< Ézéchiel 24 >

1 Et la parole du Seigneur vint à moi, en la neuvième année, le dixième mois, le dixième jour du mois, disant:
Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils de l'homme, à partir de ce jour où le roi de Babylone a fait tomber sa colère sur Jérusalem, à partir d'aujourd'hui, écris pour toi chaque jour;
“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
3 Et parle en parabole à cette maison qui m'irrite, et dis-lui: Ainsi parle le Seigneur: Mets sur le feu une chaudière et verses-y de l'eau;
Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
4 Et jettes-y des parts de victimes, des parts de choix, de la cuisse et de l'épaule réservées, la chair séparée des os,
Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
5 Et prises des bêtes choisies; et brûle les os sous les chairs. La chaudière a bouillonné, et les os ont cuit au milieu.
chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
6 Voici donc ce que dit le Seigneur: Malheur à toi, ville de sang! tu es la chaudière où il y a de la rouille, et la rouille n'en est point partie; cette ville a offert des parts de victimes, et le sort n'est pas tombé sur elle.
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
7 Parce que son sang est au milieu d'elle, je l'ai posé sur une pierre lisse; je ne l'ai point répandu sur la terre où il aurait été caché,
“‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
8 Afin que ma colère éclate et châtie; j'ai mis le sang sur une pierre lisse, de peur qu'il ne soit caché.
Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
9 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Et moi j'agrandirai le foyer.
“‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
10 Et je prodiguerai le bois, et j'y mettrai le feu, afin que les chairs soient consumées, et que le jus se réduise,
Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
11 Et que la chaudière pose sur les braises, que son airain s'échauffe et devienne brûlant, qu'il entre en fusion au milieu de son impureté, et que la rouille soit consumée.
Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
12 Et la rouille qui abonde en elle ne sortira pas d'elle.
Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
13 Et sa rouille sera hideuse, en punition de ce que tu t'es souillée. Et pourquoi ne resterais-tu pas impure, jusqu'à ce que j'aie assouvi ma colère?
“‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
14 C'est moi, le Seigneur, qui ai parlé, et le jour viendra où j'exécuterai, et je ne ferai pas de distinction, et je serai sans pitié. Selon tes voies et selon tes imaginations je te jugerai, dit le Seigneur. À cause de cela, je te jugerai selon le sang que tu as versé; je te jugerai selon les idoles que tu as adorées, toi impure, toi fameuse et féconde en moyens de m'irriter.
“‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
15 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
16 Fils de l'homme, voilà que je vais te prendre par violence les délices de tes yeux; mais tu ne te lamenteras point, tu ne pleureras point.
“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
17 Tu auras un soupir de sang, une douleur de reins; tes cheveux sur la tête ne seront point tressés, et tes sandales ne seront point à tes pieds; nulle lèvre ne te consolera, et tu ne mangeras pas le pain des hommes.
Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
18 Et je parlai au peuple le matin, comme le Seigneur me l'avait prescrit le soir; et je fis le matin même ce qui m'était commandé.
Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
19 Et le peuple me dit: Ne nous expliques-tu pas pourquoi tu agis ainsi?
Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
20 Et je leur répondis: La parole du Seigneur m'est venue, disant:
Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
21 Dis à la maison d'Israël: Ainsi parle le Seigneur: Voilà que je vais profaner mon sanctuaire, l'orgueil de ta force, les délices de tes yeux, et pour lequel vous tremblez de toutes vos âmes. Vos fils et vos filles que vous aurez laissés périront par le glaive.
‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
22 Et vous ferez comme je viens de faire: nulle bouche ne vous consolera, et vous ne mangerez pas le pain des hommes.
Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
23 Et vos cheveux sur votre tête et vos sandales à vos pieds seront comme les miens; vous ne vous lamenterez point, vous ne pleurerez point, et vous vous consumerez en vos iniquités, et chacun de vous invoquera son frère.
Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
24 Et Ézéchiel sera pour vous un signe; vous ferez comme je viens de faire, lorsque ces choses arriveront; et vous saurez que je suis le Seigneur.
Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
25 Et toi, fils de l'homme, n'est-ce pas le jour où je leur prendrai ce qui fait leur force, le sujet de leur orgueil, les délices de leurs yeux, la joie de leur âme, leurs fils et leurs filles,
“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
26 N'est-ce pas ce jour-là qu'un homme échappé à la mort viendra te trouver et te parler à l'oreille?
siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
27 Ce jour-là ta bouche s'ouvrira pour parler à cet homme sauvé; et tu ne seras pas muet plus longtemps, et tu seras pour eux un signe; et ils sauront que je suis le Seigneur.
Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”

< Ézéchiel 24 >