< Genèse 8 >
1 Puis, Dieu se souvint de Noé, et de toutes les bêtes fauves, et de tous les bestiaux, et de tous les oiseaux, et de tous les reptiles qui étaient avec lui dans l'arche. Il fit souffler un vent sur la terre, et l'eau céda.
Mungu akamtazama Nuhu, wanyama wote wa mwitu, na wanyama wote wa kufugwa ambao walikuwa pamoja naye kwenye safina. Mungu akafanya upepo uvume juu ya nchi, na maji yakaanza kuzama chini.
2 Les sources de l'abîme furent fermées, ainsi que les cataractes du ciel, et la pluie du ciel cessa.
Chemichemi za vilindi pamoja na madirisha ya mbingu vikafungwa, na mvua ikakoma kunyesha.
3 L'eau qui fuyait sur la terre s'affaissa, et diminua après cent cinquante jours.
Maji ya gharika yakaanza kuzama kidogo kidogo katika nchi. na mwisho wa siku miamoja na hamsini maji yakawa yamezama chini.
4 Et, le vingt-septième jour de la septième lune, l'arche s'arrêta sur le mont Ararat.
safina ikatulia katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, juu ya milima ya Ararati.
5 Or, l'eau diminua jusqu'à la dixième lune, et, le premier jour de la dixième lune, les cimes des montagnes apparurent.
Maji yakaendelea kuzama chini hadi mwezi wa kumi. Siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.
6 Après quarante jours, Noé ouvrit la porte de l'arche qu'il avait faite,
Ikatokea kwamba baada ya siku arobaini Nuhu alifungua dirisha la safina ambayo aliitengeneza.
7 Et fit partir un corbeau, qui, étant sorti, ne revint plus, même après que l'eau se fut desséchée sur la terre.
Akatuma kunguru na akaruka hadi maji yalipo kauka katika nchi.
8 Après lui, Noé envoya une colombe pour voir si l'eau s'était retirée de la terre.
Kisha akatuma njiwa kuona kama maji yamezama chini kutoka kwenye uso wa nchi,
9 Mais la colombe, n'ayant point trouvé où poser ses pieds, revint auprès de lui dans l'arche, parce que l'eau était sur toute la surface de la terre. Et, ayant étendu la main, il la prit et l'introduisit auprès de lui dans l'arche.
lakini njiwa hakuona sehemu ya kutua unyayo wake, na akarudi kwake ndani ya safina, kwa kuwa maji yalikuwa bado yamefunika nchi yote. Akanyoosha mkono wake, akamchukua na kumuweka ndani ya safina pamoja naye.
10 Puis, après avoir attendu sept jours encore, il fit de nouveau partir de l'arche la colombe.
Akasubiri siku saba zingine akatuma tena njiwa kutoka kwenye safina.
11 Et sur le soir la colombe revint près de lui, tenant en son bec un brin de branche et une feuille d'olivier. Noé reconnut alors que l'eau s'était retirée de la terre.
Njiwa akarudi kwake jioni. Tazama! katika mdomo wake kulikuwa na jani bichi la mzeituni lililochumwa. Kwa hiyo Nuhu akatambua kuwa maji yamekwisha zama chini ya nchi.
12 Et après avoir attendu encore sept jours, il fit de nouveau partir la colombe, qui ne revint plus auprès de lui.
Akasubiri siku saba zingine na akamtuma njiwa tena. Njiwa hakurudi kwake tena.
13 Or, l'an six cent un de la vie de Noé, le premier jour de la première lune, l'eau disparut sur la terre. Et Noé ouvrit le toit de l'arche qu'il avait faite et vit que l'eau s'était retirée de la face de la terre
Ikawa kwamba katika mwaka wa mia sita na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, akatazama nje, na akaona kwamba, Tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka.
14 Et, le vingt-septième jour de la seconde lune, la terre se trouva sèche.
Katika mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, nchi ilikuwa imekauka.
15 Et le Seigneur Dieu parla à Noé, disant:
Mungu akamwambia Nuhu,
16 Sors de l'arche avec ta femme, et tes fils, et les femmes de tes fils, et toutes les bêtes fauves qui sont auprès de toi,
“Toka nje ya safina, wewe, mke wako, wanao wa kiume, na wake wa wanao pamoja nawe.
17 Et toute chair, depuis les oiseaux jusqu'aux bestiaux; fais aussi sortir tout reptile se traînant à terre; et croissez et multipliez.
Wachukuwe utoke nje pamoja nao kila kiumbe hai chenye mwili ambacho kiko nawe - ndege, wanyama wa kufugwa, na kila kitambaacho ambacho hutambaa juu ya nchi - ili kwamba viweze kukua na kuwa na idadi kubwa zaidi ya viumbe hai katika nchi yote, kwa kuzaliana na kuongezeka juu ya nchi.”
18 Noé sortit donc avec sa femme, et ses fils, et les femmes de ses fils;
Kwa hiyo Nuhu akatoka nje pamoja na watoto wake wa kiume, mke wake, na wake wa wa wanawe pamoja naye.
19 Et toutes les bêtes fauves, et tous les bestiaux, et tout oiseau, et tout reptile se traînant à terre, selon leurs espèces, sortirent avec lui.
Kila kiumbe hai, kila kitambaacho, na kila ndege, na kila kiendacho juu ya nchi, kwa kabila zao, wakaiacha safina.
20 Et Noé éleva un autel au Seigneur; puis il prit de tous les bestiaux purs, et de tous les oiseaux purs, et il en offrit sur l'autel un holocauste au Seigneur.
Nuhu akajenga madhabahu kwa Yahwe. Akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya ndege walio safi, na kutoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 Et le Seigneur Dieu respira un parfum délicieux. Et le Seigneur Dieu, ayant réfléchi, dit: Je ne veux plus maudire la terre à cause des œuvres des hommes, parce que l'esprit de l'homme, dès sa jeunesse, se complaît dans le mal. Je ne veux donc plus frapper toute chair vivante, comme je l'ai fait.
Yahwe akanusa harufu nzuri ya kuridhisha na akasema moyoni mwake, “Sita laani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, ingawa nia za mioyo yao ni mbaya tokea utoto. Wala sita haribu kilakitu chenye uhai, kama nilivyo fanya.
22 Tous les jours de la terre, les semailles et la moisson, le froid et l'ardente chaleur, l'automne et le printemps, ne se reposeront jamais plus, ni jour ni nuit.
Wakati nchi isaliapo, majira ya kupanda mbegu na mavuno, baridi na joto, kiangazi na majira ya baridi, mchana na usiku havitakoma.”