< Exode 33 >

1 Le Seigneur dit alors là Moïse: Pars, quitte ce lieu, toi et ton peuple que tu as tiré de la terre d'Égypte; va jusqu'à la terre que j'ai promise â Abraham, à Isaac, à Jacob, quand je leur ai dit: Je la donnerai à votre race.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Ondoka mahali hapa, wewe pamoja na hao watu uliowapandisha kutoka Misri, mpande mpaka nchi niliyomwahidi Abrahamu, Isaki na Yakobo kwa kiapo, nikisema, ‘Nitawapa wazao wenu nchi hii.’
2 J'enverrai mon ange devant la face, et il chassera l’Amorrhéen, le Hettéen, le Phérézéen, le Gergéséen, l'Évéen, le Jébuséen et le Chananéen.
Nitamtuma malaika mbele yenu, naye atawafukuza Wakanaani, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
3 Je t'introduirai dans la terre où coulent le lait et le miel, mais je ne marcherai point avec toi; parce que tu as un peuple revêche et que je craindrais de te faire périr sur la route.
Pandeni mwende katika nchi itiririkayo maziwa na asali. Lakini mimi sitakwenda pamoja nanyi, kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu, nisije nikawaangamiza njiani.”
4 Le peuple, ayant ouï cette parole menaçante, pleura amèrement.
Watu waliposikia habari hizo za huzuni, wakaanza kuomboleza wala hakuna mtu aliyevaa mapambo yoyote.
5 Et le Seigneur dit aux fils d’Israël: Vous êtes un peuple revêche, prenez garde que je ne laisse tomber sur vous une nouvelle plaie et que je ne vous extermine; quittez donc vos vêtements de gloire et votre parure, et je vous montrerai ce que je veux faire pour vous.
Kwa kuwa Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni watu wenye shingo ngumu. Kama ningefuatana nanyi hata kwa muda mfupi, ningewaangamiza. Sasa vueni mapambo yenu, nami nitaamua nitakalowatendea.’”
6 Les fils d'Israël ôtèrent leurs robes ainsi que leurs parures, en s'éloignant du mont Horeb.
Hivyo Waisraeli wakavua mapambo yao katika Mlima wa Horebu.
7 Moïse prit à part son tabernacle, et il le dressa hors du camp, à une grande distance, et il fut nommé tabernacle du témoignage; et quiconque cherchait le Seigneur sortait et venait auprès du tabernacle, hors du camp.
Basi Mose alikuwa na desturi ya kuchukua hema na kuliweka wakfu nje ya kambi umbali kiasi, akaliita “Hema la Kukutania.” Kila aliyekuwa akiulizia shauri kwa Bwana, angelikwenda katika Hema la Kukutania nje ya kambi.
8 Lorsque Moïse entrait dans le tabernacle, hors du camp, tout le peuple se tenait chacun devant la porte de sa tente, les yeux fixés sur Moïse, jusqu'à ce qu'il fût entré dans le tabernacle.
Wakati wowote Mose alipokwenda kwenye Hema, watu wote waliinuka na kusimama kwenye maingilio ya mahema yao, wakimwangalia Mose mpaka aingie kwenye Hema.
9 Or, dès que Moïse était entré dans le tabernacle, une colonne de nuée descendait et s'arrêtait vers la porte, et elle parlait à Moïse.
Kila mara Mose alipoingia ndani ya hema, nguzo ya wingu ingeshuka chini na kukaa kwenye ingilio, wakati Mungu akizungumza na Mose.
10 Tout le peuple voyait la colonne de nuée devant la porte du tabernacle, et tout le peuple debout adorait, chacun de la porte de sa tente.
Kila mara watu walipoona hiyo nguzo ya wingu ikiwa imesimama kwenye ingilio la hema, wote walisimama wakaabudu, kila mmoja kwenye ingilio la hema lake.
11 Et le Seigneur parlait à Moïse face à face, comme, on parle à son propre ami. Moïse revenait ensuite au camp; et son serviteur Josué, jeune homme, fils de Nau, ne sortait pas du tabernacle.
Bwana angezungumza na Mose uso kwa uso, kama vile mtu azungumzavyo na rafiki yake. Kisha Mose angerudi kambini, lakini msaidizi wake kijana Yoshua mwana wa Nuni hakuondoka mle Hemani.
12 Moïse dit au Seigneur: Vous m'avez dit: Conduis ce peuple, et vous ne m'avez point montré celui que vous m’enverrez pour m'accompagner, mais vous m'avez dit: Je te connais avant tous les autres, et tu as trouvé grâce, devant moi.
Mose akamwambia Bwana, “Umekuwa ukiniambia, ‘Ongoza watu hawa,’ lakini hujanifahamisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Umesema, ‘Ninakujua wewe kwa jina lako, nawe umepata kibali mbele zangu.’
13 Si donc j'ai trouvé grâce devant vous, montrez-vous à moi; que je vous voie véritablement, afin que réellement je trouve grâce devant vous, et que je sois assuré que vous avez choisi pour votre peuple cette grande nation.
Ikiwa umependezwa nami, nifundishe njia zako ili nipate kukujua, nami nizidi kupata kibali mbele zako. Kumbuka kuwa taifa hili ni watu wako.”
14 Et le Seigneur répondit: Moi-même je marcherai devant toi et je te ferai trouver le repos.
Bwana akajibu, “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”
15 Moïse reprit: Si vous-même ne marchez point avec moi, ne me faites pas partir d'ici.
Kisha Mose akamwambia, “Kama Uso wako hauendi pamoja nasi, usituondoe hapa.
16 Comment, en effet, sera-t-il manifeste que moi et le peuple, avons trouvé grâce devant vous, si vous ne marchez pas avec nous? Mais si vous m'accompagnez moi et votre peuple, nous serons glorifiés aux yeux de toutes les nations qui sont sur la terre.
Mtu yeyote atajuaje kuwa mimi pamoja na watu wako tumepata kibali mbele zako, usipokwenda pamoja nasi? Ni nini kingine kitakachoweza kututofautisha mimi na watu wako miongoni mwa watu wengine wote walio katika uso wa dunia?”
17 Le Seigneur dit alors à Moïse: Je ferai ce que tu demandes; car tu as trouvé grâce devant moi, et je te connais avant tous.
Bwana akamwambia Mose, “Nitakufanyia jambo lile uliloomba, kwa sababu ninapendezwa nawe, nami ninakujua kwa jina lako.”
18 Moïse ajouta: montrez-vous donc vous-même à moi.
Kisha Mose akasema, “Basi nionyeshe utukufu wako.”
19 Et le Seigneur reprit: Je passerai devant toi dans ma gloire, et je prononcerai mon nom: Le Seigneur, devant toi, j'aurai pitié de qui j'aurai pitié, et je ferai miséricorde à qui je ferai miséricorde.
Ndipo Bwana akasema, “Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza Jina langu, Bwana, mbele ya uso wako. Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”
20 Et le Seigneur ajouta: Tu ne peux voir mon visage; car nul homme, en voyant mon visage, ne vivra.
Lakini Mungu akasema, “Hutaweza kuuona uso wangu, kwa kuwa hakuna mtu yeyote awezaye kuniona akaishi.”
21 Et le Seigneur dit: Vois ce lieu, près de moi, tu te tiendras sur cette pierre.
Kisha Bwana akasema, “Kuna mahali karibu nami ambapo unaweza kusimama juu ya mwamba.
22 Lorsque passera ma gloire, je te mettrai dans l'enfoncement du rocher, et je t'ombragerai de ma main jusqu’à ce que j'aie passé.
Utukufu wangu unapopita, nitakuweka gengeni kwenye mwamba na kukufunika kwa mkono wangu mpaka nitakapokwisha kupita.
23 Puis, j'ôterai ma main, et alors tu me verras par derrière; mais mon visage ne sera pas vu par toi.
Kisha nitaondoa mkono wangu nawe utaona mgongo wangu; lakini kamwe uso wangu hautaonekana.”

< Exode 33 >