< Genèse 11 >

1 Toute la terre avait alors une même parole; il y avait une seule langue pour tous.
Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
2 Et il arriva qu'en s'éloignant de l'Orient, ils trouvèrent en la terre de Sennaar une plaine où ils s'établirent.
Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
3 Et chacun dit à son voisin: Allons, façonnons des briques et faisons-les cuire au feu. La brique leur servit donc de pierre, et le bitume de ciment.
Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
4 Puis ils dirent: Allons, bâtissons-nous une ville et une tour dont la tête ira jusqu'au ciel, et faisons-nous un nom, avant de nous disséminer sur toute la face de la terre.
Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
5 Le Seigneur descendit voir la ville et la tour que bâtissaient les fils des hommes.
Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
6 Et il dit: Les voilà une seule famille, avec une seule et même langue, et s'ils ont commencé par de tels travaux, rien désormais ne pourra échouer de tout ce qu'ils entreprendront.
Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
7 Allons, et étant descendus, confondons ici leur langage de telle sorte que nul n'entende plus la parole de son voisin.
Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
8 Et de ce lieu, Dieu les dispersa sur la face de toute la terre, et ils cessèrent de bâtir la ville et la tour.
Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
9 À cause de cela, ce lieu fut appelé Babel (confusion), parce que là le Seigneur confondit les langues de toute la terre, et dispersa les hommes sur la face de toute la terre.
Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
10 Or, voici les générations de Sem: le fils Sem avait cent ans lorsqu il engendra Arphaxad, deux ans après le déluge.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
11 Sem vécut, après avoir engendré Arphaxad, cinq cents ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
12 Arphaxad vécut cent trente-cinq ans, et il engendra Caïnan.
Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
13 Arphaxad vécut, après avoir engendré Caïnan, quatre cent trente ans, et il engendra des fils et des filles, et il mourut. Caïnan vécut trente ans, et il engendra Salé. Caïnan vécut, après avoir engendré Salé, cent trente ans, et il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
14 Salé vécut cent trente ans, et il engendra Héber.
Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Et Salé vécut, après avoir engendré Héber, trois cent trente ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
16 Héber vécut cent trente-quatre ans, et il engendra Phaleg.
Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Et Héber vécut, après avoir engendré Phaleg, deux cent soixante-dix ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
18 Phaleg vécut cent trente ans, et il engendra Réhu.
Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Et Phaleg vécut, après avoir engendré Réhu, deux cent neuf ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
20 Réhu vécut cent trente-deux ans, et il engendra Sarug.
Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
21 Et Réhu vécut, après avoir engendré Sarug, deux cent sept ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
22 Sarug vécut cent trente ans, et il engendra Nachor.
Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Et Sarug vécut, après avoir engendré Nachor, deux cents ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
24 Nachor vécut soixante-dix-neuf ans, et il engendra Tharé.
Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Et Nachor vécut, après avoir engendré Tharé, cent vingt-neuf ans; il engendra des fils et des filles, et il mourut.
Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
26 Tharé vécut soixante-dix ans, et il engendra Abram, Nachor et Aram.
Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
27 Or voici les générations de Tharé: Tharé engendra Abram, Nachor et Aram, lequel engendra Lot.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
28 Et Aram mourut devant son père Tharé, en la terre où il était né, au pays des Chaldéens.
Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
29 Et Abram ainsi que Nachor épousèrent des femmes. Le nom de la femme d'Abram était Sara; et le nom de la femme de Nachor, Melcha, fille d'Aran, père de Melcha et d'Iescha.
Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
30 Sara était stérile, et elle n'enfanta point.
Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
31 Tharé prit Abram son fils, et Lot fils d'Aran, son petit-fils, et Sara, femme d'Abram, son fils, et il les emmena du pays des Chaldéens pour être transportés en la terre de Chanaan; ils allèrent ainsi jusqu'à Haran et ils y demeurèrent.
Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
32 Et tous les jours de Tharé, en la terre de Haran, formèrent deux cent cinq ans, et il mourut à Haran.
Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.

< Genèse 11 >