< Ézéchiel 31 >

1 Et en l'année onzième, le troisième mois, le premier jour du mois, la parole du Seigneur me vint, disant:
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa tatu, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Fils de l'homme, dis au Pharaon, roi d'Égypte, et à son peuple: À qui t'es-tu comparé en ton orgueil?
“Mwanadamu, mwambie Farao, mfalme wa Misri, na watu wake wanaomzunguka, 'Katika ukuu wako, je! wewe ni kama nani?
3 Voilà qu'Assur était un cyprès du Liban, et il était beau par ses branches, par la hauteur de sa tige et par sa cime s'élevant au milieu des nuées.
Tazama! Ashuru ilikuwa mwerezi katika Lebanoni pamoja na matawi mazuri, yakitoa kivuli kwenye msitu, na mirefu katika kimo, na matawi yalitengeneza kilele cha mti wake.
4 Les eaux l'avaient nourri; l'abîme l'avait fait croître en conduisant ses fleuves autour de ses racines, et ses ondes se répandaient vers tous les arbres des champs.
Maji mengi yaliufanya kuwa mrefu; maji ya chini yaliufanya kuwa mkuba. Mito ilitiririka sehemu zake zote, kwa kuwa mifereji yake ilitoa kuelekea kwenye miti yote katika shamba.
5 Aussi dépassait-il en hauteur tous les arbres des champs, et ses rameaux s'étaient déployés, grâce à l'abondance des eaux.
Kimo chake kikubwa kilikuwa zaidi kuliko miti mingine yote katika shamba, na matawi yake yakawa mengi; matawi yake yalikuwa marefu kwa sababu ya maji mengi yalipokuwa yakikua.
6 Tous les oiseaux du ciel faisaient leurs nids dans ses branches, et toutes les bêtes des champs mettaient bas sous son feuillage, une multitude de nations habitaient sous son ombre.
Kila ndege wa mbinguni alitengeza kiota kwenye matawi yake, wakati kila kiumbe hai cha shamba kilizaa mtoto chini ya tawi. Mataifa mengi yote yaliishi chini ya kivuli chake.
7 Il était beau par sa grandeur et par la multitude de ses rameaux; car ses racines étaient arrosées d'une eau abondante.
Kwa kuwa ulikuwa uzuri katika ukuu wake na kimo cha matawi yake, kwa kuwa mizizi yake ilikuwa katika maji mengi.
8 Tels sont les cyprès du paradis de Dieu; les pins ne peuvent lui être comparés pour leurs rejetons; les sapins ne peuvent lui être comparés pour leurs rameaux; nul autre arbre du paradis de Dieu ne lui ressemble en beauté,
Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kuwa sawa nayo. Hakuna miongoni mwa miti ya mivinje iliyofanana matawi yake, na miti ya miamori haikuweza kuwa sawa na majani yake. Hapakuwa na mti mwingine katika bustani ya Mungu ulikuwa kama huo katika uzuri wake.
9 Pour la multitude de ses rameaux. Et les arbres du paradis de délices de Dieu lui portaient envie.
Nimeufanya kuwa mzuri pamoja na matawi yake mengi na miti yote ya Edeni iliyokuwa katika bustani ya Mungu ilimwonea wivu.
10 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: En punition de ce que tu as tant grandi, de ce que tu as élevé ta cime au milieu des nuées, et que je l'ai vu se glorifier ainsi,
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu ilikuwa mirefu kwa kina, na imekiweka kilele chake kati ya matawi yake, moyo wake umeinua kwa sababu ya urefu wake.
11 Je l'ai livré aux mains du prince des nations, et il a préparé sa ruine.
Nimeuweka kwenye mikono ya yeye mwenye uweza wa mataifa, kuishughulikia kulingana na yale maovu anayostahili. Nimeufukuza.
12 Et des hommes de pestilence, des étrangers, venus des nation l'ont détruit, et ils l'ont abattu sur les montagnes; ses rameaux sont tombés dans tous les vallons; sa tige a été brisée dans toutes les plaines de la terre, et tous les peuples des nations se sont retirés de son ombre, et ils l'ont rasé au niveau du sol.
Wageni waliokuwa wakiogofya wa mataifa yote wameikatilia mbali kuiacha ife. Matawi yake yameanguka kwenye milima na mabonde yote, na matawi yake yameanguka katika mito yote ya nchi. Kisha mataifa yote juu ya nchi wakatoka nje kutoka chini ya kivuli na kwenda zao wakamwacha.
13 Sur ses ruines se sont reposés tous les oiseaux du ciel, et toutes les bêtes des champs se sont blotties sous ses grosses branches;
Ndege wa agani watapumzika kwenye shina la mti ulioanguka, na kila mnyama wa shambani atakuja kwenye matawi yake.
14 Afin que nul des arbres qui croissent au bord des eaux ne se glorifiât de sa grandeur. Ils ont élevé leur cime au milieu des nues; mais ils ne se maintiendront pas en leur élévation; tous ces arbres, baignés des eaux, ont tous été donnés à la mort; ils iront tous au fond de la terre, au milieu des fils des hommes, avec ceux qui descendent à l'abîme.
Hii litokea ili kwamba pasiwe na miti mingine itakayopandwa karibu na maji yatang'oa majani yake hata kwenye kina cha miti mirefu, na kwamba hakuna miti mingine itakayomea karibu na maji itakayofikia kwenye hicho kina. Wote wametolewa kufa, chini ya nchi, miongoni mwa watoto wa binadamu, pamoja na wale washukao chini.
15 Et voici ce que dit le Seigneur Maître: Le jour où cet arbre est descendu aux enfers, l'abîme a pleuré sur lui. Et j'ai suspendu le cours de tous ses fleuves, et j'ai arrêté les grandes eaux qui l'arrosaient; et le Liban, à cause de lui, s'est couvert de ténèbres, et tous les arbres se sont affaissés de douleur. (Sheol h7585)
Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku wakati mkangazi uliposhuka chini nilileta maombolezo kwenye dunia. Niliyafunika maji ya chini juu yake, nikayarudisha maji ya bahari. Nilizuia maji makuu, nikaleta maombolezo hata Lebanoni kwa ajili yake. Hivyo miti yote ya shambani ikaomboleza kwa sababu yake. (Sheol h7585)
16 Au bruit de sa chute, les nations ont tremblé; car je l'ai fait descendre aux enfers avec ceux qui étaient tombés dans l'abîme; et tous les arbres de délices de la terre le consolaient, et tous les beaux arbres du Liban arrosés par les eaux. (Sheol h7585)
Nimeleta tetemeko kwa mataifa wa sauti ya kuanguka kwake, wakati nitakapomtupa chini mpaka kuzimu pamoja na wale walioenda chini kwenye shimo. Hivyo niliitia moyo miti ya Edeni yote katika pande zote za nchi. Hii ilikuwa imechaguliwa na miti iliyokuwa bora ya Lenanoni; miti iliyokunywa maji. (Sheol h7585)
17 Et ceux-là aussi sont descendus avec lui aux enfers, parmi les morts frappés par le glaive; et sa race, qui demeurait sous son abri, a péri au milieu de sa vie. (Sheol h7585)
Kwa kuwa walikwenda chini pia pamoja nayo hata kuzimu, kwa wale waliokuwa wameuawa kwa upanga. Kulikuwa na jeshi lake imara, yale mataifa yalikuwa yakiishi kati kivuli chake. (Sheol h7585)
18 À quoi te comparer? Descends; sois entraîné, avec tous les arbres de délices, au plus profond de la terre; tu seras étendu au milieu des incirconcis avec les morts frappés par le glaive. Tel sera le Pharaon, telle sera la multitude qui faisait sa force, dit le Seigneur Maître.
Umefanana na nani hivi katika utukufu na ukuu kati ya mti wa Edeni? Kwa kuwa utashushwa chini pamoja na miti ya Edeni hata pande zote nne za dunia miongoni mwa wasiotahiriwa; utaishi pamoja na watu wake wote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavy.”

< Ézéchiel 31 >