< Ézéchiel 43 >

1 Et il me conduisit vers la porte qui regarde l'orient et il me fit entrer.
Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
2 Et voilà que la gloire du Dieu d'Israël vint par la voie de l'orient, et le bruit qu'elle fit à son entrée était comme le bruit d'une grande multitude qui redouble ses clameurs; et à l'entour de cette gloire la terre resplendit comme une flamme.
nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
3 Et la vision que j'eus fut comme la vision que j'avais eue lorsque je vins pour marquer la ville. Et j'eus la vision d'un char, comme dans la vision que j'avais eue sur le fleuve Chobar. Et je tombai la face contre terre.
Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
4 Et la gloire du Seigneur entra dans le temple par la voie de la porte qui regarde l'orient.
Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
5 Et l'Esprit me ravit, et il m'introduisit dans le parvis intérieur, et voilà que le temple était plein de la gloire de Dieu.
Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
6 Et je me tins immobile; et voilà qu'une voix me parla du temple, et l'homme se tenait auprès de moi.
Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
7 Et la voix me dit: Fils de l'homme, tu vois la place de mon trône et la trace de mes pieds; c'est ici que mon nom s'abritera pour tous les siècles au milieu de la maison d'Israël. Et la maison d'Israël, ses enfants et leurs rois ne profaneront plus mon saint nom, soit par leurs prostitutions, soit par les meurtres qu'au milieu d'eux commettaient leurs rois,
Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
8 Lorsqu'ils avaient mon portique près de leurs portiques, et mes portes auprès de leurs portes. Et ils avaient fait de mon mur comme un lien entre eux et moi; mais ils ont profané mon saint nom par leurs iniquités. Et je les ai broyés en ma colère, et ils ont péri.
Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
9 Et maintenant, qu'ils répudient loin de moi leurs prostitutions, et je m'abriterai au milieu d'eux dans tous les siècles.
Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
10 Et toi, fils de l'homme, montre ce temple à la maison d'Israël, et ils cesseront de pécher; montre-leur son plan et sa distribution.
“Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
11 Et eux-mêmes accepteront les châtiments de toutes les choses qu'ils ont faites. Décris-leur le temple, ses issues, toute sa structure; fais-leur connaître ses règlements et toutes ses lois; décris-les devant eux, et ils garderont mes ordonnances et mes commandements, et ilsles mettront en pratique.
Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
12 Et tu leur montreras le plan du temple sur le sommet de la montagne, et toute son étendue sera sainte et sacrée.
“Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
13 Et voici les mesures de l'autel: il sera d'une grande coudée, c'est-à-dire d'une coudée et un palme; sa cavité aura une coudée; il aura une coudée de large, et un palme pour la corniche du rebord tout alentour. Et voici la hauteur de l'autel:
“Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
14 À partir du commencement de la cavité jusqu'au grand propitiatoire, deux coudées de haut sur une de large; et du petit propitiatoire an grand propitiatoire, quatre coudées de haut et une de large.
Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
15 Et l'Ariel sera de quatre coudées, et à partir de l'Ariel, au-dessous des cornes, il y aura une coudée.
Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
16 Et l'Ariel sera long de douze coudées sur douze de large; c'est un tétragone aux côtés égaux.
Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
17 Et le propitiatoire sera long de quatorze coudées sur quatorze de large; ses quatre côtéssont égaux. Et il a tout alentour une corniche d'une demi-coudée en saillie d'une coudée de hauteur; et ses degrés regardent l'orient.
Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
18 Et la voix me dit: Fils de l'homme, ainsi parle le Seigneur Dieu d'Israël: Voici la règle pour l'autel: du jour où il aura été fait, on y offrira des holocaustes, et on y versera le sang des victimes:
Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
19 Et tu donneras aux prêtres lévites, à. ceux de la famille de Sadduc, qui s'approchent de moi, dit le Seigneur Dieu, un veau choisi parmi le troupeau, afin de me le sacrifier pour le péché.
Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
20 Et ils prendront de son sang, et ils le mettront sur les quatre cornes de l'autel et sur les quatre angles du propitiatoire, et sur la base tout alentour, et ainsi ils le purifieront.
Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 Et ils prendront le veau offert pour le péché, et il sera brûlé par le feu, dans le lieu séparé du temple, hors du sanctuaire.
Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
22 Et le second jour ils prendront deux chevreaux sans tache pour le péché, et ils purifieront l'autel, comme ils l'auront purifié avec le veau.
“Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
23 Et lorsqu'ils auront achevé la purification, ils offriront un veau sans tache et un bélier sans tache.
Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
24 Et vous les offrirez devant le Seigneur; et les prêtres les saupoudreront de sel, et ils les offriront en holocauste au Seigneur.
Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
25 Pendant sept jours, tu offriras chaque jour pour le péché un chevreau, un veau et un bélier choisis parmi les bœufs et les brebis; et on sacrifiera ces victimes, toutes sans tache,
“Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
26 Durant sept jours. Et ils purifieront l'autel, ils le sanctifieront, et ils consacreront leurs mains.
Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
27 Et à partir du huitième jour et dans la suite les prêtres sacrifieront sur l'autel vos holocaustes et vos victimes pour le salut; et je vous agréerai, dit le Seigneur.
Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 43 >