< Exode 9 >

1 Le Seigneur dit alors à Moise: Entre chez le Pharaon; dis-lui: Voici ce que dit le Seigneur Dieu des Hébreux: Renvoie mon peuple, afin qu'il m'offre un sacrifice.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
2 Si tu refuses de renvoyer mon peuple, si tu le retiens encore,
Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
3 La main du Seigneur s'appesantira sur le bétail de tes champs, sur les chevaux, tes ânes, tes chamelles, tes bœufs et tes brebis; la mortalité sera grande et terrible.
mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
4 Et je montrerai avec éclat la différence entre le bétail des Égyptiens et celui des fils d'Israël; nulle bête ne mourra parmi celles des fils d'Israël.
Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
5 Dieu a même fixé le temps; il a dit: Dans la journée de demain le Seigneur accomplira sur la contrée cette menace.
Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
6 Le lendemain, le Seigneur tint parole, et tout le bétail des Égyptiens mourut; mais rien ne périt parmi les bestiaux des fils d'Israël.
Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
7 Et le Pharaon même après avoir vu que parmi les bestiaux des fils d'Israël, rien n'avait péri, s'endurcit le cœur; il ne renvoya pas le peuple.
Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
8 Le Seigneur alors parla à Moïse et à son frère, disant: Prenez plein vos mains de la cendre de fournaise, et que Moïse la jette en l'air devant le Pharaon et ses serviteurs.
Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
9 Qu'elle forme un tourbillon de poussière sur toute la terre d'Égypte; et il y aura sur les hommes de l'Égypte, et sur les quadrupèdes, des ulcères et des tumeurs enflammées.
Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
10 Ils prirent donc de la cendre de forge devant le Pharaon; Moïse la jeta en l'air, et il vint aux hommes ainsi qu'aux quadrupèdes, des ulcères et des tumeurs enflammées.
Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
11 Les magiciens eux-mêmes ne purent demeurer en présence de Moïse, à cause des ulcères, car il vint des ulcères aux magiciens dans toute l'Égypte.
Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
12 Et le Seigneur endurcit le cœur du Pharaon; il n'écouta ni Aaron ni Moïse, ainsi que l'avait dit le Seigneur.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
13 Après cela, le Seigneur dit à Moïse: Lève-toi de grand matin, et présente-toi devant le Pharaon, et dis lui: Voici ce que dit le Seigneur Dieu des Hébreux: Renvoie mon peuple, afin qu'il m'offre un sacrifice.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
14 Car, en ce moment, je fais tomber sur ton cœur, sur celui de tes serviteurs et sur celui de ton peuple, tous mes coups, afin que tu voies que nul sur la terre n'est semblable au Seigneur.
au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
15 Aussitôt que j'aurai laissé tomber ma main, je le frapperai, et je ferai périr ton peuple, et il sera effacé de la terre.
Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
16 Tu n'as été conservé qu'afin que je montre en toi ma force, et pour que mon nom soit révélé à toute la terre.
Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
17 Quoi donc! tu insultes encore mon peuple en refusant de le renvoyer!
Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
18 Eh bien, moi, dès demain, à pareille heure, je ferai tomber une grêle abondante, telle qu'il n'y en a jamais eu en Égypte, depuis le jour de sa fondation jusqu'à aujourd'hui.
Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
19 Hâte-toi d'abriter tout le bétail que tu as aux champs, car les hommes et les bestiaux qui se trouveront aux champs, et qui ne seront pas rentrés, seront surpris par la grêle et périront.
Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
20 Ceux des serviteurs du Pharaon qui craignaient la parole de Dieu rassemblèrent leurs bestiaux en leurs demeures.
Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
21 Ceux qui ne faisaient aucune attention à la parole du Seigneur, laissèrent leur bétail aux champs.
Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
22 Et le Seigneur dit à Moïse: Étends la main vers la ciel, et la grêle tombera sur toute la terre d'Égypte, sur les hommes, sur les bestiaux et sur toutes les plantes qui couvrent la terre.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
23 Moïse étendit donc la main vers le ciel, et le Seigneur envoya tonnerre et grêle; le feu parcourut la terre, et le Seigneur fit tomber une pluie de grêle sur toute la terre d'Égypte.
Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
24 La grêle tombait mêlée de flammes; elle était terriblement épaisse, telle qu'il n'y en avait jamais eu en Égypte depuis que la nation s'y était établie.
mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
25 Tout fut donc frappé par la grêle dans toute l'étendue de l'Égypte, depuis l'homme jusqu'aux bestiaux. Toute l'herbe des champs fut frappée par la grêle; et tous les arbres des campagnes furent brisés par elle.
Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
26 Excepté dans la terre de Gessen, où étaient les fils d'Israël; là il n'y eut point de grêle.
Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
27 Et le Pharaon fit appeler Moïse et son frère, et il leur dit: J'ai péché jusqu'à cette heure; le Seigneur est juste; mon peuple et moi nous sommes des impies.
Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
28 Priez donc pour moi le Seigneur, pour faire cesser la voix de Dieu, la grêle et les flammes, et je vous congédierai, et vous ne continuerez plus de demeurer ici.
Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
29 Moïse répondit: Aussitôt sorti de la ville, j'étendrai les mains vers le Seigneur, et les voix cesseront; la grêle et la pluie s'arrêteront, et tu connaîtras que la terre est au Seigneur.
Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
30 Mais je sais que ni toi, ni tes serviteurs, vous ne craignez point le Seigneur encore.
Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
31 Or, le lin et l'orge avaient été frappés, car l'orge était levée et le lin était monté en graine.
(Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
32 Mais le froment et l'épeautre n'avaient pas été frappés, parce qu'ils étaient tardifs.
Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
33 Moïse, ayant quitté le Pharaon et la ville, étendit les mains vers le Seigneur, et les voix cessèrent, et il n'y eut plus sur la terre ni grêle ni pluie
Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
34 Le Pharaon ayant vu que les voix, et la grêle et la pluie avaient cessé, continua de pécher, et il endurcit son cœur, et le cœur des hommes de sa maison.
Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
35 S'étant ainsi endurci le cœur, le Pharaon refusa de congédier les fils d'Israël, ainsi que le Seigneur l'avait dit à Moïse.
Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.

< Exode 9 >