< Genèse 23 >
1 Or, la vie de Sarra atteignit cent vingt-sept ans.
Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba. Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara.
2 Et Sarra mourut en la ville d'Arboc, dans la vallée (c'est aujourd'hui Hébron, en la terre de Chanaan). Abraham y vint pour pleurer Sarra et mener grand deuil.
Sara akafa katika Kiriathi Arba, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abraham akaomboleza na kumlilia Sara.
3 Ensuite Abraham partit d'auprès de sa morte, et il parla aux fils de Het, disant:
Kisha Abraham akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa, akanena na watoto wa kiume wa Hethi, akisema,
4 Je suis parmi vous passager et voyageur; accordez-moi donc l'achat d'un sépulcre parmi vous, et, me séparant de ma morte, je l'ensevelirai.
“Mimi ni mgeni kati yenu. Tafadhari nipatieni mahali pa kuzikia miongoni mwenu, ili kwamba niweze kuzika wafu wangu.”
5 Les fils de Het répondirent à Abraham, disant:
Wana wa Hethi wakamjibu Abraham, wakasema,
6 Non, Seigneur, écoute-nous: Tu es parmi nous un roi suscité de Dieu; ensevelis ta morte en nos sépulcres d'élite; nul de nous ne refusera de te céder son propre sépulcre pour que tu l'y ensevelisses.
“Tusikilize, bwana wangu. Wewe ni mwana wa Mungu miongoni mwetu. Zika wafu wako katika makaburi yetu utakayochagua. Hakuna miongoni mwetu atakaye kuzuilia kaburi lake, kwa ajili ya kuzikia wafu wako.”
7 Et, s'étant levé, Abraham se prosterna devant les fils de Het, peuple de cette terre,
Abraham akainuka na kusujudu chini kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi.
8 En disant: Si votre cœur consent que j'ensevelisse ici ma morte que je ne verrai plus, écoutez-moi, et parlez en ma faveur à Éphron, fils de Saar,
Akawaambia, akisema, “ikiwa mmekubali mimi kuzika wafu wangu, ndipo nisikilizeni, msihini Efroni mwana wa Sohari kwa ajili yangu.
9 Pour qu'il me donne la double caverne qui lui appartient, celle qui fait partie de son champ; qu'il me la cède à prix d'argent, pour être ma sépulture au milieu de vous.
Mwambieni aniuzie pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake. Kwa bei kamili aniuzie waziwazi mbele ya watu kama miliki ya kuzikia.”
10 Or, Éphron était assis parmi les fils de Het; et répondant à Abraham, l'Hettéen, Éphron parla, les fils de Het l'entendant, ainsi que tous ceux qui entraient dans la ville, et il dit:
Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi, hivyo Efroni Mhiti akamjibu Abraham alipowasikia wana wa Hethi, wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake, akasema,
11 Viens près de moi, Seigneur, et écoute-moi: Le champ et la caverne qu'il contient, je te les donne; je te les donne en présence de tous mes concitoyens; ensevelis ta morte.
“Hapana, bwana wangu, nisikilize. Ninakupatia shamba na pango ambalo limo ndani yake. Ninakupatia mbele ya wana wa watu wangu. Ninakupatia uzike wafu wako.”
12 Abraham se prosterna devant le peuple de cette terre;
Kisha Abraham akasujudu chini mbele ya watu wa nchi ile.
13 Et il dit à Éphron, en présence du peuple de cette terre: Puisque tu m'es favorable, écoute-moi: reçois le prix du champ, et j'y ensevelirai ma morte.
Akamwambia Efroni watu wa nchi ile wakisikiliza, akasema, ikiwa uko radhi, tafadhari nisikilize. Nitalipia shamba. Chukua fedha kwangu, na nitazika wafu wangu pale.”
14 Éphron répondit à Abraham:
Efroni akamjibu Abraham, akisema,
15 Nullement, Seigneur, j'ai bien entendu; la terre est de quatre cents doubles drachmes d'argent; mais qu'est-ce que cela peut faire entre moi et toi? Ensevelis donc ta morte.
“Tafadhari bwana wangu, nisikilize. Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe? wazike wafu wako.”
16 À ces paroles d'Éphron, Abraham plaça devant lui l'argent qu'il avait dit, au su des fils de Het: quatre cents doubles drachmes d'argent, éprouvé par les marchands.
Abraham akamsikiliza Efroni na akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema mbele ya wana wa Helthi wakisikiliza, shekeli mia nne za fedha, kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara.
17 Ainsi le champ d'Éphron, avec sa double caverne, qui est en face de Membré, le champ et la caverne, et tous les arbres du champ et tout ce qui se trouvait compris dans ses limites,
Kwa hiyo shamba la Efroni, lililokuwa katika Makpela, mbele ya Mamre, shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote iliyokuwamo ndani ya shamba na iliyokuwa mpakani ikatolewa
18 Furent acquis à Abraham, en présence des fils de Het, et de tous ceux qui entraient en cette ville.
kwa Abraham kwa njia ya manunuzi mbele ya wana wa Hethi, na mbele ya wote waliokuja malangoni pa mji wake.
19 Après cela, Abraham ensevelit Sarra sa femme dans la double caverne du champ, laquelle fait face à Membré: aujourd'hui Hébron, en la terre de Chanaan.
Baada ya haya, Abraham akamzika Sara mkewe katika pango la shamba la Makpela, lililo mbele ya Mamre, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani.
20 Et le champ et la caverne qu'il contenait furent confirmés à Abraham, comme sépulture, par les fils de Het.
Kwa hiyo shamba pamoja na pango likatolewa na wana wa Hethi kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia.