< Ézéchiel 21 >
1 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 À cause de cela, prophétise, fils de l'homme, tourne ton visage contre Jérusalem, et regarde ses lieux saints, et prophétise contre la terre d'Israël.
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 Et dis à la terre d'Israël: Ainsi parle le Seigneur: Voilà que je suis contre toi, et je tirerai le glaive du fourreau, et j'exterminerai parmi-toi l'injuste et le pécheur.
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Et parce que j'exterminerai en toi l'injuste et le pécheur, mon glaive sortira du fourreau, contre toute chair, de l'orient à l'aquilon.
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 Et toute chair saura que moi, le Seigneur, j'aurai tiré le glaive du fourreau, et je ne le remettrai plus.
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 Et toi, fils de l'homme, pousse des soupirs à te rompre les reins; et en tes douleurs gémis devant leurs yeux.
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 Et s'ils te disent: Pourquoi gémis-tu? réponds: À cause d'une nouvelle, parce que l'ennemi vient; et tout cœur sera brisé, et toutes mains seront énervées; et toute chair, tout souffle seront défaillants, et tous genoux souillés d'humeurs; car voilà qu'il vient, dit le Seigneur.
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 Fils de l'homme, prophétise, et dis: Ainsi parle le Seigneur: Dis: Glaive, glaive, aiguise-toi, et mets-toi en fureur,
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 Pour égorger des victimes; aiguise-toi pour briller; prépare-toi pour tout affaiblir. Égorge, anéantis, abats tout arbre.
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 Et il l'a préparé pour le tenir en sa main. Le glaive est aiguisé, il est préparé pour être dans la main de celui qui transperce.
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Pousse des cris et des hurlements, fils de l'homme; car ce glaive est venu sur mon peuple, il est venu sur tous les princes d'Israël; ils seront comme des passagers; le jugement avec le glaive est venu sur mon peuple. C'est pourquoi bats des mains.
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 Car il est condamné. Et qu'arrivera-t-il, si la famille entière est répudiée? Cela ne sera pas, dit le Seigneur Maître.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 Et toi, fils de l'homme, prophétise et bats des mains; prends deux glaives; et prends-en un troisième, le glaive, le grand glaive des tués. Mets-les hors d'eux-mêmes;
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 De peur que leur cœur ne se brise, et que les malades ne se multiplient auprès de toutes les portes; c'est par le glaive qu'ils doivent périr; il est tout prêt à les égorger; il est tout prêt à resplendir.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Accours, glaive, aiguise-toi à droite, aiguise-toi à gauche, aiguise-toi sur toutes tes faces.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 Et moi aussi, je battrai des mains, et j'assouvirai ma colère; c'est moi, le Seigneur, qui ai parlé.
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 Et toi, fils de l'homme, représente-toi deux voies par où entrera le glaive du roi de Babylone. Toutes les deux partiront d'une même contrée; et il y aura une main à l'extrémité du chemin de la ville; tu la traceras à l'extrémité du chemin,
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Par où le glaive entrera pour attaquer Rabbath, l'un des fils d'Ammon, puis la Judée, et au milieu Jérusalem.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 Car le roi de Babylone s'arrêtera sur le vieux chemin, à la tête des deux chemins; attendant que les devins prennent les augures, que l'eau bouillante rejette une baguette, que l'on consulte les idoles, et que l'on interroge à droite le foie des victimes.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 Et la divination a été faite contre Jérusalem; et le roi y plantera des palissades, il ouvrira la bouche pour crier, et il poussera une voix formidable; il plantera des palissades devant les portes de la ville, il fera des levées de terre, et il établira des balistes.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 Cependant à leurs yeux il ne sera pour eux qu'un devin prenant les augures; mais il se rappellera les iniquités de leur prince.
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 C'est pourquoi voici ce que dit le Seigneur: Parce que vous lui avez donné occasion de se rappeler le souvenir de votre iniquité, en dévoilant votre impiété, en faisant voir vos péchés: à cause de toutes vos impiétés et de vos idoles, en punition des crimes que vous lui avez rappelés, vous périrez.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 Et toi, profane, impie roi d'Israël, dont le jour est venu, le jour marqué comme terme à ton iniquité,
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 Voici ce que dit le Seigneur: Tu lui as ôté la tiare, tu as mis à sa place ta couronne, et il n'y en aura plus de pareille; tu as abaissé ce qui était haut; tu as élevé ce qui était bas.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 À cette couronne j'imputerai iniquité, iniquité, iniquité. Malheur à elle! telle elle restera, jusqu'à ce que vienne celui à qui elle est destinée, et je la lui livrerai.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 Et toi, fils de l'homme, prophétise et dis: Ainsi parle le Seigneur aux fils d'Ammon pour leur opprobre: Glaive, glaive, tiré pour le carnage, et tiré pour la destruction, lève-toi pour briller!
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 Pendant ta vision vaine, ô Ammon, pendant ta fausse divination, glaive, anime-toi pour frapper au col les impies dont le jour est venu, le jour marqué comme terme à l'iniquité d'Ammon!
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 Rentre dans le fourreau; mais tu ne trouveras pas le repos au lieu où tu es né; je te jugerai en ta propre terre.
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 Et je ferai tomber ma colère sur toi; je soufflerai contre toi dans le feu de ma colère, et je te livrerai aux mains d'hommes barbares, habiles à porter avec eux la destruction.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 Tu seras la pâture du feu; ton sang sera au milieu de ta terre, et il ne restera de toi aucun souvenir; car c'est moi, le Seigneur, qui ai parlé.
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”