< Genèse 10 >

1 Voici les générations des fils de Noé: Sem, Cham et Japhet; des fils leur naquirent après le déluge.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 Fils de Japhet: Gomer, Magog, Madaï, Javan, Elisa, Thubal, Mosoch et Thiras.
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 Fils de Gomer: Ascenez, Riphat, et Thogorma.
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 Fils de Javan: Elisa, Tharsis, Cettim et Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 Ceux-ci sont les pères des gentils, qui se partagèrent les îles et les eurent pour territoire, chacun selon sa langue, par tribus, par nations.
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 Fils de Cham: Chus, Mesraïm, Phuth et Chanaan.
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 Fils de Chus: Saba, Hevila, Sabatha, Regma et Sabathaca. Fils de Regma: Saba et Dadan.
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 Et Chus engendra Nemrod: celui-ci commença à être puissant sur la terre.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 Il était grand chasseur devant le Seigneur; c'est pourquoi l'on dit: Grand chasseur comme Nemrod devant le Seigneur.
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 Le commencement de son royaume fut Babylone, puis il eut Arach, Archad, Chalané, et la terre de Sennaar.
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 De cette terre sortit Assur, qui bâtit Ninive, et la ville de Rhooboth et Chalé,
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 Et Ressen, grande ville, entre Ninive et Chalé.
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 Mesraïm engendra les Ludim, les Ananim, les Laabim, les Nephtuïm,
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 Les Phétrusim, les Chasluïm (d'où est sorti Philistin) et les Caphtorins.
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 Chanaan engendra Sidon son premier-né, puis le Hétéen,
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 Le Jebuséen, l'Amorrhéen, le Gergéséen,
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 L'Evéen, l'Arucéen, l'Asennéen,
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 L'Aradien, le Samaréen et l'Amathéen. Après cela, les tribus des Chananéens se dispersèrent.
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 Les limites des Chananéens étaient la côte depuis Sidon jusqu'à Gérara et Gaza; puis elles s'étendirent jusqu'à Sodome et Gomorrhe, et passèrent par Adama et Séboïm jusqu'à Léba.
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 Tels furent les fils de Cham et leurs tribus, selon leurs langues, par contrées, et par nations.
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 Sem fut père aussi, et eut Héber de l'un de ses fils, frère de Japhet le plus grand.
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 Fils de Sem: Elam, Assur, Arphaxad, Lud, Aran et Caïnan.
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 Fils d'Aram: Hus, Hul, Gether et Mosoch.
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 Arphaxad engendra Salé, et Salé engendra Héber.
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 D'Héber naquirent deux fils, nommés, l'un Phaleg, parce que de son temps la terre fut partagée, et l'autre Jectan.
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 Or, Jectan engendra Elmodad, Saleph, Asarmoth Jaré,
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Aduram, Uzal, Décla,
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 Abimaël, Saba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ophir, Hévila et Jobab: tels furent les fils de Jectan.
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Ils habitèrent depuis Messa jusqu'à Séphar, montagne de l'Orient.
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 Tels furent les fils de Sem et leurs tribus, selon leurs langues, par contrées et par nations.
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 Telles furent les tribus des fils de Noé, par familles et nations; et c'est ainsi que les fils de Noé peuplèrent les pays des nations, sur la terre, après le déluge.
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.

< Genèse 10 >