< Ézéchiel 3 >
1 Et l'esprit me dit: Fils de l'homme, mange ce rouleau et pars, et parle aux fils d'Israël.
Akanambia, “Mwanadamu, kile ulichokikuta, kula. Kula hili gombo, kisha nenda kaongee na nyumba ya Israeli.”
2 Et il m'ouvrit la bouche, et il me fit manger le rouleau.
Basi nikafungua kinywa changu, na akanilisha hilo gombo.
3 Et il me dit: Fils de l'homme, ta bouche mangera, et tes entrailles seront rassasiées de ce rouleau qui t'est donné. Et je le mangeai, et il fut à ma bouche comme du miel le plus doux.
Akanambia, “Mwana wa adamu, lisha tumbo lako na jaza tumbo lako kwa hili gombo ambalo nimekupa!” Basi nikalila, na lilikuwa tamu kama asali kwenye mdomo wangu.
4 Et l'esprit me dit: Fils de l'homme, pars et va trouver la maison d'Israël, et répète-leur mes paroles.
Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, nenda kwenye nyumba ya Israeli na ongea maneno yangu kwao.
5 Car c'est à la maison d'Israël que je t'envoie, et non à un peuple qui parle une langue inconnue,
Kwa kuwa hujatumwa kwa watu wenye maneno ya kushangaza au lugha ngumu, lakini kwa nyumba ya Israeli-
6 Ni à maintes nations parlant d'autres langues, des langues étrangères, difficiles, inintelligibles pour toi; et quand même je t'aurais envoyé à de tels peuples, ils t'écouteraient encore.
sio kwa taifa lenye nguvu ya maneno ya ajabu au lugha ngumu ambao maneno yao hutaweza kuyaelewa! Kama nikikutuma kwao, watakusikiliza.
7 Mais la maison d'Israël ne voudra pas t'écouter; car ils ne veulent pas m'écouter moi-même, parce que toute la maison d'Israël est opiniâtre et a le cœur endurci.
Lakini nyumba ya Israeli haitakuwa tayari kukusikiliza, kwa kuwa hawako tayari kunisikiliza mimi. Hivyo nyumba yote ya Israeli ni paji gumu na moyo mgumu.
8 Et voilà que j'ai fait ta face puissante devant leurs faces, et j'affermirai en toi un pouvoir plus fort que leur pouvoir,
Kumbe nimeufanya uso wako kama kaidi kama nyuso zao na paji lako kuwa gumu kama mapaji yao.
9 Et qui sera toujours plus ferme qu'un rocher. Ne les crains pas, ne tremble pas devant leur visage; car c'est une maison qui m'irrite.
Nimekufanya paji lako kama almasi, gumu kuliko jiwe la kiberiti! Usiwaogope wala kufadhaika kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba ya uasi.”
10 Et l'esprit me dit: Fils de l'homme, toutes les paroles que je t'ai dites, reçois-les dans ton cœur, entends-les de tes oreilles.
Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, maneno yote niliyokutangazia-yachukue kwenye moyo wako na wasikize kwa sikio lako!
11 Et pars, va parmi les captifs près des fils de mon peuple; parle-leur et dis: Voici ce que dit le Seigneur; pour voir si par hasard ils t'écouteront, si par hasard ils rentreront en eux-mêmes.
Kisha nenda kwa watumwa, kwa watu wako, na uzungumze nao. Waambie, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo; iwapo watasikia au hapana.”
12 Et l'esprit me saisit, et j'entendis derrière moi une voix, comme le bruit d'un grand tremblement de terre, disant: Bénie soit la gloire du Seigneur du lieu où il réside.
Kisha Roho akaniinua juu, na nikasikia nyuma yangu sauti yenye tetemeko la aridhi: “Ubarikiwe utukufu wa Yahwe kutoka mahali pake!”
13 Et je recueillis le bruit des ailes des quatre animaux ailés, battant l'une contre l'autre, et la voix semblable à un tremblement de terre.
Ilikuwa sauti ya mabawa ya viumbe hai vilipokuwa vikigusana kila kimoja, na sauti ya magurudumu ambayo yalikuwa pamoja na hivyo viumbe, na sauti ya tetemeko kubwa arithi.
14 Et l'esprit me souleva, et il me ravit, et je m'en allai soulevé par l'impulsion de mon propre esprit, et la main puissante du Seigneur était sur moi.
Roho akaniinua juu na kunichukua, Nikaenda kwa uchungu katika hasira kali rohoni mwangu, kwa kuwa mkono wa Yahwe ulikuwa na nguvu ukigandamiza juu yangu!
15 Et je traversai l'air, et j'arrivai parmi les captifs, et je parcourus les demeures de ceux qui étaient sur le fleuve Chobar. Et je restai là sept jours, allant et venant au milieu d'eux.
Hivyo nikaenda kwa watumwa huko Tel Abibu waliokuwa wakiishi karibu na Kebari Kanali, na niliishi miongoni mwao huko kwa mda wa miaka saba, kushinda kabisa katika mshangao.
16 Et après sept jours la parole du Seigneur me vint, disant:
Kisha ikatokea baada ya siku saba kwamba neno la Yahwe likanijia, likisema,
17 Fils de l'homme, je t'ai mis en sentinelle parmi la maison d'Israël, et tu entendras la parole de ma bouche, et tu les menaceras en mon nom.
“Mwana wa adamu, nimekufanya uwe mwangalizi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, hivyo sikiliza neno kutoka kinywani mwangu, na uwapatie onyo langu.
18 Quand tu diras de ma part à l'impie: Tu mourras de mort; si tu ne lui enjoins pas de faire effort sur lui-même pour se détourner de ses voies afin qu'il vive, cet impie mourra dans son iniquité, et je réclamerai son sang de ta main.
Nitakaposema kwa waovu, 'Utakufa hakika' na usimuonye au kuzungumza onyo kwa waovu kuhusu matendo yao maovu hivyo anaweza kuishi-yule muovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
19 Mais si tu as averti l'impie, et qu'il ne se soit détourné ni de son impiété ni de sa voie, cet impie mourra dans son iniquité, et toi tu auras sauvé ton âme.
Lakini kama ukimuonya muovo, na asiuache uovu wake au kutoka matendo yake maovu, kisha atakufa kwa dhambi yake, lakini utaokoa maisha yako mwenyewe.
20 Et quand le juste se détournera de la justice et fera une faute, je lui mettrai le châtiment devant la face; et il mourra parce que tu ne l'auras point averti; et il mourra dans ses péchés; car je ne garderai plus la mémoire de ses actes de justice, et je réclamerai son sang de ta main.
Kama mwenye haki ataicha haki yake na kutenda yasiyohaki, na nikaweka kizuizi mbele yake, atakufa. Kwasababu hukumuonya, atakufa katika dhambi yake, na sintokumbuka matendo ya haki aliyoyafanya, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
21 Mais si tu as enjoint au juste de ne pas pécher, et s'il ne pèche plus, le juste vivra, parce que tu l'auras averti, et toi tu auras sauvé ton âme.
Lakini kama ukimuonya mwenye mtu mwenye haki kuacha kufanya dhambi halafu akaacha kutenda dhambi, ataishi hakika tangu alipo unywa; na utakuwa umeokoa maisha yako mwenyewe.”
22 Et la main du Seigneur vint sur moi, et il me dit: Lève-toi, et sors dans la plaine, et là il te sera parlé.
Hivyo mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu huko, akanambia, “Inuka! nenda uwandani, na nitaongea na wewe huko!”
23 Et je me levai et je sortis dans la plaine, et voilà que la gloire du Seigneur s'y tenait, pareille à la vision et à la gloire du Seigneur que j'avais vue sur le fleuve Chobar. Et je tombai la face contre terre.
Nikainuka na kwenda uwandani, na huko utukufu wa Yahwe ulisimama, kama utukufu ambao niliokuwa nimeuona karibu na Kebari Kanali; hivyo nikaanguka kifudifudi.
24 Et un esprit vint en moi, et il me remit sur mes pieds, et il parla et me dit: Rentre, et enferme-toi au milieu de ta maison.
Roho akaja kwangu na kusimama juu ya miguu yangu; akaongea na mimi, na kunambia, “Nenda na jifungie mwenyewe kwenye nyumba yako,
25 Et toi, fils de l'homme, voilà que des chaînes sont préparées pour toi, et ils te chargeront de ces chaînes, et tu n'en sortiras point.
kwa sasa, mwana wa adamu, wataweka kamba juu yako na kukufunga ili usiweze kutoka nje miongoni mwao.
26 Et je te nouerai la langue, et tu seras muet, et tu ne seras plus pour eux un reproche vivant; car c'est une maison qui m'irrite.
Nitaufanya ulimi wako ugandamane na paa ya mdomo wako, ili kwamba uwe kimya, na hutaweza kuwakemea, kwa kuwa ni nyumba ya waasi.
27 Mais quand je t'aurai parlé, je t'ouvrirai la bouche et tu leur diras: Voilà ce que dit le Seigneur: Que celui qui vaut écouter écoute; que celui qui veut désobéir désobéisse; car c'est une maison qui m'irrite.
Lakini nitakapozungumza na wewe, nitafungua mdomo wako hivyo utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.' Yeye asikiaye na asikie; yeye asiyesikia na asisikie, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi!”