< Ézéchiel 19 >

1 Et toi, chante une lamentation sur le prince d'Israël;
“Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
2 Et dis: Pourquoi ma mère est-elle devenue une jeune lionne au milieu des lions? Pourquoi, au milieu des lions, a-t-elle multiplié ses lionceaux?
na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
3 Et un de ses lionceaux s'est élancé, et il est devenu lion, et il a appris à ravir sa proie, et il a dévoré des hommes.
Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
4 Et les nations en ont ouï parler, et il a été pris comme il les détruisait, et elles l'ont emmené, dans un filet, en la terre d'Égypte.
Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
5 Et la lionne, ayant vu qu'il était séparé d'elle, et que son espérance en lui avait péri, prit un autre de ses lionceaux, et le fit lion.
“‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
6 Et celui-ci se montra au milieu des lions, et il devint lion, et il apprit à ravir sa proie, et il dévora des hommes.
Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
7 Et il se reput en son audace, et il dépeupla les villes de la voix de ses rugissements; et il désola la terre et ce qui la remplit.
Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
8 Et les peuples des royaumes l'entourèrent, et ils tendirent contre lui leurs filets, et pendant qu'il les détruisait il fut pris.
Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
9 Et on le mit dans une cage de fer, enveloppé de son filet; et il arriva chez le roi de Babylone, qui le jeta en prison, afin qu'on n'entendit plus sa voix sur la montagne d'Israël.
Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
10 Ta mère est comme une vigne et comme une fleur de grenadier planté au bord des eaux; son fruit et ses bourgeons ont crû dans l'abondance de l'eau.
“‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
11 Mais elle est devenue une verge pour la tribu des rois, et elle s'est élevée dans sa grandeur, au milieu des autres tiges. Et elle a vu sa grandeur en la multitude de ses rameaux.
Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
12 Et elle a été brisée avec fureur; elle a été jetée à terre, et un vent brillant a flétri ses meilleures branches; ils se sont vengés d'elle, et la verge de sa puissance a été desséchée. Le feu l'a dévorée.
Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
13 Et maintenant on l'a plantée dans le désert en une terre aride.
Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
14 Et une flamme est sortie d'une verge de ses meilleurs rameaux, et elle l'a dévorée, et elle n'eut plus la verge de sa puissance. Sa race est devenue une parabole de lamentation, une lamentation que l'on chantera.
Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”

< Ézéchiel 19 >