserai l'enveloppe de leurs cœurs, et les lionceaux de la forêt les dévoreront, et les bête fauves les mettront en lambeaux.
Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
9 En ta destruction, ô Israël, qui te portera secours?
“Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
10 Où est celui-là? Est-ce ton roi? Qu'il te sauve en toutes tes villes; qu'il te juge celui à qui tu as dit: Donne-moi un roi et un prince!
Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
11 Je t'ai donné un roi dans Ma colère, et Je t'ai traité dans Mon courroux.
Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
12 Éphraïm a fait un complot d'iniquité; son impiété a été cachée.
Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
13 Les douleurs de la femme qui enfante lui viendront. celui-là est ton fils, le Sage, parce qu'il ne se tiendra pas immobile pendant le massacre de tes enfants.
Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
14 Je les tirerai de l'enfer, dira-t-il; je les affranchirai tous de la mort. Ô mort, où est ta sentence? Enfer, où est ton aiguillon? Mais cette consolation est cachée à mes yeux. (Sheol h7585)
“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol h7585)
15 Et quand l'enfer sèmera la division entre les frères, le Seigneur enverra contre lui un vent brûlant du désert, et Il desséchera les veines de la mort, et Il tarira ses sources; Lui-même fera de ses champs une terre aride, et enlèvera ses vases les plus précieux. (questioned)
hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
16 Samarie sera détruite, parce qu'elle s'est révoltée contre son Dieu. Ils périront par le glaive; tous ses enfants à la mamelle seront écrasés à terre, et les femmes enceintes seront déchirées.
Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

< Osée 13 >