< Esdras 7 >

1 Et, après ces événements, sous le règne d'Arthasastha, roi des Perses, partit Esdras, fils de Saraïas, fils d'Azarias, fils d'Helcias,
Sasa baada ya hili, kipindi cha kutawala Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra akaja kutoka Babeli. Watangulizi wa Ezra walikuwa: Seraya, Azaria, Hilkia,
2 Fils de Selum, fils de Saddoc, fils d'Achitob,
Shalumu, Sadoki, Ahitubu,
3 Fils de Samarias, fils d'Esrias, fils de Maréoth,
Amaria, Azaria, Merayothi,
4 Fils de Zaraïas, fils d'Ozias, fils de Bocci,
Zerahia, Uzi, Buki,
5 Fils d'Abisué, fils de Phinéès, fils d'Eléazar, fils d'Aaron le premier prêtre.
Abishaua, Fineasi, Eliazari ambaye ni mtoto wa Haruni kuhani mkuu.
6 Cet Esdras partit de Babylone; il était scribe et très instruit en la loi de Moïse donnée par le Seigneur Dieu d'Israël. Et le roi le lui permit, parce que la main du Seigneur son Dieu était près de lui en tout ce qu'il demandait.
Ezra akaja kutoka Babeli na alikuwa mtalaam mwandishi wa sheria ya Musa, ambayo Yahwe, Mungu wa Israel aliwapa. Mfalme akampatia kila kitu alichooomba kwa kuwa mkono wa Yahwe ulikuwa pamoja naye.
7 Et des chantres, et des portiers, et des Nathinéens, parmi les fils d'Israël, prêtres ou lévites, partirent pour Jérusalem en la septième année du règne du roi Arthasastha.
Baadhi ya wazao wa Israel, na makuhani, walawi, waimbaji, walinzi, na wale waliochaguliwa kuhudumu katika Hekalu pia wakaenda Yerusalem katika mwaka wa saba wa mfalme Artashasta.
8 Et ils arrivèrent à Jérusalem le cinquième mois de cette même année;
Naye akafika Yerusalem mwezi wa tano kama mwaka huo.
9 Car, le premier jour du premier mois, ils commencèrent à partir de Babylone, et, le premier jour du cinquième mois, ils entrèrent à Jérusalem, parce que la main du Seigneur était favorable à Esdras.
Naye akaondoka Babeli siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza. Ilikuwa siku ya kwanza ya mwezi wa tano ambapo alifika Yerusalem, kwa kuwa mkono mzuri wa Mungu ulikuwa pamoja naye.
10 Esdras, en effet, s'était adonné de tout son cœur à étudier la loi, à la mettre en pratique, et à enseigner aux fils d'Israël les commandements et les préceptes.
Ezra alikuwa ametoa moyo wake kusoma, kutenda, na kufundisha maagizo na sheria za Yahwe.
11 Et voici la traduction de l'ordre qu'Arthasastha donna à Esdras, scribe du livre des lois et commandements du Seigneur, plus de ses prescriptions concernant Israël:
Hii ndio amri ambayo mfalme Artashasta alimpa Ezra kuhani na mwandishi wa sheria za Yahwe na maagizo kwa Israeli.
12 Arthasastha, roi des rois, à Esdras, scribe de la loi du Seigneur Dieu du ciel: Que ta demande et ma réponse s'accomplissent.
Mfalme wa wafalme Artashasta, kwa kuhani Ezra, mwandishi wa sheria za Mungu wa mbinguni.
13 J'ai fait un édit pour que, dans mon royaume, tout homme du peuple d'Israël, et des prêtres, et des lévites, qui le voudra, parte avec toi pour Jérusalem.
Ninatoa amri kwamba mtu yeyote Israel katika ufalme wangu pamoja na makuhani na walawi ambao wanatamani kwenda Yerusalem, wanaweza kwenda pamoja na wewe.
14 Esdras est envoyé par le roi et ses sept conseillers, pour visiter la Judée et Jérusalem, conformément à la loi de Dieu qui est en ta main.
Mimi mfalme na washauri wangu saba, tunawatuma wote kwenda kufahamu kuhusu Yuda na Yerusalem kuhusiana na sheria ya Mungu, ambayo iko mkononi mwako.
15 Et tu porteras l'or et l'argent que le roi et ses conseillers offrent volontairement, pour le temple du Seigneur, au Dieu d'Israël qui réside en Jérusalem,
Itakupasa kuleta Dhahabu na fedha ambazo walitoa kwa ajili ya Mungu wa Israel, ambaye makazi yake ni Yerusalem.
16 Et tout l'argent et l'or que tu recueilleras en tout le royaume de Babylone, donné volontairement par le peuple et les prêtres, pour le temple de Dieu, à Jérusalem.
Fedha iliyotolewa kwa hiari na Dhahabu yote iliyotolewa Babeli pamoja na matoleo ya hiari waliotoa watu na makuhani kwa ajili ya nyumba ya Mungu katika Yerusalem.
17 À tous ceux qui iront à ce temple, prescris équitablement, selon ta loi, d'amener des agneaux avec leurs oblations et leurs libations; tu les offriras sur l'autel du temple du Seigneur votre Dieu à Jérusalem.
Basi ununue vyote sadaka ya kondoo, beberu, kondoo, unga na kinywaji, uvitoe kwenye madhabahu ambayo ni nyumba ya Mungu wako katika Yerusalem.
18 Et si à toi et à tes frères il plaît, avec le reste de l'or et de l'argent, de faire quelque chose, faites-le comme il sera agréable à votre Dieu;
Fanya hivyo pamoja na sehemu ya fedha na dhahabu, vyovyote utakavyoona inakupendeza wewe na ndugu zako, kumpendeza Mungu.
19 Et remettez en leur place, devant Dieu à Jérusalem, les vases qui te sont donnés pour le service du temple de Dieu.
Viweke vitu vilivyotolewa kwa hiari mbele yako kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu Yerusalem.
20 S'il est en outre des choses nécessaires au temple de ton Dieu qu'il te semble bon de donner, tu les donneras aux frais du trésor royal
Kitu chochote kingine ambacho kinahitajika kwenye nyumba ya Mungu wako ambacho unahitaji, Gharama yake itatoka kwenye hazina yangu.
21 Et de mon domaine. Moi, Arthasastha, roi, j'ai fait un édit pour que l'on donne promptement à Esdras, prêtre et scribe du Dieu du ciel, tout ce qu'il vous demandera des trésors publics qui sont au delà de l'Euphrate,
Mimi mfalme Artashasta, natoa amri kwa wotunza hazina wote mjini ngambo ya mto, chochote Ezra atakachoomba kwenu anapaswa kupewa chote,
22 Jusqu'à cent talents d'argent, cent mesures de froment, cent tonneaux de vin, cent tonnes d'huile; outre le sel, dont la quantité n'est pas fixée.
hata zaidi ya talanta mia moja za fedha, vipimo mia vya ngano, bathi mia za divai na bathi mia za mafuta, pia na chumvi isiyo na kikomo.
23 Que tout ce qui est selon la volonté du Dieu du ciel soit exécuté. Et vous, mes serviteurs, veillez à ce que nul ne mette la main sur le temple du Dieu du ciel, de peur que sa colère ne s'allume contre le royaume du roi et de ses fils.
Chochote ambacho kimeamriwa kutoka kwa Mungu wa mbinguni, kifanye hicho kwa utukufu wa nyumba yake. Kwa nini hasira yake ije kwenye ufalme wangu na watoto wangu?
24 Sachez aussi, pour ce qui regarde tous les prêtres, lévites, chantres, portiers, Nathinéens, employés au service de ce Dieu, qu'ils n'ont point à vous payer d'impôt, et que vous n'avez point le pouvoir de leur rien demander de servile.
Tutawapa taarifa wao kuhusu ninyi kwamba wasiwatoze ushuru wowote au kodi kwa kuhani, mlawi, mwimbaji, mlinzi au kwa mtu aliyechaguliwa kwenye huduma ya Hekalu na mtumishi katika nyumba ya Mungu.
25 Et toi, Esdras, comme tu as en ta main la sagesse de Dieu, institue des scribes et des juges, afin qu'au delà du fleuve ils rendent la justice à tout le peuple, à tous ceux qui connaissent la loi de ton Dieu, et enseignez cette loi à ceux qui l'ignorent.
Ezra, kwa hekima aliyokupa Mungu, inakulazimu kuteua waamuzi na mtu muelewa kuwahudumia watu katika mji ngambo ya mto na kusaidia yeyote anayejua sheria za Mungu wako. Pia inakubidi ufundishe wale ambao hawajui sheria.
26 Et quiconque ne se conformera pas avec zèle à la loi de Dieu et à la loi royale, sera jugé et condamné à mort, ou à une correction, ou à l'amende sur son bien, ou à la prison.
Toa adhabu kwa yeyote asiyetii sheria ya Mungu au sheria ya mfalme, ikiwezekana kwa kifo, kuhamishwa, kuchukuliwa mali zake au kufungwa.
27 Béni soit le Seigneur Dieu de nos pères, qui a donné au roi un tel cœur, pour glorifier le temple du Seigneur à Jérusalem,
Atukuzwe, Yahwe, Mungu wa watangulizi wetu, ambaye aliweka ndani ya moyo wa mfalme ili kutuza Nyumba ya Yahwe Yerusalem,
28 Et qui a fait tourner sur moi les yeux et la miséricorde du roi, de ses conseillers, des chefs du royaume et des grands. Et moi, j'ai été fortifié par la main bienveillante de Dieu qui s'est posée sur moi, et j'ai rassemblé les chefs d'Israël pour les emmener avec moi.
ambaye akaendeleza agano kwangu kwa uaminifu mbele ya mfalme, na washauri wake na wakuu wake wenye mamlaka, nilitiwa nguvu na mikono ya Yahwe, Mungu wangu, nami nikawakusanya viongozi kutoka Israel kwenda pamoja nami.

< Esdras 7 >